Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote naunga mkono hoja. Pili, nampongeza Waziri, Naibu Waziri, Makatibu Wakuu na watendaji wote wa Wizara kwa kazi kubwa wanayofanya ya kuleta mapinduzi ya kiuchumi katika Sekta ya Mifugo. Sekta hii ya Mifugo ilikuwa imedorora kwa miaka mingi pamoja na kuwa ni sekta muhimu kwa uchumi wa Taifa letu. Sera ya Mifugo ya mwaka 2006 na Sheria ya Nyanda za Malisho ya Mwaka 2010 zinasisitiza kwamba uchumi wa mifugo una nafasi muhimu na ya kipekee katika kujenga uchumi imara wa Taifa letu. Ili mifugo iwanufaishe wafugaji na kuliletea mapato makubwa Taifa ni lazima mifugo ipate maeneo ya malisho, maji, tiba na masoko sambamba na miundombinu ya barabara, viwanda vya nyama na mazao ya mifugo.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa hotuba ya Waziri imeagiza haya yote naomba atekeleze aliyoyasema kwa kuhakikisha kuwa wafugaji hasa wa asili wanapimiwa na kutengewa maeneo yao mahsusi ya kufugia. Kwa mfano, katika Jimbo langu la Longido, sisi tuna nyanda za malisho zaidi ya 20 ambazo zikiendelezwa kwa kuchimba mabwawa na visima virefu vitawezesha ufugaji wenye tija ili viwanda vya nyama vinavyoendelea kujengwa nchini ipite rasilimali ya kutosha na yenye ubora unaohitajika. Baadhi ya maeneo yetu ya malisho yanayohitaji kuendelezwa ni pamoja na Loorboro, Oldenja na Engasurai.

Mheshimiwa Spika, tiba, chanjo na uogeshaji izingatiwe. Tatu, masoko mpaka masoko ya ndani ya uhakika yapatikane, masharti na tozo za kuuza mifugo na bidhaa zake nje zilegezwe ili wafugaji wasiendelee kuumia. Mwisho naomba Wizara izingatie na kuongeza suala la jinsi ya kukab iliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na kwenye suala zima la uendelezaji wa Sekta ya Mifugo hususan nyanda za malisho na vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi ya kuchangia na naunga mkono hoja.