Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kumshukuru Mungu kwa majaliwa yake kwetu sote.

Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kuipongeza Serikali kwa kazi kubwa inayofanya katika kuwatumikia Watanzania.

Mheshimiwa Spika, aidha, nampongeza Mheshimiwa Rais wetu kwa kuzuia uuzaji wa Chakula/Nafaka ya chakula nje ya nchi kwa kuwa nchi yetu mwaka huu maeneo mengi yamekumbwa na ukame.

Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kuishauri Serikali kuongeza Bajeti ya Wizara hii kutokana na kwamba sekta hii huchangia zaidi ya asilimia 25 ya Pato la Taifa.

Mheshimiwa Spika, upungufu wa maafisa ugani tunaomba sana Serikali iajiri maafisa ugani walau hata kwa ngazi ya Kata kote nchini.

Mheshimiwa Spika, Serikali ichukue hatua za makusudi kupata fursa ya kuokoa mauzo ya korosho ili hata hasara itakayotokea iwe ndogo. Sote tunafahamu lengo la Serikali lilikuwa ni kukomesha hujuma walizokuwa wanafanyiwa wakulima wa korosho.

Mheshimiwa Spika, sote tunafahamu nia hiyo njema ya kumwezesha mkulima kupata faida kupitia kilimo cha korosho.

Msheshimiwa Spika, mwisho naomba Wizara kupita wataalam wake wafanye ziara katika Jimbo la Mbulu Mjini. Tulikuwa na bwawa la Tlawi, katika Kijiji cha Tlawi. Bwawa hili la Tlawi limefanyiwa usanifu wa kina mwaka 2005 na kuombewa fedha kuanzia mwaka 2009 mpaka sasa. Hata hivyo nampongeza sana Mheshimiwa Isack Kamwelwe alifanya ziara ya kutembelea eneo lililotarajiwa mwaka 2017 na kuahidi kulitafutia hela. Kwa kuwa bwawa hilo ni muhimu na wananchi wa Kijiji cha Tlawi tayari wamepeleka mawe lori hamsini (50) katika eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, hivyo basi, naomba Mheshimiwa Waziri kama tulivyo kubaliana ufanye ziara kwa ajili ya ufumbuzi wa suala hilo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na ninaunga hoja asilimia 100 kwa maslahi mapana ya taifa.