Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Wizara ya Kilimo na kumpongeza Waziri na Manaibu wote wawili. Ombi langu ni kuhusu Skimu ya Umwagiliaji ya Lwafi iliyopo Jimboni Kwangu Katika Kata ya Kipili na Kirando. Skimu hii imegharimu pesa shilingi bilioni moja na mia nane milioni, kubwa sana haijasaidia wakulima wa mpunga wa kata hizo kabisa na wakandarasi wamepewa fedha zote hizo.

Mheshimiwa Spika, Skimu hiyo ilikuwa isaidie sana wakulima wetu, leo hii skimu hiyo ni bomu kubwa. Kusema kweli fedha iliyotumika hailingani na kazi, inaonesha wataalamu wetu hawakusimamia sawa au hawana utaalamu wa kutosha na kusababisha kupoteza pesa bilioni
1.8 bure. Naomba uchunguzi ufanywe na skimu ikamilike.