Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii

Hon. Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii ya awali ya kuweza kuchangia katika ripoti za kamati hizi mbili ambazo kwa bahati nzuri sana mimi ni Mjumbe wa kamati zote mbili. Niwapongeze sana Wenyeviti waliosoma, pia nipongeze na kukubaliana kabisa na maoni ya Kamati hizo kwa sababu hiyo ndio hali halisi. Nitaanza na Wizara ya Afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo kubwa ambalo linajitokeza katika Wizara hii ya Afya ni tatizo kubwa sana la watumishi. Tatizo la watumishi katika Wizara ya Afya ni almost 50 percent. Ukiangalia lile lengo namba tatu la kuhakikisha kwamba tunakuwa na taifa lenye afya na watu wenye siha njema si rahisi kabisa kufikiwa kwa jinsi ambavyo tunaenda na trend ya bajeti. Pamoja na kwamba Mwenyekiti wangu amesema bajeti ya Wizara ya Afya imekuwa ikiongezeka, ni kweli inaongezeka kwa fedha lakini ukiangalia kwa percentage inapungua sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe tu takwimu mwaka 2014/2015 tulikuwa na asilimia 9, na that was the highest. Mwaka jana ilikuwa asilimi 5.5 ilhali sisi kama nchi tumesaini Abuja Declaration ambayo inapaswa Wizara ya Afya walau Sekta ya Afya itengewe asilimia 15, lakini jambo hilo hatujaweza kulifikia. Kwa maana hiyo, pamoja na juhudi zote za Waziri, Naibu na watendaji wote unakuta kwamba tatizo kubwa linakuwa ni bajeti. Kwa hiyo, ni ombi langu kwamba ni muhimu sana bajeti ya afya ikaongezeka kwa percentage na sio kwa figures.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo nilitaka kuzungumzia kwenye Wizara ya Afya na hili ni jambo kubwa sana, ni suala la bima ya afya. Waheshimiwa Wabunge mjue kwamba bima yetu ya afya inaisha Juni, kwa hiyo mjue kuanzia Julai mpaka Novemba hapo mtajijua wenyewe. Kwa hiyo, ni muhimu sana wakati tunajua sisi tuna bima, tuwaangalie wenzetu huko nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, kamati imesema kwamba magonjwa yasiyoambukiza yameongezeka kwa kiasi kikubwa na magonjwa haya ni ya gharama kubwa sana. Jambo ambalo linasikitisha leo, wagonjwa wa figo ni wengi sana lakini dialysis ni very expensive. Ukiingia kwenye dialysis kipimo siku moja tu kusafishwa figo ni shilingi kuanzia 250,000 mpaka 350,000 lakini unatakiwa process hii ndani ya wiki moja mara tatu, kwa hiyo Mtanzania gani ataweza kujilipia kuanzia 750,000 mpaka 1,000,000 na? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kinachosikitisha naambiwa kuna ambao tayari walikuwa kwenye hiyo package, leo wameenda ku-renew bima zao wanaambiwa dialysis imeondolewa kwenye hiyo package. Kwa hiyo, kuna kilio kikubwa sana kwa wananchi ambao wana matatizo makubwa sana ya figo, lakini matatizo ya moyo na mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niombe sana Serikali iangalie ni jinsi gani tumepiga kelele walete muswada ili kuhakikisha kwamba wananchi wote wanakuwa covered kwenye bima ya afya ili sasa gharama zipungue kwa wale ambao wanapata magonjwa haya makubwa, lakini jambo hilo bado hakijaweza kutekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la lishe; ni jambo la kusikitisha kuona kwamba kama nchi bado tuna watoto wenye udumavu wengi sana, takribani asilimia 32. Kinachosikitisha fedha iliyotolewa kwa ajili ya masuala haya ya lishe ilikuwa bilioni 289 lakini zilizopelekwa ni bilioni 123 sawa na asilimia 43 pekee. Kinachosikitisha zaidi, katika fedha hii asilimia 95 inatoka kwa wafadhili, yaani Tanzania kama nchi ni asilimia sita tu. Hivi kweli tunawategemea wafadhili hata kwenye lishe? Hili ni jambo ambalo halikubaliki. Kwa hiyo, haya ni mambo ambayo kama nchi
lazima tuone kwamba tunajikomboa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikija kwenye suala la elimu; imezungumzwa vyema kwamba msingi wa elimu ni elimu ya awali (nursery) lakini kwa takwimu zinatisha; kwamba tuna upungufu mkubwa sana wa walimu wa nursery, tunao walimu 9000 kati ya watoto takribani 1,000,000. Kwa hiyo, unakuta uwiano ambao unatakiwa katika nursery iwe mwalimu 1 kwa watoto 25 sasa hivi wastani ni mwalimu 1 kwa watoto 146 lakini inatisha zaidi kwa Jimbo la Serengeti peke yake wastani mwalimu 1 wanafunzi 3,300. Hizi ni data tulizozipata kutoka MCM. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kama mtoto ametoka nyumbani anaenda kuanza shule, wakati huo ubongo wake hauna chochote zaidi ya kile anachokiona hivi kweli mtoto anaenda kwenye darasa la watoto 200/300, atakuwa na mapenzi au na passion na shule? hawezi kuwa na hiyo passion. Kwa hiyo, ni muhimu sana tunahitaji takribani walimu 43,000 wa shule za awali ili tuweze kuhakikisha kwamba tatizo hilo linaondoka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba sana Mheshimiwa Waziri uone umuhimu wa kupata walimu katika shule za awali lakini vilevile katika shule za msingi. Leo tunavyoelekea kwenye shule za msingi tunajua elimu bure imekuja na mambo yake mengi na changamoto nyingi. Je, Serikali mmejipanga vipi kuhakikisha kwamba watoto wanaoenda kumaliza darasa la saba mwaka 2022 ambao watakuwa doubled; sasa hivi wanamaliza takribani 900,000 – 1,000,000 wataenda mpaka 1,500,000; je, mmejipagaje watoto hawa sekondari? Kwa sababu kila siku ikifika mwezi wa kwanza ndipo tunaanza kusema/Waziri Mkuu na Wakuu wa Mikoa wanatoa matamko ya kujenga shule. Hivi hamna utaratibu wa kutenga tengeo kwa sababu kama tunahitaji leo bilioni 700 na kwa ajili ya kujenga madarasa, kwa nini msiyaweke kwa awamu kila mwaka mkatenga walau nusu au robo kwa miaka mitano ili mhakikishe kwamba tatizo hili linapungua au kuisha kabisa? Hawana mpango. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mimi niseme tu kwamba kuna kila sababu ya kuwa na mpango mahsusi wa kuhakikisha kwamba mnatenga kila baada ya muda fulani kwa ajili ya kuhakikisha kwamba watoto wanafaulu wanaenda kusubiri madarasa bali madarasa yawasubiri wanafunzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile bajeti ya Wizara ya Elimu Sekta ya Elimu nayo inapungua, hela inaongezeka lakini ukiangalia asilimia inazidi kupungua. Tulianza na trilioni 4.7 mwaka 2016/2017 leo tupo trilioni 4.5; kwa maana ya kwamba bilioni 255 zimeshapungua. Je, tunapunguza fedha wakati tumekuwa na changamoto kubwa lakini wanafunzi wameendelea kuongezeka, walimu hakuna.

Mheshimiwa Naibu Spika, natoa ushauri kwamba walau kwenye total budget ya Wizara ya Afya na Elimu 0.05 mtoe kwa ajili ya kuajiri watumishi wa afya na watumishi wa Wizara ya Elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye UKIMWI; suala la UKIMWI ni suala mtambuka na kwa maana hiyo suala la Mfuko wa UKIMWI ninaomba sana, mfuko huu about 90 percent unategemea nje, lakini wagonjwa ni wetu na wagonjwa wakishaanza dawa hizi hawawezi kuziacha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni muhimu sana Mheshimiwa Jenista muhakikishe kwamba Mfuko wa UKIMWI sasa tunakua tunautegemeza wenyewe na hatutegemei watu wa nje kwa kiasi kikubwa, 90 percent leo wakikata maana yake wagonjwa wote waliopo kwenye dawa watakuwa hatarini kupoteza maisha yao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye suala la UKIMWI kuna suala la VAT exemption. Kama Kamati tumekutana na wadau, hawa ambao ni development partners na hasa wale wanaotoka Mfuko wa Rais wa Marekani ambao kwa kiasi kikubwa umekuwa ukisaidia sana masuala ya UKIMWI.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kumekuwa na mkinzano mkubwa sana wa kisheria kwa maana ya kwamba ile VAT exemption inasema kwamba NGO hazipata huo msamaha. Kikubwa ni kwamba tunaomba basi kuwe na utaratibu madhubuti ambao utawezesha hawa watu wapate VAT ili waweze kusaidia wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, asante. (Makofi)