Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, pamoja na Wizara hii kusheheni mipango bado tuna changamoto za kibajeti kuminywa na huku wafugaji wakiendelea kuteseka na kero za majosho, ukosefu wa viwanda vya kuchakata bidhaa za ngozi, changamoto za malisho, upungufu wa watumishi katika sekta hii, migogoro mikubwa na tozo holela kwa wafugaji.

Mheshimiwa Spika, mapendekezo; nashauri kuweka mazingira bora ya kisera na kisheria kwa Sekta Binafsi kujenga viwanda kwenye Sekta ndogo ya Ngozi na kuzalisha bidhaa za ngozi kwa wingi. Tanzania ina mifugo zaidi ya milioni 17.7 inayoweza kutoa bidhaa za ngozi isipokuwa bidhaa za ngozi zinazozalishwa ni milioni 2.6 kwa mwaka. Sehemu kubwa ya ngozi inauzwa nje bila kuchakatwa, ni 10% pekee ndiyo huchakatwa nchini. Napendekeza Serikali iweke mazingira bora ya kisera na kisheria kwa sekta binafsi kujenga viwanda vya nyama na maziwa.

Mheshimiwa Spika, Sekta ya Kilimo inachangia asilimia 29.1 ya Pato la Taifa. Endapo tutaongeza juhudi katika uzalishaji huenda Sekta ya Kilimo ndiyo ikaleta mageuzi makubwa nchini. Changamoto tuliyonayo ni kufeli kwa mipango ya Serikali yetu, kufungamanisha miradi mikubwa ya kiuchumi na Sekta ya Kilimo sambamba na mikakati ya kuongeza thamani kwenye uzalishaji wa Sekta ya Kilimo. Mwenendo wa takwimu za hifadhi ya chakula nchini tangu 2015 mpaka 2019 zinaonesha kiwango cha uzalishaji wa chakula kimeshuka kwa asilimia kubwa.

Mheshimiwa Spika, nimeangalia takwimu zilizotumiwa na Benki Kuu April 2019 – Hifadhi ya chakula imeshuka kwa 82.7 kutoka mwezi Machi, 2015 mpaka kufika 17.3 Machi, 2019. Ukiangalia takwimu hizo utaona Machi, 2015 hifadhi ya chakula ilikuwa tani 452,054.0, lakini kufika Machi 2019 hifadhi ya chakula imeshuka mpaka 78,336.0.

Mheshimiwa Spika, matumizi ya ardhi kuongeza uzalishaji. 53.3 ya ardhi yetu ni misitu na 15.4 iliyobaki ni ardhi yenye rutuba. Sehemu kubwa ya ardhi yetu hapa nchini inafaa kwa kilimo ila uzalishaji wetu umeendelea kushuka siku kwa siku. Kumekuwa hakuna utoshelevu wa kutosha wa chakula ilhali tuna ardhi yenye rutuba isipokuwa tu na maarifa duni ya kuongeza kiwango cha uzalishaji.

Mheshimiwa Spika, endapo tungekuwa na utoshelevu wa kutosha wa chakula basi hata ujenzi wa reli (standard gauge) unapaswa kutumika kusafirisha chakula Afrika Mashariki (Kongo DRC, Burundi, Uganda na Rwanda).

Mheshimiwa Spika, takwimu za uagizaji chakula nje ya nchi na bei za vyakula; bei zimeshuka na kuumiza wakulima, uagizaji umeongezeka kutoka dola milioni 13.3 mwezi Machi, 2018 mpaka kufikia dola milioni 15 Machi, 2019. Katika mazao sita makuu bei zimeshuka Machi, 2018 gunia la mchele 185.735.4 na sasa 168,520.5 kwa 9.3. Maharage ilikuwa 170,140 na zaidi, sasa imefikia 165,300 na zaidi kwa 2.81. Uwele gunia kutoka 76,712.1, sasa ni 75,677.4 kwa asilimia 1.3. Gunia la viazi 69,033.8 imeshuka kwa 1.0 mpaka 68,302.9. Mtama 148,8371 mpaka sasa ni 134,724.3. Hatujafanya juhudi za kutosha kutumia sehemu ya ardhi yenye rutuba.

Mheshimiwa Spika, mapendekezo yangu; ifanyike juhudi ya kuongeza thamani ya mazao kama matunda kwa kufanya (packaging) na processing ya matunda (juice) kuweka mazingira bora ya kisheria na kisera kwa Sekta Binafsi kujenga viwanda na kuchakata korosho. Kuweka mazingira bora ya kisera na kisheria kwa Sekta Binafsi ili kujenga viwanda vya kukamua mbegu za mazao kama alizeti. Kuweka mazingira bora ya kisera na kisheria kwa Sekta Binafsi kujenga viwanda vya utengenezaji wa nguo (textile industries) pamba inayozalishwa nchini ni nyingi (20) pekee huchakatwa nchini.