Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Rose Kamili Sukum

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ROSE K. SUKUM: Mheshimiwa Spika, Fungu 99 Sekta ya Mifugo. Changamoto kubwa ni migogoro inayowahusisha wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi pamoja na sheria kandamizi kwa wafugaji ambayo hutumiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Spika, ng’ombe wakiingia kwenye hifadhi wanakamatwa na kutaifishwa, kutozwa fine kila ng’ombe mmoja Shs. 100,000; mchungaji hutozwa fine ya laki 300,000/= na mwenye ng’ombe kufungwa.

Mheshimiwa Spika, kwafano mfugaji Wambura wa Serengeti alipigwa fine ya shs. 5,000,000/=, kifungo miaka mitano na ng’ombe 294 kutaifishwa. Hiyo siyo halali kwa kuwa ukisha muadhibu si vema kutaifishiwa ng’ombe.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri naomba kuwe na mpango mkakati wa kuwasaidia wafugaji na kuwatembelea kwenye maeneo yao na kuwasikiliza.

Mheshimiwa Spika, Kuhusu Kero ya Usafirishaji wa Mifugo kwa Kutumia Malori. Kuna utozaji wa ushuru wa SUMATRA na TANROADS. Tunaomba ifuatilie kujua uhalali huo.

Mheshimiwa Spika, Ushindani Usio Sawa Hususan Bidhaa Mpya ya UHT. Sasa hivi ni viwanda vinne tu ndivyo vinazalisha maziwa kwa kutumia product ya ndani. Viwanda hivi vinanunua maziwa kwa wafugaji wetu na kutengeneza UHF. Cha kusikitisha hivi viwanda vinne vinavyonunua maziwa kwa wafugaji wa ndani hawakupewa punguzo la kodi. Ila Azam anayesindika maziwa ya unga kutoka nje ya nchi na kutengeneza UHT amepewa punguzo la kodi kwa asilimia 87.5

Mheshimiwa Spika, natoa ushauri kwa kuweza kulinda watu wetu wawekezaji wanaonunua maziwa kwa wafugaji kupewa punguzo.

Mheshimiwa Spika, Kuhusu Uvuvi. Mheshimiwa Waziri nachangia kuhusu maziwa madogo, kati na mabwawa. Ninatambua lengo la kuimarisha usimamizi, uendelezaji, uhifadhi na matumizi endelevu ya rasilimali za uvuvi na utunzaji wa mazingira.

1. Unyanyasaji, kwa wavuvi, wachuuzi na watumiaji wengine wa samaki.

2. Kufunga maziwa kwa muda wa miezi sita wakati huo mvuvi amelipa leseni ya mwaka moja.

3. Kufunga maziwa kunasababisha wachuuzi wanaotegemea mboga kukosa huduma hiyo kwa miezi sita.

4. Hawa wote kushindwa kujikimu kwa maisha yao kwa kuwa hawana pato lingine ni kuwatia umaskini.

Mheshimiwa Spika, nashauri maeneo yote ya mazalio ya samaki yasivuliwe kwa muda wote na mwaka mzima ili wavuvi nao wavue kwa muda wote kwa kuwa hiyo ndiyo sehemu ya kipato.