Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii. Nami najikita kwenye Azimio la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Afrika (SADC) kuhusu kulinda hatimiliki ya Wagunduzi wa Aina Mpya za Mbegu Pamoja na Mimea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu hawa, wagunduzi, ambao wamefanya utafiti wao wa muda mrefu, kama hii ikiridhiwa itakuwa nzuri sana kwa sababu ya kupata motisha. Watakuwa wanamotisha sana na wataona kuwa wametambuliwa na watazidi kufanya utafiti wao kusudi waweze kupata huo ugunduzi na waweze kugundua aina mpya za mbegu pamoja na mimea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Azimio hili likiridhiwa, nchi yetu nayo itaweza kufaidika kwa njia mbalimbali kupitia mapato kwa sababu aina mpya hii ya mbegu za mimea tunaweza kubadilishana pamoja na nchi nyingine za SADC kwa njia ya uhalali. Hapo mwanzoni ilikuwa haibadilishwi kwa njia ya halali kwa sababu tulikuwa tumejifunga kwenye nchi yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, vijana wetu na wenyewe watapata motisha kuweza kuchukua haya masomo ya Plant Breeding ambayo yatawawezesha kufanya utafiti na kugundua aina hizi mpya za mbegu za mimea kusudi waweze kutambulika na waweze kuendelea vizuri pamoja na nchi yetu kuweza kunufaika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tulivyosema kwenye Kamati, nchi yetu itaweza kufaidika pamoja na wagunduzi kwenye mrabaha ambao pia unaweza kutumika mrabaha mwingine kuendeleza ugunduzi mpya kwenye mambo haya ya aina mbegu za mimea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe mwenyewe na watu wengine walikuwa wanafahamu kuwa tatizo la mbegu hasa hapa nchini ni kubwa sana, lakini kwa kuridhia huu mkataba, hawa watafiti baadaye wakigundua na kuwa wagunduzi, wataweza kujikita sana kwenye tafiti zao na kugundua aina mpya za mbegu za mimea ambazo zitaweza kuzalisha mbegu nyingi hapa Tanzania na tutaweza kupata mbegu hizi kwa urahisi bila matatizo yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikisema wagunduzi, simaanishi wale ambao wamesoma tu, kuna wagunduzi wakulima ambao na wenyewe wanagundua na hawa wakulima na wenyewe itawalinda kusudi waweze kugundua aina mpya za mimea pamoja na mbegu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajira itazidi kuwepo kwa sababu vijana wengi na wakulima watajikita kwenye ugunduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo ambalo naweza kuongelea hapa ambalo nchi yetu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante. Dakika tano zako zimekwisha. Mheshimiwa Eng. Chiza.

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa hilo. Ahsante sana. (Makofi)