Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. DKT. SUSAN A. KOLIMBA: Mheshimiwa Spika, naomba kuipongeza sana Serikali kupitia Wizara ya Kilimo kwa juhudi kubwa wanayoifanya katika kuhakikisha wanatatua changamoto zinazojitokeza katika sekta hii muhimu kwa taifa, sekta ya kilimo; ikiwemo utafutaji wa masoko kwa mazao ya kimkakati.

Mheshimiwa Spika, pamoja na pongezi hizi naomba kuishauri Serikali kutafuta masoko ya mazao ndani na nje ya nchi yetu. Mazao hayo ni pamoja na zao kama mahindi, viazi, maparachichi, mananasi matunda mengine kama maembe, apples, nk yanayolimwa katika Mkoa wetu wa Njombe.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali (Wizara ya Kilimo) kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya TAMISEMI ili kufanya utafiti katika Mikoa ili kujua wapi wamezalisha zao gani kwa wingi na mikoa ipi ina uhitaji wa zao hilo. Kwa mfano Njombe wanazalisha mahindi kwa wingi na mara nyingi wakulima wanavuna wanapata changamoto kubwa ya kuuza mahindi hayo ilhali kuna mikoa au wilaya nyingine zina uhitaji mkubwa wa chakula kama mahindi, maharage n.k. Kwa mfano mwaka jana Wilaya ya Longido walikuwa na uhitaji mkubwa wa chakula ikiwemo wananchi wa wilaya ya Ludewa/Njombe walikuwa na mahindi ya kutosha.

Mheshimiwa Spika, Masoko Nje ya Nchi. Naipongeza Serikali kwa kupata masoko ya nje ya nchi. Kuna baadhi ya mazao kama mihogo, maparachichi n.k; naendelea kuishauri Serikali kuitumia Wizara ya Mambo ya Nje kupitia mabalozi walioko ndani na nje ya nchi ili kuweza kupata masoko ya maparachichi, mahindi, maharage na viazi; nchi kama vile Sudan Kusini, nchi za Falme za Kiarabu, nchi za SADC na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, Upatikanaji wa Pembejeo. Naomba kuipongeza Serikali kuweka mikakati ya upatikanaji wa pembejeo ikiwemo mbegu, mbolea na viuatilifu vilivyowafikia wakulima kwa wakati. Niishauri na kuiomba Serikali kuhakikisha mbegu bora ikiwemo mbegu za mahindi, viazi mviringo, maharage na maparachichi kwa Mkoa wa Njombe vinasambazwa kwa wakati na kusimamiwa vizuri ili kuwafikia wakulima kwa wakati sahihi.

Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali/Wizara kwa kutoa mafunzo ya uongozi wa mbolea kwa maafisa kilimo kutoka Mkoa wa Njombe ili kuweza kuleta tija katika kilimo. Naomba Wizara itoe mafunzo kwa wafanyabiashara wa mbolea wa Njombe kama ilivyofanya katika mikoa mingine.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Wizara hii.