Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nashukuru kupata nafasi na kama wenzangu walivyosema na mimi naunga mkono maazimio haya ya Bunge ya kuridhia ubadilishaji na kuongeza hadhi haya mapori kama ilivyokuwa imetajwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nipende kusema mambo machache. La kwanza kama ambavyo pia Kamati imesema sasa hivi tunaenda na kitu kinaitwa conservation with sustainable development, maana yake ni nini kwamba kwa kuyapa hadhi hii mapori haya moja itaimarisha ulinzi, lakini pili itajenga mazingira bora ya kuendeleza utalii. Sasa ili hayo yaweze kufanyika na kufanikiwa kuna kitu sisi katika nchi yetu tunasema ni ya pili kwa vivutio vya utalii baada ya Brazil, maana yake tukizungumza katika ile tunaita comparative advantage sisi tuko vizuri katika dunia baada ya Brazil, lakini tukizungumzia competitive advantage bado kuna mambo ya kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi nijielekezee katika kutoa ushauri sasa kwa Serikali pamoja na kupongeza jitihada hizi basi kuongeza nguvu ili tuweze kuwa competitive katika suala zima la utalii kusudi kuongeza mapato kutoka asilimia 17 iliyoko sasa hivi na kuendelea.

Sasa ili tuwe competitive maana yake ni nini, lazima tuboreshe mazingira ya kuwekeza katika shughuli za utalii, lakini pili kuiongezea ngu TANAPA na TTB katika kujitangaza. Lakini la tatu pia kupunguza vikwazo ambavyo kwa namna moja au nyingine vimekuwa kizuizi katika kuhakikisha kwamba sekta hii ya utalii pamoja na kuongeza hadhi hizo hatufikii malengo ambayo yanaweza kutufanya tukawa competitive katika masuala mazima ya utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine na la muhimu ambalo Mheshimiwa Masele alilisema pale ni kujengea uwezo vyuo vyetu vya mafunzo ya utalii ikiwa ni pamoja na kuviongezea nguvu katika mafunzo ya lugha, kwa sababu tunatarajia watalii waje kutoka maeneo mbalimbali pamoja na lugha yetu ya Kiswahili pamoja na lugha ya Kiingereza, lakini vyuo hivi vipewe msisitizo wa kuongeza mafunzo ya lugha nyingine za ziada ili watalii wanapokuja basi kunakuwa na mawasiliano ambayo ni mepesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho napenda kuipongeza Serikali na hasa Mheshimiwa Kigwangalla na timu yake na Naibu wake na watendaji wake kwa kweli kama ambavyo niliwahi kusema wakati fulani mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, wanafanya kazi nzuri, katika utendaji wao kazi nzuri basi wasisite pia kutazama na kutupia jicho katika suala zima la historical sites. Nimewahi kutoa mfano pale Kihesa Mgagao ambayo ilikuwa ni kambi ya wapigania uhuru….

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. COSATO D. CHUMI: ...tungeitazama na tungeweza kuongeza mapato zaidi. Naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)