Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia hoja iliyo mezani ambayo tukiamua kama nchi kuwekeza kwenye sekta ya kilimo na uvuvi tutapata faida kubwa kwa kukuza uchumi wa wananchi wetu na pia Pato la Taifa.

Mheshimiwa Spika, ni dhahiri kuwa bajeti zinazotengwa kwenye Wizara hii ni ndogo sana na haziendi zote na kwa wakati. Leo tunaona idadi ya kupeleka nyama nje ya nchi ni sawa na kiwango ambacho tunaingiza nyama kutoka nje.

Mheshimiwa Spika, hapa ni kwamba sisi tunapoteza maana tuna mifugo mingi; hivyo ili tukawe mosi tuanzishe viwanda vingi vya kusindika nyama na kuchakata byproducts nyingine kama vile ngozi, kwato, pembe etc. Ili sasa tuweze kumudu kuhudumia soko la ndani na kuondoa uingizwaji wa nyama kutoka nje ya nchi. Pia tunaongeza idadi ya kupeleka nyama na mazao (By-products) nyingine za mifugo nje ya nchi. Hii itakuza sana uchumi wa nchi maana tunakuwa na foreign currencies nyingi kuliko ilivyo sasa.

Mheshimiwa Spika, ni wajibu wa Serikali kuhakikisha kwamba kunakuwa na mazingira mazuri kwa wawekezaji kwenye sekta ya mifugo na uvuvi. Kwa mfano kwa kutafuta masoko, kuondoa tozo, ushuru kwenye bidhaa hizi hasa zile ambazo hazitoshi na nchi wananchama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, kwa mfano export levy kwenye ngozi.

Mheshimiwa Spika, hii inachangia sana kuua soko la ngozi na Watanazania wengi wameathirika na hapa Tanzania hamna viwanva vya kutosha ku- absorb ngozi zote. Tozo hii iwe discouraged kabisa kwenye uwekezaji kwenye ngozi; na sasa ngozi nyingi zinaharibika kwenye maghala. Ngozi mwaka 2015 ilikuwa imeanza shilingi 20,000 lakini sasa ni shilingi 1,000, tena wanakubembeleza ununue.

Mheshimiwa Spika, wakati awali ilikuwa unaweka booking na payment in advance, hii ni mbaya sana, inabidi Serikali ijue kuwa siku hizi kuna teknolojia ambayo mataifa kama China wana uwezo wa kutengeneza products equivalent na ngozi bila kutumia ngozi za wanyama (Artificial leather). Sasa with artificial leather na bado kuna hizo tozo za export levy ni dhahiri hizo ngozi zetu zitaendelea kuoza kwenye maghala. Hivyo naishauri Serikali waone umuhimu wa kuondoa hii tozo ya kusafisha.

Mheshimiwa Spika, kwenye upande wa uvuvi pia mazao yetu kama samaki na dagaa pamoja byproducts za daa (vyakula vya kuku) haviuziki kwenye masoko ya nchi jirani kama vile Kenya, Uganda, Congo n. k. Kuna export levy ya 80.16 kwa kila kilo moja ya dagaa, hii inasababisha bidhaa za dagaa zinazotoka Tanzania kuwa ghali sana na hivyo kusababisha bidhaa zetu kutouzika kabisa. kwa mfano mfanyabiashara wa Tanzania tozo na ushuru mbalimbali kwa tani 10 inagharimu takribani shilingi 4,800,000 lakini yule wa Uganda anagharimu shilingi 800,000. Sasa hapa utaona ni jinsi gani bidhaa zetu hazina thamani hata soko nyuma. Maana ni ghali sana hivyo hujikuta hawauzi bidhaa/dagaa zao.

Mheshimiwa Spika, mbaya zaidi Serikali inatoza hii tozo hata kwenye dagaa/chakula cha kuku kwenda miji ya pembezoni; mfano Mbeya, Tunduru, Sirari, Ruvuma etc; nao wanalipa nao export levy. Hii si sawa maana hawa ni Watanzania na hili linasababisha dagaa kuuzwa kwa bei kubwa sana. Nashauri Serikali kuondoa hii tozo ili bidhaa zetu ziwe sindanishi. Hii ni muhimu sana katika kukuza sekta ya uchumi na kuwapa unafuu wafanyabishara wa dagaa.

Mheshimiwa Spika, mwisho ni kuhusu kufunguliwa kwa Mnada wa Magena ambao umekuwa ukiuliza maswali hapa na kueleza umuhimu wa mnada ule ambao ungetoa fursa kwa wananchi wa Tarime na kukuza uchumi wa nchi yetu na ule Tarime.

Mheshimiwa Spika, upande wa pili, Kenya, wana Mnada wa Maabera ambao ambao upo mpakanikabisa, chini ya kilometa tatu. Hawa wanapata faida na tunakuza uchumi wao. Mheshimiwa Mwigulu alipokuwa Waziri mwaka 2016 yeye na watendaji walifika na kutembelea Mnada wa Kirumi na ule wa Magena ambao miundombinu ipo. Huu mnada tulikubaliana ufunguliwe siku moja baada ya ule wa Kirumi ili tuweze pata faida.

Pili, ilivyo sasa mifugo ya Rorya, Serengeti na Tarime inaenda maabera Kenya moja kwa moja; na ilivyo sasa kuna mianya mingi ya rushwa na upotevu wa mapato.

Mheshimiwa Spika, mnada ule ulifungwa kwa sababu ya wizi mwaka 1997. Hata hivyo wote ni mashahili, hali Tarime sasa ni shwari, mifugo inapita kutoka mikoa mingine kwenda Kenya badala ya kuuziwa pale Magena. Hii ni fursa tunayoichezea Watanzania. Ijulikane tu kuwa Kenya wanategemea ng’ombe kutoka Tanzania; inashangaza tunapoteza fursa kwa mambo ya kisiasa na si. Kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, pia alikuja Mheshimiwa Waziri Tizeba na watendaji wakaahidi kuufungua lakini nashangaa kuna nini nyuma ya pazia.

Mheshimiwa Spika, hata alivyokuja Mheshimiwa Rais Julai 2018 alielekezwa mnada wa Magena aufunguliwe. Nashangaa hata amri ya Mheshimiwa Rais inapuuzwa! Wananchi wa Tarime tungependa kujua kwa nini miradi hii inapotezewa? Hata jengo la mazao ya kimataifa la Remegwe limetelekezwa. Naomba tujulishwe hatua ya mnada wa Magena maana muhtasari upo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.