Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo Zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Nne na Mkutano wa Kumi na Tano wa Bunge

Hon. Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo Zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Nne na Mkutano wa Kumi na Tano wa Bunge

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia taarifa ya Kamati yangu ya Sheria Ndogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uhai, baada ya hapo napenda kuishukuru Kamati ya Sheria Ndogo ikiongozwa na Mtemi Chenge kwa kazi kubwa ambayo inafanya kila siku ya kuchambua Kanuni zote za Wizara zote zilizopo nchini Tanzania, Kamati hii imekuwa ikipitia Kanuni zote ambazo zinatumika kwenye Wizara zote ambazo zilizopo katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuzirekebisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Makatibu wa Kamati hii nawapongeza sana na ninapenda niseme ndani ya Bunge hili Makatibu wa Kamati ya Sheria Ndogo wamekuwa na kazi kubwa sana kupitia Kanuni ambazo huwa zinaletwa kwenye Kamati yetu ambazo zimeandikwa zimekosewa, naomba nitoe wito kwa Waandishi wa Sheria ambao wanaandika Kanuni hizi ambao wapo kwenye Wizara tofauti tofauti wawe makini wanapoandika hizi sheria, zinapoletwa kwenye Kamati, kila siku Makatibu wanakesha kuzichambua kuzioanisha kutoka kwenye Kanuni kupeleka kwenye Sheria Mama, mfano sheria labda ni ya Wizara ya Ardhi inatunga kanuni ya Wizara ya Ardhi unakuta kifungu hakiendani na Sheria Mama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu kinasema vingine Kanuni inasema vingine, hii inaleta matatizo kwa wananchi kwa sababu hizi sheria mnaisema kwamba ni sheria ndogo hizi sheria siyo ndogo ndiyo sheria ambazo mwananchi wa kawaida anaishi nazo na anaziishi kila siku, kila siku anaishi kwa zile Kanuni, mwananchi wa kawaida haishi kwa kufuata zile Sheria Mama, Sheria Mama inapotungiwa Kanuni zile Kanuni ndiyo zinambana mwananchi wa kawaida.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishauri Serikali najua kuwasomesha Waandishi wa Sheria ni gharama lakini naomba niishauri Serikali itumie pesa kusomesha waandishi wa sheria kwa sababu waandishi wengi wa sheria wamestaafu wameshafika miaka 60 wamestaafu mfano mzuri hata huyu Mwandishi mzuri hata huyu Mwandishi aliyekuwepo hapa Bungeni Mama Kibagana sijui nimekosea jina lakini kuna Mama ambaye alikuwa anaandika sheria hapa Bungeni amestaafu mwaka jana, kwa hiyo tuna CPD mpya yuko hapa, lakini wengi waliokuwa trained miaka ya nyumba wanakwenda miaka 60 kama hana miaka 60 na 58 kwa hiyo atastaafu hivi karibuni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali itumie pesa kusomesha Waandishi wa Sheria ili sheria zetu zinapotungwa zitungwe vizuri na kwa sababu nchi kama nchi inaishi na sheria na inatunga sheria kila siku, sasa sheria zinapokosewa zinaletwa pale sisi tunaanza kuchambua tena kwa kweli inaleta shida, niombe sana Serikali izingatie hili tutumie pesa tupate waandishi wazuri.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ambacho ningeweza kusema ni kwamba Kanuni ambazo zinatungwa kwenye Wizara kila Wizara inapotunga zile kanuni iangalie zile kanuni zisiwe kandamizi kwa wananchi kwa sababu zile kanuni ndiyo wanazoenda kuzitumia mtaani, sasa unapoweka kanuni ambayo inambana sana mwananchi wa kawaida unamuongezea matatizo. Kanuni ziangalie wananchi watakapoenda kutumia hii kanuni itakuwa ni friendly na wataishi nayo, siyo kanuni ambayo unatunga leo, inambana mwananchi anashindwa hata kuishi kwa sababu ya hiyo kanuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo ningependa kuchangia hayo machache kwenye Kamati yetu kwa sababu kanuni zote zililetwa hapa na tulizipitia tumejaribu kuzirekebisha lakini niombe tu labda wale Waandishi wa Sheria wanapoandika wajaribu kuwasiliana na yule Mpiga Chapa wa Serikali ili wanapochapa wasiweze kubadilisha vile vifungu kwa sababu mara nyingi unakuta kama ni kifungu ni 53 lakini kanuni imeshuka huku chini alafu imekosewa, labda Mpiga Chapa pia anaweza akawa ana matatizo katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga hoja. (Makofi)