Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kuhusu Pembejeo. Kwa kuwa wakulima wamelima mazao, kwa nguvu zote na kwa ari lakini pembejeo ni gharama sana matokeo yake wananchi wanapanda mazao bila utaalam wa kutumia mbolea na dawa za wadudu, mazao yamekuwa kidogo. Niishauri Serikali kupunguza gharama ya pembejeo ili wananchi walime kitaalam na kuwa na mavuno yenye tija.

Mheshimiwa Spika, Ukosefu wa Masoko ya Mazao. Pamoja na kwamba wakulima wanajituma kuzalisha mazao hata kwa gharama kubwa lakini mwisho wa yote hakuna soko la mazao. Naishauri Serikali kutafuta masoko kwa mazao ya wakulima wetu. Pia Serikali itoe elimu kwa wananchi juu ya usindikaji wa mazao mbalimbali kama vile mahindi ili kuongeza thamani ya mazao yetu, hii itasaidia kupata masoko ya uhakika.

Mheshimiwa Spika, Kuhusu Tafiti. Kwa kuwa tuna tatizo kubwa la kukosa soko la mahindi, naomba watumike watafiti kutafiti kwenye nchi yetu na kubaini maeneo ambayo yana chakula cha kutosha na yale ambayo hayana chakula cha kutosha, na kisha kupeleka chakula hicho kutoka maeneo ambayo hayana chakula.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.