Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa muda huu niweze kuchangia hotuba hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wawili wamezungumza kwa makini kabisa na leo niliseme ili Mheshimiwa Waziri aweze kulifahamu. Tukiondoa mrabaha wa 0.4 hivi leo, kesho tu asubuhi kuna meli zaidi ya 50 zinataka kuja kuchukua leseni ndani ya Tanzania. Tukiweza kuondoa mrabaha huu ambao ndiyo kikwazo katika uvuvi wa nchi yetu, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri aweze kuondoa mrabaha huu ili wavuvi na wawekezaji waweze kuja ndani kuvua katika Bahari Kuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiweza kuondoa mrabaha huu na siwezi kufahamu tatizo ni nini linalomkwamisha Mheshimiwa Waziri, kuondoa mrabaha huu ambao ni usumbufu mkubwa. Huu mrabaha naamini hata Mheshimiwa Waziri akija anaweza akaja na majibu mazuri kuhusu kuondoa huu mrabaha ambao ni kero kubwa katika kuwekeza katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu bila ya uvuvi hatuwezi kusogea mbele, tukiwekeza kwenye uvuvi tunaweza tukapata mafanikio makubwa kuliko ambayo anayakusudia. Nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, nilizungumza nyuma ununuzi wa meli kubwa za uvuvi umeshindikana hapa haupo kabisa, mimi mwenyewe nashangaa. Sasa leo wawekezaji wanataka kuja, anawawekea kodi kubwa ambayo itawasumbua hawawezi kuvua katika bahari kuu. Sasa hawa samaki nia yake Mheshimiwa Waziri kuwafanya nini kwa sababu samaki huwa anatembea, samaki siyo mawe, akiwazuia yeye hapa basi huko wenzake wanawavua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, naamini akija hapa, anaweza kuondoa kwa mara moja huu mrabaha ili wawekezaji wetu waweze kuja kuvua ndani ya bahari yetu hii. Tuna shida ya wawekezaji, wawekezaji wapo, tunawazuia kwa vijisheria vidogo vidogo; hili suala Mheshimiwa Waziri siyo kweli na naamini anaweza akafanya hii kazi kwa mara moja ili hizi meli ziweze kufanya kazi. Tunasubiri tuwekeze meli zetu, meli hazipo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, ukiangalia hii kodi hata na sisi upande wa Zanzibar tunafaidika asilimia kubwa tunategemea katika bajeti yetu ya Serikali, sasa leo akisema hizi fedha haziendi, leseni hakuna, sasa kule Zanzibar Mheshimiwa Waziri tufanye nini na sisi katika mategemeo yetu hili suala la uvuvi pia tunategemea kwa sababu Kisiwa cha Zanzibar kimezungukwa na habari kila mahali sasa maendeleo yetu yote yanategemea uvuvi wa bahari kuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo akiendelea kuzuia uvuvi huu, hatutafika mahali pazuri. Nimwombe sana Mheshimiwa Waziri akija kesho kutoa majibu, jibu la msamaha wa huu mrabaha, basi namwomba sana aweze kuondoa na siyo kwa muda, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Saada kazungumza aondoe kwa muda; huu unatakiwa kuondolewa kabisa, usiwepo tena. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. (Makofi)