Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia kwenye Wizara hii muhimu sana na vilevile niseme kwamba hii ni sekta ambayo inatoa chakula kwa asilimia mia moja kwa Watanzania na inatoa ajira kwa asilimia 65. Inatoa malighafi kwa Viwanda kwa asilimia 65, jamani sio Sekta ya kupuuza, lakini leo napenda sana kujielekeza kwenye suala moja tu kama ulivyotuelekeza ni suala la umwagiliaji.

Mheshimiwa Spika, suala la tabianchi kubadilika linajulikana kwa kila mmoja na nafikiri ni muhimu sana kwa Waziri wa Kilimo kulifahamu hilo, bila kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi hili suala la chakula, suala la kupata malighafi kwa viwanda, suala la ajira ya watu wengi na mambo mengine ambayo sitayasema sasa hivi litakuwa halina maana yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sina hakika, labda mimi mwenyewe sijaiona, suala la umwagiliaji halijapewa umuhimu unaotakiwa kwenye hotuba hii ya Mheshimiwa Waziri, naomba atueleze kwa nini ni kwa sababu tu ndiyo imehamia kwake. Pamoja na hilo sisi watu wa Hanang, tuna miaka kumi tuliomba kuchimbiwa Bwawa la Gidahababieg ambalo linakusanya maji ya Mlima Hanang yote kwenye eneo ambalo ni kavu na hawana uhakika wa chakula, kwa nini Mheshimiwa Waziri hajaorodhesha miradi ambayo katika bajeti hii itapewa hela ningeweza kujua kama Gidahababieg ipo au haipo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba sana na Mheshimiwa Waziri, Wilaya ya Hanang ni moja ya Wilaya ambayo ina udongo mzuri sana, ndiyo Wilaya ambayo inalima sana, lakini mvua siyo za uhakika. Kwa hiyo masuala ya Mabwawa ni muhimu sana, pamoja tunajua kwamba kuna upungufu kwenye maeneo mengine ya kilimo, lakini naomba leo niseme kwamba, kama tunataka tutumie udongo huo mzuri wa Hanang na Mkoa wa Manyara kwa ujumla, hatuna jambo lingine isipokuwa kukazania mabwawa ili watu wapate maji lakini vilevile kilimo kipate maji na mifugo vilevile ipate maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wilaya yetu ya Hanang ukiangalia tukichimba hata mita 200 ya visima hatupati maji. Kwa kweli ni mabwawa yanayotakiwa ni makubwa, wananchi wetu wanajitahidi hata wanachimba wenyewe mabwawa lakini wanahitaji kwa kweli msaada wa Serikali kwa mabwawa makubwa kwanza kwa kufanya survey, lakini kwa kuchimba mabwawa kwa namna ambayo inatakiwa kwa ufundi. Kwa hiyo naomba sana, naunga mkono hotuba hii na naunga mkono bajeti hii na ukiangalia Waziri katengeneza kitabu kizuri sana, lakini kitabu hiki basi kiweze kuwasilisha manufaa kwa wananchi. Kwa mwaka huu kwa Wilaya ya Hanang ni kujua kwamba Bwawa la Gidahababieg litachimbwa na sisi tuweze kunufaika na Mwenyezi Mungu ambariki sana Mheshimiwa Waziri katika kazi yake hiyo mpya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono bajeti hii na yote ambayo anayafanya Waziri. Ahsante sana. (Makofi)