Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi na mimi nichangie katika maazimio haya mawili. Mimi naomba nijielekeze kwenye azimio hili la kupandisha hadhi mapori haya mawili ya Ugalla na Kigosi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze tu Serikali yetu kwa nia njema ya kukuza hii circuit ya Magharibi sasa kwa sekta ya utalii. Hili ni jambo jema sana kuona kwamba utalii katika nchi yetu unakuwa haubaki upande mmoja wa Kaskazini au Kusini lakini pia upande wa Magharibi wa nchi yetu unaangaliwa maana yake katika kukuza uchumi wa nchi yetu hili likipitishwa na Bunge letu tunakwenda kugusa uchumi wa wananchi wetu, lakini pia tunaongeza pato la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hili kwa sababu utalii katika nchi yetu unatuletea forex zaidi ya asilimia 25 mpaka 30 forex inatokana na sekta ya utalii. kwa hiyo, tunapopandisha hadhi mapori haya mawili maana yake tunaongeza kiasi na circulation ya forex katika nchi yetu kwa sababu haya mapori sasa yanakuwa managed na TANAPA. Kwa hiyo, ni jambo jema sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili; katika Taifa letu, utalii inachangia Pato la Taifa zaidi ya asilimia 17.2 na mantiki yake ni nini? TANAPA wanapokuwa wana-manage sasa haya mapori ambayo yameongezwa kwa upande wa Magharibi inasaidia kukuza na kuongeza mchango katika Pato la Taifa kutoka ile 17 tunaweza tukafika 20 au 25. Kwa hiyo, ni jambo jema sana Bunge hili kupitisha mapori haya yawe chini ya TANAPA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu; utalii katika nchi yetu unachangia ajira kwa zaidi ya milioni mbili. Maana yake tutapata vijana wengi wa Magharibi na maeneo mengine ambao wataajiriwa katika sekta hii baada ya mapori haya mawili sasa kuwa chini ya TANAPA na kuwa managed. Kwa hiyo, ni jambo jema katika kuongeza pia ajira hili linaweza likawa linatusaidia sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo ninafikiri ni la muhimu sana ni suala zima la kuboresha zile changamoto ambazo TANAPA wanapitia. Nafahamu mtu ambaye ana- manage kazi vizuri anaongezewa ndio maana TANAPA wameongezewa haya mapori mawili lakini nishauri sasa Serikali pia waangalie na zile tozo ambazo TANAPA wanakuwa wanazipitia kwa sababu tumewaongezea sasa hifadhi zinafika zaidi ya 20 sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni vizuri zile tozo pia Mheshimiwa Waziri ukaziangalia zile ambazo TANAPA wanapokuwa wanatoa dividend kwa Serikali asilimia 15 wanakuwa-charged pia kodi ya asilimia 30 tena katika kile ambacho wanakichangia. Lakini wanapokuwa wanachangia miradi ya maendeleo ni vizuri pia Serikali iangalie na zile tozo zingine ambazo wamekuwa sasa wakizipitia kama changamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, otherwise naunga mkono hoja, ni jambo jema sana na naamini kwamba hili litasaidia kukuza utalii katika Ukanda wa Magharibi na mwisho wa siku tuta-share keki ya Taifa kwa pamoja na vijana wetu pia watapata ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho; nikupongeze sana Mheshimiwa Waziri na Serikali wakati mmetuletea kwenye Kamati mlieleza kwamba wananchi wale hawataguswa na mipaka ile mlikuwa makini sana. Mimi niwapongeze sana, hili Serikali kuona kwamba wananchi wale wanakuwa hawaguswi, hawasumbuliwi na mkachora ramani kwa upya sasa ili wananchi wasisumbuliwe na naamini kwamba hili litafanyika kwa nia njema na wananchi wetu watafaidika, ahsante sana. (Makofi)