Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

Hon. Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti,asante. Na mimi naomba nichangie kidogo juu ya mkataba huu ambao unataka kuhakikisha matumizi ya zebaki yanakuwa ya salama. Ulianza kutumika mwaka 2017 na sisi mwaka 2019 tunaridhia, kwa kweli tumewahi, Serikali naishukuru sana kwa kuamua kufanya hili jambo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkataba huu kama alivyoeleza Waziri una mambo kadhaa unaoelekeza. Mambo hayo ni pamoja na kuhakikisha kwamba zebaki haichimbwi tena, migodi yote ya zebaki ifungwe na mingine ambayo ipo inaendelea ihakikishe kwamba haizalishi tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini matumizi ya zebaki au bidhaa zinazotumia zebaki na zenyewe zisitumike lakini zaidi sana ni matumizi ya zebaki katika kuzalisha dhahabu. Mkataba unaelekeza kuwe na matumizi yaliyoangaliwa, sio matumizi holela, mkataba hausemi kwamba tusichimbe dhahabu kwa uchimbaji mdogo, tusiunganishe dhahabu bila kutumia zebaki, lakini tuhakikishe matumizi haya hayafanyi mazingira yakaharibika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda niseme kwamba nilivyokuwa msimamizi wa sekta hiyo ya uchimbaji mdogo, wachimbaji wadogo wengi sana wameathirika na hata watu/watoto wanaozaliwa kwenye maeneo hayo wana hali mbaya sana; wanazaliwa wengine hawana macho na wengine vichwa vikubwa. Kwa hiyo, ni jambo la msingi sana Serikali tutakapomaliza kupitisha huu mkataba, tutengeneze sheria na kanuni ambazo zitahakikisha matumizi ya zebaki kwenye maeneo ya uchenjuaji wa madini yanakuwa ya salama, tusiruhusu kama ilivyo sasa watu wanachenjua tu kwa kutumia zebaki bila control. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho; naomba niombe basi Serikali tu-domesticate huu mkataba kwa kutengeneza sheria, tusibakize zile sheria za zamani hazitoshi, tutunge sheria itakayoelekeza jambo hilo itatusaidia sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja kwa asilimia 100, ahsante sana. (Makofi)