Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Spika, kuhusu vikwazo vya kufikisha pembejeo (mbolea, viatilifu na mbegu bora) kwa wakulima wadogo vijijini na hivyo kupoteza tija; wakulima wengi wadogo wapo vijijini ambako ndiko pia shughuli za kilimo zinafanyika. Maduka ya pembejeo kwa sehemu kubwa yapo mijini. Tanzania mkulima mdogo apate pembejeo ni lazima asafiri hadi mjini kununua. Hili linaongeza gharama za uzalishaji kwa mkulima mdogo.

Mheshimiwa Spika, ili kuongeza tija haina budi maduka ya pembejeo yasambae hadi vijijini ambako wakulima wapo. Katika maeneo mengi wajasiriamali vijijini wanafanya jitihada za kufungua maduka ya pembejeo ili kufikisha huduma karibu na wakulima. Jitihada hizi zinakwamishwa na gharama kubwa za vyeti vinavyotakiwa. Vyeti ni kama ifuatavyo:-

(1) TOSCI = 100,000.
(2) TPRI = 320,000.
(3) TFRA = gharama ya chakula wakati wa mafunzo. (4) TFDA = 100,000.
(5) Leseni = 71,000.

Jumla ni 591,000

Mheshimiwa Spika, gharama hizi ni kubwa sana, zinakatisha tamaa kwa wajasiriamali. Wapo wengi wameshindwa licha ya kushiriki mafunzo na kujengewa hamasa bado wameshindwa kufungua maduka. Mifano halisi ni, katika Mkoa wa Kagera wajasiriamali 461 walijengewa hamasa na kupata mafunzo ya biashara hiyo kupitia Shirika la AGRA matokeo yake ni kama ifuatavyo:-

Waliopata mafunzo na kujengewa hamasa ni 461, Cheti TOSCI (82), Cheti TFRA (108), Cheti TPRI (17), WALIOFUNGUA MADUKA (139)

Mheshimiwa Spika, katika Mkoa wa Kigoma, kati ya Wajasiriamali 704 waliojengewa hamasa na kupatiwa mafunzo ya biashara na Shirika la AGRA ni wajasiriamali 389 tu ndiyo wamefungua maduka. Aidha, wajasiriamali 159 walipata mafunzo na TFRA Mwezi Oktoba, 2018 lakini hadi leo hawajapata vyeti vya TFRA ili kuwezesha kuanzisha maduka ya pembejeo vijijini. Utaratibu huu kama hautabadilika, ukuaji wa sekta hii utaendelea kudorora.

Mheshimiwa Spika, ushauri; Serikali iangalie upya ada hizo (TOSCI, TFRA, TPRI, TFDA) ziangaliwe upya au Serikali ibebe huo mzigo ili kuwezesha ufikishaji mbolea, viatilifu, mbegu bora kwa wakulima wadogo.