Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kupata muda wa kuchangia. Nataka kuiomba Wizara itoe taarifa rasmi hapa kuhusiana na suala zima la Mradi huu wa SPD II utaanza lini na kama umeanza, umeanza wapi na vipi hatuelewi chochote mpaka leo zaidi ya miaka miwili sasa hivi toka umezinduliwa hakuna tunachokiona kinaendelea katika eneo hilo, kwa hiyo, tunaomba Serikali au Wizara itupe maelezo ya SPD II na ile mipango iliyokuwepo katika ule mradi inakwendaje.

Mheshimiwa Spika, la pili vilevile kuitaka Wizara hasa kwenye kile kitengo chake cha Early morning iweze kuwa inatoa maelezo sahihi kitu ambacho niseme wazi kwamba kimesababisha hasa wakulima wa mikoa zaidi ya nane ndani ya nchi hii kuweza kupata na janga la njaa kidogo yaani upungufu wa mazao kwa sababu kimeshindwa kutoa taarifa sahihi za hali ya hewa au hali ya mvua inavyonyesha au ukame utakavyotoka, kitu ambacho kwa kweli hawatutendei haki kama Watanzania. Kitengo kile kipo kina taarifa ambazo wanazipata kutoka meteorological agent lakini hawatoi taarifa wamekaa kimya watu wanalima hawajui hatima yao na watu wanategemea mvua. Kwa hiyo, tunataka utupe maelezo kipi kilichosababisha kwamba mpaka wakashindwa kutoa maelezo safari hii watu mikoa mingine ikaweza kupata upungufu wa mvua.

Mheshimiwa Spika, lakini jingine nilitaka kulizungumza kwamba Serikali au Wizara kwa ujumla wake imeondoa mkono wake kutoka SAGCOT zile shughuli ambazo tulikuwa tunaziona ambazo zinasadia wananchi kuwekeza katika kilimo hasa mikoa ile ambayo ya Kusini ina mfumuko mkubwa wa uzalishaji lakini leo hii SAGCOT tunaiona inaanza kuelekea kulikokuwa siko. Kwa hiyo nitoe angalizo kwa Serikali pale ilipokuwa inaona kwamba imekosea irudi kwenye mstari SAGCOT ndio mkombozi ilikuwa kwa maeneo ya mikoa ya Kusini lakini imeelekea sasa hivi mikoa ya Pwani na mikoa mingine tunaihitaji SAGCOT irudi kwenye progress hali inayokwenda sasa hivi sivyo, hilo lazima tulizungumze. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jingine ambalo tulitaka kuona kwamba Serikali ijikite kwenye mbegu bado Tanzania tumekuwa jalala la mbegu feki mpaka leo kiwango ambacho nchi inaweza kutoa mbegu ndani ya nchi ni asilimia 12,15 mbegu zote zinatoka kwa Belgium, zinatoka South Africa, zinatoka nchini Kenya na nchi nyinginezo kitu ambacho watu wanatumia nafaasi hiyo kuingiza mbegu feki. Makampuni haa ambayo tunayaita yako hapa nchini ya KIBO, SIDCO sjui mengine ambayo yako Arusha hayazalishi mbegu yanafungasha mbegu ambazo inakaa miaka chungumzima huko kwao na zikiletwa hapa ile variability inakuwa imeshapotea kwa hiyo, hazioti na zinawatia hasara wakulima. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Salum Rehani.

MHE.SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana naunga mkono hoja. (Makofi)