Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. HASNA S.K. MWILIMA: Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kuchangia kwa maandishi. Kwanza niwapongeze Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri pamoja na Watendaji wote wa Wizara. Zao la michikichi ni zao linalolimwa Mkoa wa Kigoma na ndiyo asili ya zao hili, japo kwa siku za hivi karibuni, mikoa mingine ya Tanzania nayo inalima zao hili la michikichi. Zao hili linatupa mafuta ya mawese, tunapata mafuta ya mise, tunapata chakula cha mifugo, tunapata na sabuni. Mheshimiwa Waziri Mkuu ameamua kwa makusudi kulisimamia zao hili, binafsi nimshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa namna ambavyo amewekea mkazo zao hili la michikichi.

Mheshimiwa Spika, ombi kwa Serikali, naomba Wizara isituletee pesa bali itununulie miche ya michikichi ya miaka mitatu ili wananchi wapewe miche na kuanza kupandikiza miche hii ya muda mfupi.

Mheshimiwa Spika, ombi la pili kwa Serikali kupitia Wizara hii ya kilimo, tunaomba mbege kwa kuwa wakulima wa zao hili hawana pesa, wala hawana namna ya kupata hizo mbegu, miche ya michikichi.

Mheshimiwa Spika, ombi la tatu, mashine za kuchakata mafuta ya mawese, kwani kwa sasa wanatumia magogo kukaa watu wanne na kuzunguka hadi jasho jembamba kuwatoka ndiyo wapate mafuta ya mawese. Natambua SIDO wanazo machine za kuchakata mafuta, ni bora wapewe machine kwa mkopo watarejesha pindi watakapopata pesa kwa kuuza mafuta yao. Sambamba na mashine za kukamua mafuta safi na salama ya mise pamoja na machine za kuchakata sabuni, kwa kufanya hivyo Tanzania ya viwanda itakuwa imekamilika.

Mheshimiwa Spika, Tarafa ya Nguruka ni Tarafa yenye wakulima wengi wa za la tumbaku lakini zao hili limekuwa na changamoto nyingi sana, ikiwepo changamoto ya wakulima kubambikiziwa madeni na vyama vya msingi kuwalazimisha wakulima kuchukua mikopo hata kama hawataki siku bank wakiendelea kumdai aliyekopa wanawafilisi wote hata wale wasiokopa.

Kwa hoja, hiyo niombe Waziri au Naibu Mawaziri kupanga ziara ya kuja Uvinza na kusikiliza kilio cha wakulima wa tumbaku, pamoja na changamoto ya kukosa mbolea, mbegu na madawa ya viuatilifu ya kuulia wadudu. Natambua hivi karibuni Wizara ya Muungano chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais imepiga marufuku mifuko ya plastic ifikapo 1/7/2019, Kigoma tunalima mihogo Mkoa wote. Tunaomba Wizara ituletee mbegu ili basi wananchi walime mihogo kwa wingi, kuwezesha viwanda vya kutengeneza karatasi vifunguliwe kwa wingi kwani malighafi zitapatikana.

Mheshimiwa Spika, Uvinza tunalima alizeti, kahawa na ufuta lakini tatizo ni mbegu na pembejeo zote kwa ujumla. Niiombe Wizara ya Kilimo kutuletea mbegu za alizeti, ufuta, kahawa na mpunga tunayo mabonde mengi yanayolimika mwaka mzima hata kama hakuna mvua. Sambamba na ombi la pembejeo na mbegu, tunatambua Wizara ina mpango wa ASDP unaowezesha kujenga maghala, tunaomba Halmashauri ya Uvinza tupatiwe maghala Vijiji vya Kashagulu, Mgambazi, Nguruka, Mganza, Basanza na Ilagala.

Mheshimiwa Spika, baada ya mchango wangu huu, naomba kuunga mkono hoja.