Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. RHODA S. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, Sekta ya Kilimo inachangia 29.1% ya Pato la Taifa endapo tutaongeza juhudi katika uzalishaji huenda Sekta ya Kilimo ndio ikaleta mageuzi makubwa nchini. Changamoto tuliyonayo ni kufeli kwa mipango ya Serikali yetu kufungamanisha miradi mikubwa ya kiuchumi na Sekta ya Kilimo sambamba na mikakati ya kuongeza thamani kwenye uzalishaji wa Sekta ya Kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwenendo wa takwimu za hifadhi ya chakula nchini tangu 2015 mpaka 2019 zinaonesha kiwango cha uzalishaji wa chakula kimeshuka kwa asilimia kubwa na inatisha. Nimeangalia takwimu zilizotumiwa na Benki Kuu Aprili, 2019 hifadhi ya chakula imeshuka kwa 82.7 kutoka mwezi Machi, 2019. Ukiangalia takwimu hizo utaona Machi, 2015 hifadhi ya chakula ilikuwa tani 452,054.0 lakini kufikia Machi, 2019 hifadhi ya chakula imeshuka mpaka 78,336.0.

Mheshimiwa Spika, matumizi ya ardhi kuongeza uzalishaji. 53.3 ya ardhi yetu ni misitu na 15.4 iliyobaki ni ardhi yenye rutuba. Sehemu kubwa ya ardhi yetu hapa nchini inafaa kwa kilimo ila uzalishaji wetu umeendelea kushuka siku kwa siku. Kumekuwa hakuna utoshelevu wa kutosha wa chakula ili hali tuna ardhi yenye rutuba isipokuwa tuna maarifa duni ya kuongeza kiwango cha uzalishaji. Endapo tungekuwa na utoshelevu wa kutosha wa chakula basi hata ujenzi wa reli ya standard gauge unapaswa kutumika kusafirisha chakula Afrika Mashariki, DRC Congo, Burundi na Uganda na Rwanda.

Mheshimiwa Spika, takwimu za uagizaji chakula nje ya nchi na bei za vyakula; Bei zimeshuka na kuumiza wakulima. Uagizaji umeongezeka kutoka dola milioni 13.3 mwezi Machi, 2018 mpaka kufikia dola milioni 15 Machi, 2019.

Katika mazao sita makuu mazao manne bei zimeshuka, Machi, 2018 gunia la mchele 185.735.4 na sasa 168,520.5 kwa 9.3. Maharage ilikuwa 170,140 na zaidi imefika 165,3000 na zaidi kwa 2.8%. Uwele gunia kutoka 76,712.1 sasa ni 75.677.4 kwa 1.3%. Gunia la viazi 67033.8 imeshuka kwa 1.9 mpaka 68,302.9. Mtama 148.8371 mpaka 134,724.3 hatujafanya juhudi za kutosha kutumia sehemu ya ardhi yenye rutuba.

Mheshimiwa Spika, mapendekezo yangu ni kama ifuatavyo:-

(a) Ifanyike juhudi ya kuongeza thamani ya mazao kama matunda kwa kufanya packaging na processing ya matunda juice.

(b) Kuweka mazingira bora ya kisheria na kisera kwa sekta binafsi kujenga viwanda na kuchakata korosho.

(c) Kuweka mazingira bora ya kisera na kisheria kwa sekta binafsi ili kujenga viwanda vya kukamua mbegu za mazao kama alizeti.

(d) Kuweka mazingira bora ya kisera na kisheria kwa sekta binafsi kujenga viwanda vya utengenezaji wa nguo textile industries pamba inayozalishwa nchini ni nyingi 20 peke huchakatwa nchini.