Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Eng. Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. ENG. CHRISTOPHER CHIZA: Mheshimiwa Spika, naipongeza Wizara kwa kuleta hotuba nzuri na kuibua changamoto.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri, atakapohitimisha hoja yake naomba atoe maelezo kuhusu maeneo matatu yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali ilileta muswada wa Sheria (mwaka 2013) ulioweka muundo wa Kitaasisi (Tume ya Umwagiliji) uliolenga kugatua madaraka na huduma za umwagiliaji kutoka ofisi ya kanda na kuanzisha ofisi za mikoa na kwenye halmashauri za wilaya.

Mheshimiwa Spika, hoja ya kuomba wataalam/ wahandisi wa umwagiliaji hawatoshi kusambazwa wilayani haina nguvu. Wataalamu wanaendelea kuzalishwa na wengine wanastaafu kila mwaka. Hata extension officers hadi leo hawatoshi lakini huduma za ugani zipo wilayani. Nashauri utekeleze yaliyomo katika Sheria ya Umwagiliaji kwa sababu Wabunge waliipitisha Sheria ya Umwagiliaji na Muundo wa Tume.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali; na Wizara ilianzisha mchakato wa Price Stabilization Fund kwa kuanzia na mazao ya tumbaku, kahawa, korosho na pamba. Mchakato huu umekwamia wapi? Je, bado kuna nia ya kuanzisha Commodity Exchange Market kwa ajili ya mazao ya kilimo?

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.