Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. MARGRET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, nawapongeza sana kwa kazi kubwa Mheshimiwa Waziri, Waheshimiwa Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu na wafanyakazi wote wa Wizara na Taasisi zake, hongera kwa kazi nzito wanazofanya.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu, kwa niaba ya wananchi wa Urambo, naomba wafanyie kazi kwanza upatikanaji wa pembejeo kwa wakati, hususan mbolea. Kwa mfano, sisi tunaolima tumbaku inabidi tupate mbolea kabla ya mwezi Agosti na kwanza, bei ipunguzwe. Pili, ili wakulima walime zaidi masoko ya mazao yawe ya uhakika na tatu, wanunuzi wawe wengi ili ushindani wa bei uwepo kwa manufaa ya wakulima wetu na wananchi kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, nina maswali yafuatayo:-

Kwanza, kwa kuwa kampuni ya TLTC ilikuwa mnunuzi mkubwa wa tumbaku kwa tani zipatazo milioni 14 kwa msimu; je, Serikali imejipanga vipi kuhakikisha kuwa iwapo kampuni hii itajitoa wakulima wasikose makisio msimu ujao na wakiondoka pengo lao litazibwa na nani?

Pili, je, kuna makubaliano yoyote kati ya BAT (British American Tobacco) katika kuwa wanunuzi wa tumbaku?

Tatu, je, Serikali ina mpango gani kuhusu bima kwa wakulima na mazao yao?

Mheshimiwa Spika, mwisho, kwa niaba ya wananchi wa Urambo tunaomba mtaalam wa zao la alizeti aje atuambie mbegu ipi ni nzuri kwa ardhi yetu.