Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante niungane na wenzangu kupongeza Wizara kwa kazi nzuri wanayoifanya. Pamoja na pongezi hizo naomba niende moja kwa moja katika mambo ambayo nakusudia kuyachangia. Nakusudia kuchangia mambo yafuatayo; kwanza kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri ukianzia ukurasa ule wa 29 mpaka 32 wamezungumzia kuhusiana na suala la zao la korosho. Na zao la korosho katika maeneo yafuatayo;

Mheshimiwa Spika, kwenye ule ukurasa wamezungumzia suala la uzalishaji wa miche ambalo lilifanyika katika msimu wa 2017/2018. Ninachokumbuka kwamba kupitia Bodi ya Korosho walitoa maelekezo kwa halmashauri ili waandae vikundi wazalishe miche ile ya korosho na wote tutakuwa mashahidi miche ambayo ilizalishwa ilipelekwa katika maeneo mengi katika na wameeleza ni mikoa 17 ambayo ilipelekwa miche ile.

Mheshimiwa Spika, mpaka hivi ninavyosimama hapa wako wanavikundi ambao waliingia mikataba na Bodi ya Korosho hawajalipwa pesa zao niombe Mheshimiwa Waziri atakapokuja alizungumze hili kuona namna gani kwa sababu tunapozungumzia wanavikundi tunagusa jamii zetu na ni watu ambao wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu sasa walifanya hii kazi lakini mpaka leo unapozungumza hawajalipwa. Nikuombe Mheshimiwa Waziri utakapokuja kutoa ufafanuzi tueleze ni kwa nini hawajalipwa na vinginevyo nitashika shilingi kwa mara ya kwanza nakusudia kushika shilingi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo jingine ambalo nakusudia kuzungumza ni suala la ujenzi wa maghara, nafahamu kwamba yako maeneo ambayo tulikuwa tunaendelea kujenga maghara napozungumza maghara ni yale maghara ambayo tunafikiria kwa ajili ya uhifadhi wa korosho. Kuna Mkuranga na kuna Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru na tayari ujenzi huuulianza lakini ninapozungumza sasa hivi ujenzi huo umesimama, niombe Mheshimiwa Waziri atueleze tutamaliza lini yale majengo.

Mheshimiwa Spika, nimeshawishika kulisema hili kwa sababu hivi tunavyoendelea tunaingia katika mfumo wa ununuzi wa Ufuta na tu na tunapozungumza sasa korosho nyingi ziko maghalani, sasa sijui itakuwaje kwenye hili jambo kwamba Ufuta unatakiwa uingie kwenye maghala lakini maghala yamejaa korosho mpaka korosho hazijaondolewa, kwa hiyo niombe Mheshimiwa Waziri utakapokuja pia utuambie ule ujenzi utakamilika lini, kwa sababu tulipanga sisi kupitia Serikali yetu lakini bado hatujakamilisha ujenzi wa maghala likiwemo ghala lile katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru lilitengewa pesa ilitoka pesa kidogo na sasa ujenzi umesimama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo jingine naomba nizungumze suala la Maafisa Ugani, baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wenzangu wamelisema lakini pia naomba niliseme tunazungumza kulima kilimo cha kisasa. Naomba niseme kutoka kwenye sakafu ya moyo wangu wako wakulima wetu mpaka hivi tunavyozungumza hawajui hata namna ya matumizi ya hizi pembejeo sasa ili waweze kutumia pembejeo ni pamoja na kuwepo Maafisa Ugani katika vijiji vyetu ili waendelee kuwaekeleza wakulima wetu katika kulima kilimo bora na chenye ufanisi.

Mheshimiwa Spika, nimelazimika kushawishika kuyasema haya kwa sababu ni miongoni mwa Wabunge wanaotoka katika Mkoa wa Ruvuma na sisi Ruvuma ina wakulima tunalima kilimo cha chakula, lakini pia tunalima kilimo cha biashara ili tuwasaidie wananchi wetu ni pamoja na kuwapeleka Maafisa Ugani na hii ni sera kabisa lazima wawepo Maafisa Ugani, kwa hiyo suala la Maafisa Ugani kwanza ikumbukwe tunao wachache lakini hata wale tuliokuwa nao hawafanyi kazi ipasavyo, wengine wanageuka kuwa wanasiasa, lakini kuna sintofahamu katika ya Afisa Ugani anayeshughulika na masuala ya uvuvi na anayeshughulika na masuala ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukija kwenye vijiji vyetu akimuono Afisa Ugani anayehusika na masuala uya uvuvi ana amini kwamba anaelewa na masuala ya kilimo, sasa niombe kupitia hii Wizara na masuala ya mifugo niombe kupitia Wizara tuone uwezekano wa kuwapeleka Maafisa Ugani ili waendelee kuwasaidia wakulima wetu. (Makofi)

SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Sikudhani.

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante naunga mkono hoja mambo ni mengi lakini muda mchache ahsante sana. (Makofi)