Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi kupata fursa hii kuchangia hoja ya Wizara hii ya Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nilitaka niunge pale ambapo mchngiaji amemaliza. Tanzania takribani tumekosa kwa wastani, tungeweza kupata, kwa mwaka huu, zaidi ya meli 54 ambazo zingeweza kutuingizia si chini ya bilioni zaidi ya 20 mpaka 30 za pesa ambazo zingeweza kuingia kwa tozo ile ya 0.4. Kwa kweli lazima tuseme ukweli kile ni kikwazo na hakuna mtu ambaye atakaekuja kwa ile 0.4.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili wenzetu Comoro tu hapo safari hii wamesajili meli 31 kwa kutumia gape hilihili, kwamba sisi tumeshindwa kuweza kutoa hiyo fursa ya kuondoa hiyo tozo, imetu-cost. Wao wanasema hawajawahi kupata mapato mengi yatokanayo na uvuvi kama mwaka huu kwa vile sisi tumeshindwa kutoa hiyo tozo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ndani ya maeneo yetu ya bahari tuna zaidi ya maili 360 zinavua katika ukanda wa Tanzania katika meli za mraba zile zaidi ya mia mbili na ishirini na tatu elfu zinavuliwa, watu wanavua; na hayo ni mataifa ya nje; na ndiyo maana ikapatikana ile takwimu ya asilimia 67 ya mapato wanayochukua nje yanatokana katika ukanda wetu wa uvuvi wa bahari kuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli, tunapoteza kiasi kikubwa na hii sekta tuseme ukweli bado haijafanya vizuri. Mimi nakataa kuniambia takwimu ya kwamba, samaki walioko katika Ziwa Victoria ni wengi zaidi kuliko walioko katika ukanda wa bahari, hiyo data mimi siikubali. Naomba tupate reference iliyo ya uhakika zaidi; kwa sababu meli za mraba zaidi ya 1,400 ukaseme kwamba eneo la Ziwa Viktoria ndio samaki wengi? Si kweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, stock fishing imefanyika juzi baada ya miaka zaidi ya 20 na meli ile ya ki-Norway, taarifa rasmi hazijaja. Kwa hiyo Waziri utupe taarifa zilizokuwa sahihi zaidi kuhusiana na eneo hili. Bahari yetu bado ni potential, ina samaki wakutosha, lakini bado hatujafanya uwekezaji ulio sahihi tukaweza kuvuna samaki ambao wako katika maeneo yetu matokeo yake tunawafaidisha watu wengine ambao hawako Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jingine nililotaka kulizungumza ni kwenye sekta ya mifugo. Sekta ya mifugo pamoja na maelezo mengi na mazuri ambayo umeyatoa ya kukusanya maduhuli, lakini bado sekta ya mifugo inakabiliwa na changamoto nyingi; kwanza kwenye ngozi yenyewe. Kitendo kile cha kupiga chapa kimesababisha ngozi yetu ikose thamani na imejazana kwenye magodauni, hainunuliki popote sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ng’ombe wengi wamepigwa chapa, uchinjaji uliofanyika holela, hakuna viwanda vya kuchakata samaki matokeo yake ng’ombe wetu wanakosa thamani ya ubora katika viwanda mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kubwa zaidi sasahivi umejitokeza mtindo kwamba wenzetu wa Nigeria wanakuja kuchukua zile ngozi kwa ajili ya chakula na si kutumia kwa ajili ya kuchakata kwenye viwanda mbalimbali. Kwa hiyo nafikiri tunahitaji tujitathmini na sheria zetu na kanuni zetu ili kuona kwamba suala hili ili liweze kuboresha mazingira tuliyonayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilikuwa na watu wale wa kiwanda kile cha Magereza cha Luanda, bado wanasema ngozi zetu haziendani na thamani ya viatu ambavyo wanavitengeneza. Wakati mwingine wanalazimika kuchukua ngozi nje ya Tanzania kwa ajili ya uendeshaji wa viwanda vyetu. Tunahitaji tuone tunafaidika na rasilimali tulizonazo ndani ya nchi na si vinginevyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukija kwenye suala zima la maziwa na hasa ufugaji wa ng’ombe wa maziwa. Bado Serikali au sekta hii ya mifugo haijawekeza kwenye dairy farm. Tunahitaji kuwa na ng’ombe wa maziwa na si kuchunga ng’ombe. Watanzania wanachunga ng’ombe sana, lakini hawafugi ng’ombe inavyotakiwa, matokeo yake sasa tunashindwa kuweza kuingia katika soko la maziwa na sisi kuwa ni dampo la kuletewa maziwa kutoka nchi za nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Zimbabwe imekuwa Tanzania ndio soko lake kubwa, Malawi sasahivi ndio soko lake vilevile, Uganda wanatuletea, Kenya wanatuletea, lakini sisi tunajisifu kwamba ni wa pili sijui wa tatu kwa kuwa na ng’ombe wengi hapa Tanzania, haileti maana kwa kweli. Tunataka tuone restructuring ya maana katika sekta ya mifugo na si hivi tunavyokuwa tunaelezwa kila siku, hatujafanya vizuri katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine tunalolisema ni kwamba tunahitaji kuona kwamba viwanda vile vya maziwa vya hapa vinatengeneza bidhaa ambazo zinakubalika katika masoko. Tatizo letu bidhaa za viwanda vyetu haziingii kwenye soko la utalii. Sisi kule Zanzibar wale wanaoleta maziwa zaidi ya tani 40 kila mwezi zinashushwa pale na zinasambazwa katika ukanda wa hoteli za kitalii. Maziwa yale yangekuwa ya Watanzania pato lile lingerudi likaingia Tanzania, lakini maziwa yale unayaona ni ya Wakenya, Waganda, Wazimbabwe na Afrika Kusini, this is not fair. Tunataka tuone mabadiliko chanya sasa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Rehani, muda umeisha.

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.