Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE: Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza Mheshimiwa Japhet N. Hasunga (Mb) na Naibu Waziri Mheshimiwa Omary T. Mgumba na Mheshimiwa Innocent L. Bashungwa kwa kazi nzuri ya kuiongoza Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Spika, nimependa nichangie kwa sababu naona nchi yetu inapoteza fursa kuboresha mazao na kuzalisha mazao mapya.

Mheshimiwa Spika, moja kwa kutotenga fedha za uhakika katika utafiti wa mazao na kilimo kwa ujumla. Mbili, kupiga marufuku utafiti na controlled test ya uhandisi jeni (genetic engineering. Katika eneo la utafiti, fedha tunazotenga katika agricultural research zinapaswa ziongezeke ili kukabiliana na changamoto za kuboresha mazao hasa kuongeza uzalishaji kuangalia udongo, kukabiliana na wadudu fungi, virusi na nematodes.

Mheshimiwa Spika, aidha, kumekuwa na kupanua marufuku ya genetically Modified Crops (GMO’s). Awali sheria ilikataza majaribio ya GM crops katika mashamba au kuzalisha mazao hayo ya majaribio katika mashamba. Jambo hili lilizuiliwa kisheria kwa kuweka strict liability clause. Tangazo la Katibu Mkuu wa Wizara hii Mhandisi Mathew J. Mtigumwe likapiga marufuku kabisa utafiti wote, kwenye maabara, kwenye utafiti nje ya maabara na shambani. Jambo hili limefanywa bila kujali kuwa Tanzania ndiyo nchi ya kwanza Africa katika utafiti huu (tulikuwa mbele ya nchi zote Afrika katika kutafiti wa GMO. Tumefunga maabara na kuwatawanya wanasayansi na watafiti wetu.

Mheshimiwa Spika, hatua hii inasikitisha na kuturudisha nyuma sana. Hakuna kubisha kuwa tabianchi imebadilika kwa haraka na inaendelea kubadilika. Mazao tunayotumia ikiwa hatutayabadili kuweza kuendana na mabadiliko hayo, keshokutwa tutakuwa taifa lenye njaa sana. Wakati huo, tutakuwa hatuna majibu ya changamoto ya mvua kidogo, mvua inayonyesha kwa wiki tatu badala ya miezi mitatu, ongezeko la joto (evaporation) ongezeko la aina ya wadudu na idadi yao, virusi na visumbufu vingine, upungufu wa unyevu kwenye hewa na kwenye udongo.

Mheshimiwa Spika, maamuzi yetu yanatuchelewesha sana. Nchi yetu imefanya utafiti tayari na kuwa na mbegu yake ya GMO cotton (inaitwa Bt cotton Duniani). Hii ni kwa kuwa takriban nchi zote duniani zinazolima pamba zinazalisha na kutumia Bt cotton. Mfano wa nchi hizo ni India, Pakistan, China, Russia, USA, Brazil, Uganda, Kenya, Sudan, Egypt, Nigeria, Niger , Mali, Burkina Faso n .k. Ukiangalia ni Tanzania tu ambayo inakataza wakulima wake kutumia mbegu za Bt. Cotton.

Mheshimiwa Spika, Bt cotton inatoa longer lint (hivyo bei bora); inazalisha 3,000 kg cotton/na ukilinganisha na mbegu za kienyeji tunazotumia. Inakinzana na wadudu na visumbufu vya pamba hivyo huhitaji kupulizwa dawa (viuatilifu) mara tatu badala ya mara sita mpaka saba kwa msimu, na huhimili upungufu wa unyevu kwenye udongo. Aidha, kwa Tanzania ni muhimu kutumia Bt cotton kwa kuwa inakinzana na red american ball worm, hivyo kwa kutumia Bt cotton hatuna haja ya kuzuia kilimo cha pamba katika Wilaya ya Chunya, Rufiji, Lindi, Mtwara, na Wilaya zingine za Kusini.