Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia fursa hii muhimu ya kuchangia taarifa mbili tulizonazo mbele yetu; taarifa ambazo ni muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa letu.

Katika Taarifa ya Kamati ya Huduma za Jamii katika ukurasa wa 44, Kamati imeshauri vizuri, kwamba kuna haja ya kuweka mikakati ya maksudi ya kuhakikisha tunakabili changamoto ya upungufu wa watumishi katika sekta ya afya na sekta ya elimu. Ushauri wa Kamati ni mzuri na mapendeklezo ya Kamati ni mazuri. Hii inadhihirisha maeneo mbalimbali kila mtu kwenye eneo lake atakubaliana nami kwamba Kamati inaposema kuna changamoto ya Wataalam katika sekta ya afya na elimu ni kweli, kwa mfano; kwangu kule Wilaya ya Misenyi tuna upungufu wa Walimu katika shule za msingi, upungufu wa Walimu 750; hiyo ni Wilaya moja; na ukienda kila Wilaya tatizo linafanana.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia lazima niipongeze Serikali; kwasababu tulikuwa na tatizo pia la upungufu wa walimu upande wa walimu wa sekondari, Tanzania nzima tulikuwa na upungufu mkubwa.Ambacho kimetokea kwa sasa ni kwamba tuna upungufu wa walimu tu wa masomo ya sayansi na hisabati, lakini sasa tuna walimu wa kutosha kwa masomo ya sanaa, wapo wengi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwahiyo ndiyo maana nachukua nafasi hii kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri waliyofanya kuondoa tatizo la upungufu wa Walimuy wa sanaa. Naungana na Kamati kama ilivyoshauri kwamba mikakati itafutwe ya kukabiliana na tatizo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, niikumbushe Serikali na niiombe Serikali kwamba kwa kuwa mmeweza kuondoa tatizo la upungufu w Walimu wa sanaa, mbinu mlizotumia hizo hizo mzihamishie kwenye kuondoa upungufu wa walimu wa sayansi na hisabati; nadhani tukifanmya hivyo tutaweza kupiga hatua kwa kasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nimekuwa nikijiuliza, unakuta maeneo mengi hawa tunaowaita walimu wa sanaa, ukitembelea shule zetu hizi ukaenda ukazungumza utakuta wale walimu wa sanaa wengine watakwambia hapa hatuna mwalimu wa hisabati, hatuna mwalimu wa sayansi; sasa unauliza, kwamba wanafunzi hawafundishwi? Wanasema a‟ a! hawa walimu wengine hawa wa sanaa tunawaomba wanasaidia saidia kufundisha. kuna shule moja ambayo niliambiwa walimu wa sanaa wanaombwa, wanasidia kufundisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna vijana walikuwa wana A za hesabu, A za fizikia na A za masomo mengine ya sayansi. Maana yake ni kwamba walimu hawa ambao tunaowaita ni walimu wa sanaa kama wakiweza kuongezewa utaalam kidogo wanaweza pia wakawa walimu wazuri wa masomo ya sayansi. Kwahiyo, naungana na Kamati kama ilivyoshauri kwamba Serikali ifikirie nini kifanyike basi kimojawapo cha kufikiria ni jinsi gani wanaweza wakaandaa mafunzo maalum kwa hao walimu waliopo ili waweze kuwa walimu wa masomo ya hisabati na sayansi wakati tunaendelea kutafuta ufumbuzi wa kudumu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa nizungumzie pia suala la wagonjwa wa msamaha. Ni kweli kama ilivyoeleza Taarifa ya Kamati, ni kwamba unakuta akina mama wajawazito, wazee wasiojiweza na watoto wa chini ya miaka mitano wanakuwa ni wengi sana wanpokwenda hospitali; na kwa kuwa sera yetu iko wazi hospitali zinawajibika kuwahudumia hawa. Zikiwahudumia unakuta ndani ya muda mfupi fedha yote iliyotengwa imekwisha. Sasa nilikuwa nafikiria, kwamba kwa kuwa tunayo hoja ya kuanzisha ile bima ya afya kwa wote, basi hiyo sheria itakapoletwa pia izingatie umuhimu wa kutoa bima maalum kwa haya makundi ambayo tulishasema kwamba yapate huduma. Mimi nadhani tukifanya hivyo tutaweza kupata ufumbuzi wa kutusaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia katika ukurasa wa 53 Kamati imeshauri kwamba ni vizuri Serikali iwekeze na kuboresha vyuo vya ufundi nchini ili viweze kuzalisha mafundi wa kutosha watakjaosaidia katika kuendesha viwanda. Nakubaliana na Kamati kwa mapendekezo hayo, ni mazuri; na nipnde kuchukua nafasi hii kuishukuru Wizara ya Elimu kwa jinsi ambavyo imewekeza vya kutosha. Kule kwangu kwa kweli sina cha kulalamika, wamewekeza zaidi ya milioni 700 kwa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi-Gera.

Mheshimiwa Naibu Spika, juzi nilikuwa napita pale rafiki yangu mmoja akasema hicho ni Chuo Kikuu kipya, nikasema hiki si Chuo Kikuu, hiki ni Chuo cha Maendeleo ya Wannachi; na nashukuru sana na serikali imefanya hivyo maeneo mengi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tatizo tulilonalo maeneo mengi vyuo hivi havitumiwi vizuri. Ukivitembelea vyuo hivi maeneo mengi unakuta hatuvitumii vizuri. Kwahiyo nitoe wito kwa wenzangu Waheshimiwa Wabunge tuliopo hapa kwamba vyuo hivi tuvitumie vizuri, kwasababu tukivitumia vizuri vitatusaidia kutoa mafunzo ya kuweza kupambana na ukosefu wa ajira, kuwawezesha vijana kuweza kujiajiri pamoja na kuwaandaa na vijana ambao wanaweza wakatusaidia katika kuendesha hii Tanzania ya viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna eneo moja ambalo ningependa kulizungumzia kidogo, ni upande wa mikopo ya elimu inayotolewa kwa ajili ya vijana wetu; tunatoa mikopo kwa vijana wanaosoma shahada mbalimbali, lakini kuna kada ambazo tumezisahau. Kwa mfano mimi najiuliza, tuna Chuo chetu cha IJA (Institute of Judicial Administration) kule Lushoto; vijana wanaosoma pale wanasoma mafunzo muhimu sana ya sheria kwa Diploma, Certificate na hawa tunawahitaji sana ili watusaidie lakini wao hawapewi mikopo.

Sasa mimi najiuliza, hivi, hawa tunawahitaji na tunafikiri kwamba watatusaidia katika kutoa haki ndani ya nchi lakini kwanini inapokuja kwenye mikopo tunasema hao wasipewe? Na kwamba wapewe wa Degree peke yake? Mimi nadhani wakati umefika wa kuangalia ni kwa jinsi gani tunaweza tukapanua wigo ili vijna wengi zaidi waweze kupata mikopo ya kuwasaidia kupata elimu kila mtu kadri ya hatua ambayo anasoma. Kwa sababu kusoma Certificate au Diploma siyo dhambi wkamba usimpe mkopo kwasababu anasoma Kada ndogo.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mheshimiwa Naibu Spika, muda umekwisha au bado kidogo?

NAIBU SPIKA: Umekwisha Mheshimiwa, umeshamaliza dakika zako ahsante sana.

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naunga mkono hoja.