Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia kwenye Wizara hii. Nitumie nafasi hii kwanza nimpongeze Waziri Mheshimiwa Mpina na Naibu wake kwa angalau kuleta awareness ya Sekta ya Mifugo na jitihada wanazofanya. Mchango wangu utakuwa ni kushauri zaidi kwenye eneo la mifugo kwa maana ya ng’ombe lakini vilevile maziwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, dhana nzima ya ufugaji ni dhana ya input na output kwa maana ya kwamba unachokiingiza ndicho unachotarajia kukipata. Kwa hiyo, ukifanya wrong investment na wrong input, utarajie matokeo dhaifu. Ili viwanda vya maziwa viweze kufanya kazi vizuri, hatua ya kwanza ni kuhakikisha kwamba malighafi ya maziwa yanapatikana kwa urahisi, at a competitive rate ili yule mzalishaji wa maziwa aweze kuyanunua na mkulima apate faida.

Mheshimiwa Spika, nitatolea mfano, mfugaji anayezalisha ng’ombe wa maziwa, ng’ombe mmoja anayetoa lita 10 anahitaji kula majani makavu yenye uzito wa kilo 19. Ng’ombe huyu ili aweze kupata ile hay, hay moja inauzwa Sh.2,500 mpaka Sh.3,000, kwa hiyo, kwa siku majani yake ni Sh.3,000; tunamzungumzia mfugaji anayefuga kwa ajili ya kuuza maziwa commercially. Anahitaji kumpa supplement kilo mbili asubuhi na akilo mbili jioni, ina maana kilo nne ya supplement. Kilo nne ya supplement kwa bei ya sasa hivi iliyopo sokoni ni kati ya Sh.470 mpaka Sh.500. Kwa hiyo, kama atampa kilo nne maana yake ni Sh.2,000. Kwa hiyo, kampa majani yenye thamani ya Sh.3,000 halafu kamlisha supplement ya Sh.2,000, gharama yake ni Sh.5,000.

Mheshimiwa Spika, mifugo yetu yote iliyopo katika nchi hii wastani wake wa uzalishaji ni lita 10 maximum, hatuna ng’ombe wanaozalisha lita 20 au lita 30, ni wachache sana na wafugaji wetu katika household wengi capacity ya ng’ombe wao wengi ni ten litres at the best. Kwa hiyo, maziwa anayauza shilingi ngapi, anayauza Sh.900 mpaka Sh.100; kwa hiyo kapata Sh.9,000 wakati yeye kagharamikia Sh.5,000 mpaka Sh.6,000; hizi ni gharama za moja kwa moja. Bado kuna gharama za madawa na maji, matokeo yake ni kwamba bei ya uzalishaji wa maziwa per litre compared na bei ya ununuzi kiwandani, wafugaji hawapati faida yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mfugaji ana-opt kufanya nini? Ana-opt kufanya uchungaji wa kawaida, hata hapa Dodoma ukipita barabarani unaona ng’ombe wa kisasa wanachungwa barabarani kwa sababu hawana uwezo wa kupata input ya kumlisha ng’ombe, kwa hiyo tunaingia kwenye tatizo la feeding. Kinachotokea kwa kuwa ng’ombe hajalishwa vizuri, hawezi kuzalisha vizuri, kwa hiyo viwanda haviwezi kupata maziwa ya kutosha.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nini ushauri wangu kwa Serikali? Ushauri wangu wa kwanza, ni lazima Wizara ya Fedha, Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Mifugo, Wizara ya Ardhi, Wizara ya TAMISEMI wakae chini pamoja kuja na master plan. Ukisoma Tanzania Livestock Master Plan iliyozinduliwa na Waziri, it is centered kwenye Wizara moja na suala la ufugaji ni crosscutting, siyo la Wizara ya Mheshimiwa Mpina peke yake. Leo tuna shamba la Serikali la kuzalisha malisho lipo Dar es Salaam, ni under capacity, haliwezi kuzalisha chakula cha mwaka mzima. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimeona hapa Mheshimiwa Waziri amesema anafanya uhilimishaji wa ng’ombe wa kienyeji milioni tatu kupata mitamba milioni moja. Ni hivi, ukimchukua ng’ombe wa kienyeji Mheshimiwa Mpina anafahamu Tarime ya kule kwetu Tabora na Shinyanga, ukampandisha dume wa Fraiesian atapatikana F1, F1 huyu capacity yake ya uzalishaji wa maziwa is maximum of three and four litres. Ukimpelekea mfugaji akamfanye zero grazing is an economical, haiwezekani, hawezi kumzalisha na kupata mazao. Ili aweze kupata ng’ombe wa kumpatia maziwa mazuri anayetokana na ng’ombe wa kienyeji ni third generation, apatikane F1, F2, F3 ndiyo huyu F3 atafika at least 10 litres kwa sababu genetically ni 25, 50 and 75 yaani generation ya tatu ndiyo tutapata. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu ambao nataka niishauri Serikali, hawawezi kufanya mass insemination nchi nzima, lazima tufanye clustering ni wapi tunazalisha ng’ombe wa maziwa, wapi tunazalisha ng’ombe wa nyama, huu ni ushauri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili kwenye maziwa, leo kiwanda cha maziwa kinahitaji kuzalisha maziwa na wao Wizarani wanajua, walikuja watu wa Tanga Fresh kwenye Kamati ya Bajeti eti waliomba kibali na mimi niwapongeze Wizara ya Mifugo waligoma, wanaomba kibali wa-import maziwa raw kutoka Rwanda.

Sasa what is the success story ya Rwanda? Success story ya Rwanda ilikuwa ni moja, kila kaya ilipewa programu ya ng’ombe mmoja wa maziwa lakini kwenye vijiji zikaanzishwa collection center kwamba wafugaji wote wanaleta maziwa yao kwenye center moja, pale kwenye center, kiwanda kinakuja kuyachukua yale maziwa. Sasa hivi wafugaji wetu wapo scattered, hawezi kusafirisha maziwa yake kuyaleta kwenye center au kumfikishia mtu wa kiwandani kwa sababu gharama ni kubwa na kwa hali hii hatuwezi ku-break through. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu, Asas yupo nyanda za juu, it’s better kukaa chini na Wizara ya Fedha kuangalia incentive za kikodi na kumtengenezea clustering centers kwenye Mikoa ya Mbeya na Iringa, yeye ajenge cooling centers ambazo wafugaji watapeleka maziwa yao pale, yeye ataenda kuyachukulia pale ili gharama zake za uzalishaji ziwe ndogo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ambalo nataka niongelee, nataka nimshauri Waziri, ukienda NAIC pale Arusha wana ngo’mbe anaitwa Friesian, wana ng’ombe labda anaitwa Borani, wana ng’ombe anaitwa Ayrshire. Kwenye breeding ya ng’ombe wa nyama the best breed ni aina mbili; ni Borani na Sahiwal, lakini kwa insemination hatuwezi kubadilisha ng’ombe wetu wa Kisukuma na Kigogo na Kimasai.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu; Serikali ianzishe programu, mnunue madume ya Borani; wakati wa Mwalimu Nyerere kulikuwa kuna holding grounds zilikuwa zinatumika kwa ajili ya breeding; kwa hiyo yale madume ya Borani mnayapeleka Nzega, halmashauri inakabidhiwa, katika kila kijiji kunakuwa na centers au kata halafu mnaenda kuhasi madume ya kienyeji, mnaanzisha programu ya kupandisha ng’ombe wa Borani kwenye ng’ombe wa kienyeji, tutabadilisha breed namna hii.

Mheshimiwa Spika, lakini ziki-run parallel ng’ombe wa kienyeji na Borani ambao wanauzwa milioni moja na nusu, milioni mbili, wafugaji hawawezi ku-afford. Ili anunue dume mmoja wa Borani inabidi auze ng’ombe zaidi ya sita wa kienyeji, he cannot afford kwa sababu ana ng’ombe wake kumi anaona anaingia umaskini. Kwa hiyo mimi nashauri Serikali tafakarini…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante, malizia.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, namalizia la mwisho, dakika moja tu nakuomba.

Mheshimiwa Spika, ngozi; rudisheni utaratibu wa zamani, zamani kulikuwa kuna kitu kinaitwa Tanzania Hides and Skin, ngozi zinauzwa kwenye mnada kwenye machinjio. Bila kufanya namna hiyo mazao ya ngozi hamuwezi kuya- control. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru, naunga mkono hoja. (Makofi)