Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza Waziri na Naibu Waziri, pamoja na Wataalam kwa hotuba na pia kwa kazi nzuri ya kusimamia Wizara hii muhimu. Pamoja na mikakati mizuri ya Wizara iliyoonyeshwa kwenye bajeti hii, kuna changamoto nyingi ambazo nashauri Wizara ichukue hatua za kutatua. Napendekeza, Wizara kujenga mabwawa ya maji kwa wafugaji wa Kata ya Mjelena Mshewe, katika Wilaya ya Mbeya ili kukabiliana na ukame.

Mheshimiwa Spika, napendekeza hatua zichukuliwe za kulinda hali ya mazingira ya Ziwa Rukwa ambalo kwa kiasi kikubwa linazidiwa na mchanga unaotokana na mmomomyoko wa mito inayoingiza maji katika Ziwa Rukwa. Pia hatua za makusudi zichukuliwe za kuhamasisha vijana kuanzisha miradi ya ufugaji samaki katika Ziwa Rukwa.

Mheshimiwa Spika, napendekeza Wizara iangalie uwezekano wa kuanzisha shamba ka kisasa la mifugo ya ng’ombe wa nyama na pia ujenzi wa kiwanda cha nyama katika eneo jipya lililotengwa na halmashauri kwa kunenepesha mifugo na kiwanda cha nyama. Halmashauri imetenga zaidi ya eka 6,000 katika Kata ya Mjeta ili kubadilishana na eneo la iliyokuwa Tanganyika Packers ambayo kwa sasa limezungukwa na Mji Mdogo wa Mbalizi. Eneo hili jipya litawezesha Wilaya ya Mbeya kuzalisha ng’ombe wa kiwango kizuri sana na kuweza kukidhi ushindani wa soko la Kimataifa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.