Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia, nianze tu na hoja iliyomalizika. Mimi ni mwanamazingira kwa kweli kama wenzetu hawa hoja za toka jana na leo wataendelea kuwa hivyo wa upande wa kushoto wanafanya kazi nzuri sana. Mheshimiwa ametoa mwelekeo mzuri sana wa mambo ya mazingira na kweli mimi nakupongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kusema ukweli hili tatizo lipo isipokuwa kwamba sumu ya zebaki ipo kila mahali, hata chakula chochote unachokula kuna kasumu ndani yake.Tatizo la binadamu ni kiasi gani cha sumu kinachoweza kuathiri, lakini sumu kama sumu zipo tu kila siku zipo kila mahali, nikupongeze kwa kweli umefanya vizuri na mimi nadhani sina mjadala kwenye hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapokuja kwenye hoja ya pili, tunapokuwa tunapandisha haya Mapori ya Ugalla na Kigosi. Mapori haya tunachotaka kufanya ni kutengeneza circuit. Nataka nikukumbushe circuit maana yake nini, ukisema uende kutembelea Mikoa ya Kanda ya Ziwa maana yake unaenda kwenye Mikoa ya Mara, Kagera, Geita, Mwanza na Shinyanga, hapo umetengeneza circuit ya kutemebelea maeneo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye tourism industry kuna kitu tunaita circuit, kwa hiyo tukienda kwa mfano mgeni anataka kuja Kilimanjaro anatakiwa atoke Kilimanjaro aende KIA, akitoka KIA aende Lake Manyara, akitoka Lake Manyara aende Ngorongoro, akitoka Ngorongoro aende Serengeti; hapo umetengeneza circuit ya Serengeti na mafungu yake yanaweza kuwa yanaongezeka kutokana na hiyo circuit.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapokuwa tunapandisha Mapori ya Kigosi na Ugalla tuna maana kwamba kuna Burigi, Kigosi, Ugalla na Katavi, lakini katikati yake kuna Mapori ya Akiba Muyowosi, Ugalla na Kigosi. Kwa hiyo, tunatengeneza circuit ya Kusini ambayo mtu akitembea; mtu/mgeni ukimwambia atoke Dar es Salaam aende Katavi, atembee Mbuga ya Katavi arudi Dar es Salaam hawezi kwenda anaona kama hajatengeneza kitu. Kwa hiyo, tunataka atembee Katavi aende Ugalla, aende Kigosi na aende Burigi, kwa hiyo tunakuwa tumetengeneza hiyo circuit ya upande wa Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, hali iko sawa na maendeleo yanakuja kwa njia hiyo. (Makofi)