Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi niweze kutoa mchango wangu katika bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi.
Awali ya yote namshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema, mwingi wa neema ambaye ameniwezesha kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie fursa hii kumpongeza sana Rais wetu mpendwa Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuliongoza Taifa hili.
Vilevile nampongeza Makamu wa Rais Mheshimiwa Mama Samia Suluhu, Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa, Baraza la Mawaziri kwa namna ambavyo wanajituma kuhakikisha kero za Watanzania zinapungua au zinakwisha kabisa. Ninapenda kuwatia moyo waendelee kukaza buti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie fursa hii pia kuwashukuru sana wananchi wa Mkoa wa Singida hususan wanawake na vijana kwa kuniamini na kunichagua kwa kura nyingi za ndio napenda kuwahakikishia kwa heshima hii kubwa waliyonipa sitawaungusha na wala sitaanguka katika kuwatumikia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya utangulizi huo najielekeza moja kwa moja katika kuchangia. Mwanafalsa mmoja John Dew aliwahi kusema education is not preparation for life, education is life itself, akimaanisha kuwa elimu siyo maandalizi ya maisha, elimu ni maisha yenyewe, hivyo basi, elimu ndiyo msingi mkuu katika kuyamudu maisha ya kila siku na ndiyo mkombozi wa maendeleo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania inatajwa kuwa na elimu ya kiwango cha chini ukilinganisha na nchi nyingine za Afrika Mashariki, hii ni kutokana na ukweli kwamba elimu inayotolewa haikidhi viwango vya ubora.
Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu inayotolewa katika vyuo na shule zetu za Serikali haimuandai kijana kujiamini, kuwa mbunifu, kuwa ni mwenye uwezo wa kubembua mambo, kuwa na communication skills, kuweza kujiajiri au kuajiriwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii kijana aliyemaliza elimu ya kidato cha nne kutoka nchini Kenya au Uganda akija Tanzania anapata ajira bila wasiwasi wowote, hii ni kwa sababu elimu aliyopata ni bora, inamwezesha kujiamini, inamwezesha kujielezea kwa ufasaha kwa lugha ya kiingereza ambayo hapa nchini kwetu ni lugha ya biashara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo sababu kadhaa ambazo zinachangia kushuka kwa kiwango cha elimu katika shule zetu za Serikali. Sababu hizi nitazitaja kama ifuatavyo:-
Kwanza, ni utayarishaji wa mitaala ambayo haiendani na wakati na mazingira ya sasa. Mitaala ambayo inakosa skills ambazo zingeweza kumsaidia mwanafunzi kujiamini au kujitegemea baada ya kumaliza elimu yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tafiti zimeonyesha kwamba kuna changamoto za utayarishaji na utekelezaji wa mitaala bila kufanyiwa majaribio jambo linalopelekea walimu wengi kukosa stadi za maisha, kukosa maarifa ya kufundishia. Mfano katika Taifa la Netherland mtaala wake unasisitiza kufundisha elimu ya ujasiriamali kuanzia shule za sekondari. Hivyo basi, ningeishauri Serikali kutizama upya mitaala ambayo itazingatia uchambuzi wa kina wa kumwezesha kijana kuweza kujitegemea na kujiamini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya pili inayochangia kushuka kwa kiwango cha elimu, ni uhaba wa vitendea kazi na teaching methodology ambazo kimsingi hazimjengi mwanafunzi kujitegemea au kujiamini. Shule zetu nyingi za Serikali zinafundisha kwa nadharia zaidi kuliko vitendo. Wenzetu wa dunia ya kwanza wanasema practice makes perfect. Unapomfundisha mwanafunzi kwa nadharia na vitendo unamwezesha mwanafunzi huyo kulielewa somo hilo vizuri zaidi. Hivyo kuna haja ya msingi ya kurudisha elimu ya vitendo katika shule zetu za msingi na sekondari. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano, ukimfundisha mwanafunzi mapishi ya keki kwa nadhari na baadaye ukaweza kumuonyesha namna ya keki hiyo inavyopikwa ataelewa zaidi. Kusoma kwa nadharia tu ni sawa na kuwa-feed wanafunzi kitu ambacho hawana reference nacho. Hivyo basi, ningeomba sana elimu ya vitendo ilirudishwe kama zamani ilivyokuwa ikifundishwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo linachangia elimu yetu kuendelea kuwa duni ni kukosekana kwa uwiano kati ya mwalimu na wanafunzi darasani katika shule zetu wanafunzi katika darasa moja wanaweza kufikia idadi ya wanafunzi 35 mpaka 50, idadi hii inamuwia mwalimu ugumu kuweza kufanya assessment kwa kila mwanafunzi. Matokeo yake anaangalia tatizo la mwanafunzi mmoja na kulitolea suluhu kwa wanafunzi wote darasani. Tofauti ya darasa lenye wanafunzi kumi mpaka kumi tano, ni rahisi mwalimu assessment ya kila mwanafunzi na kujua wana tatizo gani pindi atakapomaliza kufundisha na kuona namna gani ya kuwasaidia hao wanafunzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutomuandaa mwalimu vema ili afundishe kuendana na wakati wa sasa nayo ni sababu inayochangia kuporomoka kwa elimu yetu. Ajira ya ualimu imewekwa katika kundi la kitu ambacho hakina thamani. Leo hii wanaochukuliwa kujiunga na ajira hii ni wahitimu waliopata daraja la nne katika kidato cha nne.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande mwingine maslahi ya walimu ni duni. Mwalimu kwa kweli hawamjali mwalimu, mwalimu huyu hana nyumba ya kuishi, anaishi katika mazingira duni, mshahara wake ni mdogo na wala haumkidhi mahitaji yake na wakati mwingine haufiki kwa wakati. Ningeiomba Serikali yangu kuwaangalia walimu na kuangalia maslahi yao upya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, unategemea nini kwa mwalimu kama huyo na atakuwa kweli na morali ya kufundisha si ata-beep tu kutimiza wajibu wake na kuondoka zake. Ndiyo maana kiwango cha elimu kimeendelea kushuka kutoka asilimia 22.3 mwaka 1985 na kufikia asilimia 49.6 mwaka 2010.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaishauri Serikali kuja na mpango utakaowawezesha walimu kupata training za mara kwa mara na semina zinazolenga mahitaji ya sasa ili kuwawezesha kufundisha kwa ufanisi na ufasaha katika dhama hizi za sayansi na teknolojia. Lakini pia vilevile walimu watakaokuwa wamejiendeleza wapewe incentives kulingana na madaraja yao, hii itasaidia sana kupunguza madai ya uhamisho ya mara kwa mara na kuwafanya walimu watulie katika maeneo yao ya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiofichika kwamba katika shule zetu za Serikali hatuna programu za kuhamasisha watoto wapende kusoma vitabu, wanafunzi wetu hawana tabia ya kujisomea vitabu, lakini pia vitabu vyenyewe hakuna vya kutosha. Serikali ione umuhimu wa kuanzisha programu au iwena slogan maalum ambayo itawahamasisha wanafunzi wetu na katika kila mkoa uwe na e-library ambayo wanafunzi watapata ku-access vitabu mbalimbali zikiwemo story books ambazo zitaweza kuwasaidia katika ku-improve english language ambayo ni medium of instruction in secondary schools.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Singida ni miongoni mwa mikoa yenye changamoto nyingi katika sekta ya elimu. Mkoa wa Singida una jumla ya shule 542, kwa wastani kwa mwaka watoto 25,000 humaliza shule ya msingi ukilinganisha na ufaulisha watoto 13,383 kwa mkoa mzima. Ukilinganisha idadi hii ya wananfunzi waliomaliza shule za msingi hailingani kabisa na wale wanaondelea na masomo ya shule za sekondari. Zaidi ya vijana 10,000 wanakaa mitaani…