Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia fursa ya kuchangia Wizara hii muhimu. Nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mpina na Mheshimiwa Naibu Waziri mjomba Kerebe wanamsubiri, apitie kwenye diary yake kabla hajaenda Kerebe. Jambo la kwanza niwaeleze asilimia 70 ya Halmashauri yangu ni maji, Ziwa Victoria asilimia 70 ya Wilaya yangu ya Muleba ni maji, kwa hiyo mimi ni mvuvi. Sehemu kubwa ya eneo ambalo Wizara hii inajinasibu nalo katika ufugaji wa ng’ombe (NARCO) ni Jimbo langu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia bajeti hii nataka kuzungumzia mafanikio ya kampeni ya uvuvi haramu, ni pale tulipofanikiwa kuweza kupata samaki wale wanaokidhi hata kwenda kwenye ule utamu wa samaki mwenyewe hayo ndio mafanikio. Hakuna aliyejua njia hiyo ndio maana njia zilizotumika mimi siwezi kuziunga mkono, nakubaliana na Waheshimiwa Wabunge wanaosema yale makandokando yaliyofanyika yarekebishwe. Nami nampa Mheshimiwa Waziri makandokando ambayo ningeomba ayarekebishe, atoe amnesty, kuna watu walinyang’anywa injini zao, atamke kwamba wale walionyang’anywa injini zao naziachia, wale waliovunjiwa mitumbwi yao hiyo tuiache. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tena nami nina dhambi hiyo, tuliwahamasisha wana viwanda wa Tanzania wakauze nyavu, tukazuia wana viwanda wa nje, kumbe kuna wana viwanda wa Tanzania wakapeleka nyavu zisizokuwa na viwango, Mheshimiwa Waziri ashirikiane na Mheshimiwa Waziri wa Viwanda waende walete zile nyavu, wenye viwanda waliouza nyavu kanyaboya waweze kuwakamata kusudi mbele ya wananchi tuweze kuonekana ni watu wazuri kwa wananchi. Sio kwamba namchomekea mjomba aende Kerebe kwamba hatarudi, hapana, lakini hawa wavuvi wanaweza kutushangilia kwa mikono lakini moyoni wanaumia. Sasa namna ya kuweza kusawazisha mambo haya ni kukaa pamoja na wao. Mheshimiwa Waziri arudishe injini za watu mambo yaishe, twende mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la nyavu, Jimbo langu linapakana na Uganda kwa maji na linapakana na Kenya kwa maji, milimita sita linavua dagaa kwa watu wa kutoka Uganda na Kenya, wewe unaniambia mpaka nilete milimita nane. Tukae chini tusawazishe mambo haya, tunachekwa. Mganda anatoka Uganda anavua Goziba, anavua Zilagura anachukua samaki, samaki hana mpaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la leseni; sisi tunafuata sheria za Wizara ya Mifugo, hatuwezi kuruhusu mtu aharibu mazingira, tunatunza eneo letu la maji square kilomita saba, siwezi kukubaliana na Serikali kwamba mtu akakate leseni Bunda aje kuvua kwangu, hapana, aende Muleba akate leseni Muleba, ukikata leseni Bunda, kavue huko huko, kila mtu atunze mazingira yake. Hatuwezi kuhakikisha halmashauri hizi tunazinyang’anya mapato, mapato ya Wilaya yangu yanatokana na leseni, kama unaipenda Muleba nenda kwa Shilembi akukatie leseni uvue, kama hutaki nenda huko kwao ambako wanaharibu mazingira. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie cage, ufugaji wa vizimba Uganda wameanza kufuga kwa vizimba, Tanzania mnaweka masharti, haiwezekani, ndio hayo mambo Profesa Kishimba anakwambia nenda na wenzako. Hata hivyo, ni kuna watu wa Maalia, watu wa Bumbire wakati wa mvua tulikuwa tunapiga samaki kwa fimbo mkaleta over fishing kwa teknolojia ya kisasa, wale ambao wamewaondoa kwenye mavuno yao ya asilia, chonde waende wakawape pesa, hizo pesa nyingi wanazovuna warudishe kwa jamii wasaidie vijana waweze kufuga kwa vizimba. Hawezi kwenda mbele akasema amekusanya asilimia 147 hawatamwelewa, hizo kama 147 asilimia 100 wapelekee Mheshimiwa Mzee Mpango atashukuru, 47 arudishe kwa wananchi watampenda sana. Zile njia ambazo wanavuna sizo, hizo waachane nazo, akimnyang’anya nyavu haramu ampe nyavu halali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie Sekta ya Maziwa; Tanzania wanachakata maziwa lita 150,000, wengine wanasema hazifiki, Uganda wanachakata lita milioni mbili. Napenda niwashauri walielewe hili, hii ndio sekta na Mheshimiwa Waziri nazungumza ili kumsaidia, yeye ndiye ng’ombe wa maziwa wa uchumi wa nchi hii. Hizi ndizo sekta za kutupelekea uchumi wa kati ulio jumuishi, ukiwalisha wafugaji, ukawalisha wavuvi, uchumi unachangamka, uchumi jumuishi uko kwenye sekta hizi. Kwa hiyo ni suala la Serikali kupeleka pesa nyingi, watu wa Uganda wanawasaidia watu kuwatengenezea malisho, wanawapa mabirika ya kukusanyia maziwa, wanajengea viwanda. Kiwanda Uganda ni market wanatengeneza lita milioni 2,000,000 kwa siku.

Mheshimiwa Spika, samahani, Mheshimiwa Mwenyekiti, naona unaniangalia nakuchulia mambo mema. Naunga mkono hoja na nitawasilisha kwa maandishi. (Makofi)