Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya eneo la Pori la Akiba la Selous kuwa Hifadhi ya Taifa ya Nyerere

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya eneo la Pori la Akiba la Selous kuwa Hifadhi ya Taifa ya Nyerere

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nami naomba nitoe maoni yangu machache kuhusiana na upandishaji wa hadhi wa pori hili kuwa National Park.

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kupandisha hadhi pori hili kwa sababu tukiangalia wenzetu wa Kaskazini kule Mji kama wa Arusha umeendelea sana kutokana na utalii, namii kwa mfano Jimbo langu la Ulanga sehemu kubwa sana ni Selous Game Reserve sasa kwa kupandisha hadhi kuwa National Park kuna vitu vingi sana tutapata fursa vikaweza kuonekana. Kwa mfano tu nilienda maeneo ya Monduli nikakuta watalii wanaangalia ngoma za Maasai ambao wanaruka ruka, lakini kwetu Ulanga tuna ngoma inaitwa Sangula ni ngoma nzuri sana, nadhani itajulikana hata Kimataifa pia kuna milima mizuri na mambo mengine.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba niongelee suala la Stigler’s. Mheshimiwa Rais wakati anatoa kauli wakati wa anazindua ujenzi wa bwawa hili alisema kuwa watu watakuwa wanaruhusiwa kwenda kufanya uvuvi lakini tunafahamu sheria za TANAPA na Sheria za Uhifadhi haziruhusu watu kwenda kwenye maeneo haya, kwa hiyo naomba hili liwekwe clear.

Mheshimiwa Spika, pia tunapokuja kutoa matamko hayo pia tuangalie na Sheria hizi za Uhifadhi na Sheria za TANAPA kwa sababu Sheria ya Uhifadhi wa Misitu ya Wanyamapori inasema kuwa, ng’ombe wakikamatwa au mifugo ikikamatwa inataifishwa lakini ile Sheria ya TANAPA ni ya kupiga faini, hivyo tunataka sheria moja uniform ambayo itakuwa haiathiri mifugo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala langu zito nililokuwa nataka niongelee ni kuhusu wafanyakazi, naona Wizara wanalikwepa na Kamati wanalikwepa. Wote tunafahamu Game Reserve zinakuwa chini ya TAWA, mfanyakazi wa TAWA kima cha chini cha mshahara hakizidi shilingi laki nne. Leo hii inapandishwa hadhi inaenda kuwa chini ya TANAPA na TANAPA mshahara kima cha chini siyo chini ya shilingi milioni moja, leo hii inapoenda kupandishwa hadhi TANAPA hawataki kuwarithi hawa wafanyakazi ambao wamefanyakazi kwa muda mrefu sana.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo naomba Waziri wakati ana-wind up atuambie hawa wafanyakazi wa TAWA na wenyewe waende wawe chini ya TANAPA irithi pori pamoja na wafanyakazi kwa sababu wamefanyakazi muda mrefu, vyuo wanavyosoma ni vilevile, fani ni ile ile, mapori ni yale yale wanyama ni wale wale, kwa nini TANAPA ing’ang’anie kwenda kuajiri wafanyakazi wengine wakati wafanyakazi wapo ambao wana uzoefu na taaluma zile zile. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri naomba atoe kauli kuhusiana na hilo.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la mwisho ni suala la vitendeakazi. TAWA wana miliki wanyama wote ambao wako ndani ya mbuga na nje ya mbuga lakini vifaa hawapewi, TANAPA wanamiliki wanyama wachache ambao wako kwenye National Park tu lakini wanapewa kila kitu resources zote wanazo, tunaona kwa mfano tembo walioonekana Dodoma TAWA ndiyo wanahusika, tembo wanaoingia maeneo ya makazi yote ni TAWA lakini hawana vifaa kama alivyosema Mheshimiwa Suzan unakuta Kanda nzima wanapewa gari moja ama mawili. Kwa mfano wa Ulanga kule sasa hivi tembo wanasumbua mitaani lakini hawana vifaa. Kwa hiyo naomba TAWA waongezewe vitendeakazi.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana naunga mkono hoja lakini naomba suala la wafanyakazi litolewe kauli. (Makofi)