Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuchangia katika Wizara hii ya kilimo. Kwanza kabisa naomba nichukue nafasi kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri, Manaibu wote Mawaziri wa Wizara hii kwa kazi nzuri sana ambayo wamekuwa wakiifanya kwa kipindi kifupi ambacho wamekuwa katika Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kutokana na muda kuwa mchache, naomba niende moja kwa moja kwenye hoja. Kwanza kabisa nichangie kuhusiana na changamoto katika vituo vya utafiti. Kwa kweli mimi ni mjumbe, tumetembelea katika hivi vituo, hali ya vituo ni mbaya mno. Ningeomba Serikali sasa itambue umuhimu wa vituo vya utafiti, ili sasa tuweze kufanya utafiti wa uhakika katika mbegu, magonjwa, dawa za tiba, viuatilifu, udongo, ili tuweze kutenda haki kwa wakulima wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia, nizungumzie kuhusiana na NDC, inafanya kazi nzuri sana za kuwakopesha wakulima zana za kilimo za kisasa. Je, wakulima wanatambua kuhusiana na haya matrekta kwa sababu, ni bei rahisi na tunategemea kwamba, kama wakulima watapata matrekta yatasaidia kulima kilimo cha kisasa ambacho kitaleta tija katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, lakini moja kwa moja niende katika Mkoa wangu wa Iringa kuhusiana na zao la pareto. Hili ni zao la biashara katika Mkoa wetu wa Iringa, linatuingizia pato katika mkoa wetu na katika nchi hii, lakini kuna kiwanda ambacho kiko katika Wilaya ya Mufindi. Vilevile tushukuru kwamba, katika hiki kiwanda kinahitaji kama tani 5,000 za maua ya pareto, lakini kuna walanguzi ambao wamekuwa wakija kuwarubuni wakulima katika hili zao la pareto kwa sababu, sasa hivi kiwanda kinapata maua kama tani 2,500 tu na kiwanda tushukuru kwamba, wamekuwa wakiwa- support wakulima kwa kuwapa pembejeo na utaalam, tuwapongeze sana, lakini sasa je, Serikali inalindaje viwanda kama hivi na inalindaje wakulima?

Mheshimiwa Spika, inalindaje kuhakikisha kwamba, walanguzi hawaji kulangua malighafi katika maeneo ambayo wakulima wanafanya maana tunaelekea kwenye uchumi wa viwanda. Sasa kama Serikali itakuwa haina mpango mzuri, mkakati wa kuhakikisha kwamba, inalinda hivi viwanda bado tutakuwa tunapiga mark time. Sasa niombe je, hakuna sheria inayolinda viwanda ambavyo vinawekeza katika nchi yetu?

Mheshimiwa Spika, vilevile nizungumzie kuhusiana na masoko. Tatizo kubwa la mkulima ni masoko. Nyanda za Juu Kusini tunalima mahindi, pareto, parachichi, viazi, lakini mkulima leo hii anapolima hajui soko atalipata wapi, lakini kuna Bodi ya Mazao Mchanganyiko ambayo tulikuwa tunategemea kwamba, sasa itatusaidia kututafutia masoko, lakini bado unaona kwamba ina changamoto kubwa sana, haipatiwi fedha za kutosha kuhakikisha kwamba, inafanya kazi inayotakiwa; sasa je, Serikali mmejipangaje? Maana bila soko bado wakulima wetu wamekuwa maskini.

Mheshimiwa Spika, mkulima wa leo hawezi hata kumsomesha mtoto. Mkulima wa leo yani analima, lakini wanaofaidika ni wale walanguzi. Sasa ifike sehemu Serikali hii imwezeshe mkulima, ili ajisikie kama wakulima walivyo katika nchi nyingine wanapata heshima. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie Benki ya Kilimo; Benki ya Kilimo tulikuwa tunategemea itusaidie katika kuhakikisha kwamba, mkulima anakopesheka, kwa sababu, mkulima wa sasa hivi hakopesheki kutokana na risk kubwa ambazo anazo. Tuombe kwamba, bima ya mazao iwekewe udhibiti, ili aweze kukopesheka, lakini tuombe benki hii iongezewe mtaji wa kutosha...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)