Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Spika, nianze kwa kuchangia upande wa uvuvi. Wavuvi wa Mkoa wa Tanga wana malalamiko makubwa sana juu ya nyavu zao ambazo tamko lililotoka warudishiwe lakini mpaka leo hawajarudishiwa ukizingatia wanategemea shughuli za uvuvi kusomesha watoto na kuendesha shughuli zao za familia kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, tozo na faini zimekuwa nyingi, lakini kwa nini Serikali isijikite kutoa zaidi elimu kwa watu hawa ili kupunguza matatizo yanayosababisha tozo hizo?

Mheshimiwa Spika, tunaomba tupatiwe kiwanda cha kusindika samaki, Tanga samaki ni wengi ila masoko na sehemu ya kutunzia ni tatizo. Hivyo, tusaidiwe kiwanda Mkoa wa Tanga kitakachosaidia hata kwa upande wa ajira. Pia mitaji hasa kwa vijana ambao wanajua uvuvi lakini wanazagaa tu kwa kukosa vitendeakazi. Vile vile iwasaidie hata kuboresha mazingira yao ya kuvulia, ikibidi hata wakopeshwe.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa mifugo tuna migogoro mingi sana kati ya wafugaji na wakulima, hasa Wilaya ya Handeni Kata za Misima, Sindeni, Kwamatuku, Mkata na Ndolwa. Tatizo la ni malisho ya mifugo, kesi ni nyingi sana.

Mheshimiwa Spika, pamoja na yote niiombe Wizara ione umuhimu wa kutoa zaidi elimu kwa wafugaji na hata wavuvi ili kuboresha shughuli zao. Mfano mdogo ni Tanzania kuwa termed chini ya kiwango cha kutumia maziwa kilichowekwa na FAO huku tukiwa na mifugo ya kutosha. Hapa tatizo ni elimu, wapewe elimu na mazingira bora ili wapate matokeo yaliyo bora zaidi. Pia wahamasishwe kujiunga katika vikundi ambavyo vitawasaidia sana katika kupata matokeo yaliyo bora na kulinda pamoja na kutunza mazingira ya kazi zao wakati huohuo kufuata sheria na taratibu za nchi.

Mheshimiwa Spika, ahsante na naomba kuwasilisha.