Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa niwe mchangiaji wa kwanza siku ya leo kwenye bajeti hii iliyoko mezani, Bajeti ya Sekta ya Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Spika, sekta ya mifugo na uvuvi, kwangu ni sekta ambayo imenilea, imenikuza na imenisomesha. Kwa hiyo, nitachangia kwa passion sana kwa sababu, sekta hii ni sehemu ya maisha yangu.

Mheshimiwa Spika, Sekta ya Mifugo na Uvuvi inaajiri takribani asilimia 50 ya watanzania, lakini inachangia asilimia 6.9 ya pato la TTaifa, kuliko hata Sekta ya Madini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kwa masikitiko makubwa, sekta hii imepuuzwa na Serikali ya Awamu ya Tano. Kama Serikali itaamua kuwekeza kwenye sekta ya mifugo, uvuvi pamoja na kilimo, tutakwenda kwenye uchumi wa kati, kwa sababu sekta hizi ni inclusive, ni jumuifu na zinamgusa kila mtanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninachoshangaa ni kwamba, Serikali imeshindwa kuipa sekta hii kipaumbele, imeenda kuwekeza kwenye maeneo ambayo hayana impacts kwa wananchi wengi, na nitakwenda kuthibitisha hili baadaye. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Tano imerudisha sekta ya mifugo na uvuvi miaka mitano, sita nyuma, wanasema, historia nishahidi mzuri sana, na leo nitakwenda kutumia hisitoria ku-substantiate mchango wangu. Hapa nina hotuba za bajeti tatu, nina hotuba ya bajeti ya mwaka 2013/2014 ya Serikali ya Awamu ya Nne, nina hotuba ya mifugo na uvuvi ya mwaka 2018/2019 na nina hotuba ya bajeti pendekezwa ya mwaka huu.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia kwa mfano tu vitu vichache, kwa mfano maduhuli ambayo yalipangwa kukusanywa kwenye bajeti ya mwaka 2018/2019 na Wizara hii ya bilioni 18.5 yalikusanywa mwaka 2014 na Serikali ya Awamu ya Nne, halafu tunasema tunatekeleza, hivi tunatekeleza kitu gani! Mauzo ya mazao ya uvuvi mwaka 2014 yalikuwa dola za kimarekani milioni 832 lakini mwaka 2017 yameshuka mpaka dola za kimarekani milioni 182. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuko serious kweli? Tunataka kuwekeza kwenye mifugo? kwenye uvuvi! Naomba niende kwenye bajeti ya miaka hii mitatu muone tofauti kubwa na muone jinsi gani tumerudi nyuma kwenye sekta hii ya mifugo na uvuvi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka 2013/2014 bajeti yote iliyopitishwa na hili Bunge lako ilikuwa bilioni 54.5, mwaka 2018/ 2019 bajeti yote ilikuwa bilioni 35.3, yaani miaka mitano baadaye, bajeti ya sekta ya mifugo na uvuvi, inapungzwa kwa bilioni 19.2, sawa asilimia 35, ndiyo bajeti ya maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka 2013/2014, ilikuwa bilioni 13.8, mwaka 2018/2019, ilikuwa bilioni nukta tano, yaani Serikali kwa miaka mitano, imepunguza bajeti ya wafugaji na wavuvi kwa shilingi bilioni 8.4. Mwaka 2013 bajeti ya maendeleo ilitekelezwa kwa asilimia 40, mwaka 2018/2019 ilitekelezwa kwa asilimia 43. Yaani within six years, implementation ya bajeti ya maendeleo ni asilimia tatu, kwa sekta muhimu kama hii ya uvuvi na mifugo! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, halafu tuje hapa tuwasifie, tusifie nini? This is not a praise and worship team, hili ni Bunge, tunatakiwa kuisimamia na kuiwajibisha Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, njoo kwenye bajeti pendekezwa, mwaka 2019/2020, bajeti hii iliyoko mezani, bajeti yote ni shilingi billioni 64.9, baada ya miaka sita Serikali inaongeza only 10 billion, kwenye sekta ambayo inaajiri zaidi ya asilimia 50 ya watanzania, lakini kwenye bajeti ya maendeleo ni shilingi bilioni 13.8, wakati mwaka 2013/2014, bajeti ya maendeleo ilikuwa bilioni 14. Yaani ongezeko la milioni 200 kwa miaka sita, are we real serious, kweli tunataka kutoka hapa tulipo, sijui tunakwama wapi!

Mheshimiwa Spika, naomba niende kwenye sekta ndogo ya maziwa, mwaka 2013/2014, uzalishaji wa maziwa ulikuwa lita bilioni 1.92, mwaka 2018/2019 ulikuwa bilioni 2.4, ongezeko la asilimia 20 ndani ya miaka mitano kwa maana ya aslimia nne kila mwaka, hakuna efficiency, tukubali tu, hakuna efficiency. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, twende kwenye usindikaji sasa, mwaka 2013, viwanda vyetu vilikuwa na uwezo wa kusindika lita 135,000 kwa siku, mwaka 2018/2019, viwanda vyetu vina uwezo wa kusindika lita za maziwa 154,000 kwa siku, yaani ongezeko la lita 19,000 kila mwaka, halafu tunasema Serikali ya wanyonge, wanyonge gani tunaowazungumzia? Wakati huo viwanda vilikuwa 67, sasa hivi tuna viwanda 91, hapa hatuzungumzii wingi wa viwanda, tunaongelea uwezo wa uzalishaji wa viwanda vyetu, operating capacity, viwanda vya maziwa vina operate kwa asilimia mbili. 98% ya viwanda vyetu vya maziwa vina operate under capacity, hakuna efficiency kwenye viwanda vyetu. Kwa hiyo, siyo hoja kwa na viwanda vingi, hoja ni uwezo wa uzalishaji wa viwanda vyetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunaweza tukawa na viwanda vichache, lakini tukaweza kuzalisha zaidi na uzalishaji ukawa na tija. Kwa maana hiyo, asilimia 98 ya mazao ya wafugaji wa nchi hii, hayana soko, na hii imepelekea wafugaji wa nchi hii wameendelea kuwa maskini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niende kwenye suala la sekta ndogo ya nyama, na hapa ningependa nimnukuu Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Mpina, “Tanzania inaagiza tani 2000 za nyama kila mwaka na wakati huo huo inauza nje tani 2000 za nyama” utaona kuwa kiasi cha nyama tunachouza nje kwa bei rahisi kabisa ndicho kiasi hichohicho tunachoagiza kutoka nje kwa bei ya juu. Natamani kuona wawekezaji wengi wakiwekeza katika sekta hii, kwa sababu fursa zilizopo ni kubwa. Mheshimiwa Waziri, hapa issue siyo kuwekeza kwenye viwanda, viwanda tayari tunavyo, issue ni kuhakikisha viwanda vinakuwa na tija, vinakuwa na efficiency na vonaweza ku-operate at full capacity.

Mheshimiwa Spika, na ningependa, with due respect my brother, wakati unakuja kuhitimisha hoja yako, utuambie, ni kwa nini viwanda vyetu vimeendelea ku-operate under capacity, vyote vya nyama na maziwa! Pia, ni kwa nini kama nchi tumeendelea kuagiza mazao ya mifugo, uvuvi kutoka nje, wakati tuna viwanda katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, tuna viwanda 25 vinavyoweza kusindika maziwa katika nchi yetu na uwezo wake kama vingekuwa vinafanya kazi, kwa uwezo halisi kwa maana ya full operating capacity, vingekuwa na uwezo wa kuzalisha lita tani 626,000 za nyama, lakini sasa hivi zinazalisha tani 81,220 za nyama. Kwa hiyo, vinazalisha chini ya uwezo wake kwa asilimia 87.3. sasa halafu tunaongelea kuongeza viwanda, we don’t need quantity, we need quality. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna…

SPIKA: Ahsante sana ni kengele ya pili.

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. (Makofi)