Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. DKT. CHARLES J. TIZEBA: Mheshimiwa Spika, nyavu za kuvulia dagaa milimita sita zimezuiliwa Tanzania lakini Kenya na Uganda zinatumika bila kuhojiwa na Ziwa Victoria ni lile lile. Jambo hili si sawa, litazamwe upya.

Mheshimiwa Spika, operations zinazofanyika hazipati maelekezo ya awali ya AG. Ni vyema Mwanasheria Mkuu wa Serikali akatoa maelekezo mahsusi kwa watendaji hawa ili utekelezaji wa sheria ufanyike bila kuonea wananchi. Kwa mfano, makosa ya uvuvi kutolewa adhabu za mazingira, rushwa na wizi wa waziwazi unafanyika.

Mheshimiwa Spika, ufugaji wa samaki kwa vizimba umegubikwa bado na urasimu mkubwa. Leseni ni nyingi, masharti ni magumu sana kwa wananchi wa kawaida. Hivi kwanini zana za kutengenezea vizimba hazipo/haziruhusiwi hapa nchini? Wizara inaniapa vibali kuagiza toka Kenya mara kwa mara, hii ni aibu. Utaratibu ufanyike, wawepo wauzaji maalum wa zana hizi.

Mheshimiwa Spika, Soko la Samaki la Nyakarilo hadi leo halijafunguliwa. Naomba katika kuhitimisha hoja itangazwe kufunguliwa kwa soko hilo.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.