Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. SALUM MWINYI REHANI - MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru kwa kuweza kunipatia muda tena wa kuja kuhitimisha hoja yetu tuliyoanza nayo asubuhi, lakini kwa makofi mengi yaliyopigwa hayo yanaanshiria kwamba sasa hivi niko ki-diplomatic zaidi. (Vicheko)

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge mbalimbali wamepata fursa ya kuchangia kwenye Wizara zetu hizi tatu, na mimi niseme wazi kwa dhati kabisa nimechukua maoni yote na mawazo waliyokuwa wametushauri. Yako ambayo yametolewa ufafanuzi na baadhi ya Waheshimiwa Mawaziri na yako ambayo sisi kama Kamati tutakwenda kuyafanyiakazi. Hata hivyo na mimi nilitaka niyaweke sawa tu baadhi ya mambo ambayo yamejitokeza na kuahisi kwamba haya tutakwenda kuyafanyiakazi.

Mheshimiwa Spika, lilikuja suala zima la Sera na Sheria ya Ulinzi binafasi; hili lazima tukubali ukweli katika eneo hili watu wengi wameajiriwa na hatuwezi kutaacha kundi la watu zaidi ya 250,000 wasiwe na sera na sheria inayoweza kuwaongoza. Makampuni mengi kama tulivyokwishasema ni ya kurithiwa tu. Wazee wao walianzisha wao wakarithi watoto na hakuna sheria inayoweza kuwasimamia. Kwa hiyo hilo bado tutarudi kuweza kuhakikisha kwamba Wizara inaitekeleza na kuiwasilisha hapa Bungeni ili kuweza kupata sheria itakayoweza kuwalinda na kuweza kuwa na Mashirika au Kampuni ambazo zinajiendesha kwa sheria iliyo thabiti.

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo limezungumzwa ni suala la NIDA; bado kwetu kama Kamati tumeliona kama ni donda ndugu. Watanzania wengi hawajapata fursa ya kupata Vitambulisho vya Taifa na bado wengine wako waliokuwa hawajaandikishwa. Sisi kama Kamati tumeshalizungumza lakini tunasema wazi kwamba bado tunakwenda kulikalia na kuhskikisha kwamba mitambo iliyokuwa imewekwa kuweza kutoa vile vitambulisho kwasababu tulikuwa na ahadi ya vitambulisho milioni 20 Disemba mwaka jana, ahado ambayo kwa mitambo iliyokuwepo haikuweza kufikiwa; kwahiyo tunakwenda kusimama na mitambo mipya kuhakikisha kwamba ahadi hiyo Watanzania wanapata vitambulisho vyao mapema na kila mmoja atakuwa anatambulika kihalali.

Mheshimiwa Spika, lingine dogo lilidokezwa na Mheshimiwa Masele; suala la uwekezaji kwenye sekta ya ulinzi; nalo hili tumelichukua na bado tutaendelea kuisgauri Serikali iweze kuwekeza kwenye suala zima la ulinzi wa nchi.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Bobali aliligusia suala la mipaka; ni kweli kabisa Tanzania ina mipaka mirefu sana na hasa upande huu wa. Mimi nilipata fursa ya kuwa mwangalizi katika uchaguzi ule wa Msumbiji, maeneo yale ya Tunduru ukiangalia mipaka zaidi ya kilometa 70 na ina Panya road zaidi ya 300 na zaidi. Kwahiyo, hili nalo ni suala ambalo linatakiwa tujipange zaidi kuhakikisha kwamba haipitishi wahalifu katika maeneo yale.

Mheshimiwa Spika, kubwa zaidi linalojitokeza hapa, wenzetu, hasa wa ule upande wa Kusini wa Msumbiji wamekuwa wakijiegesha au wanasema kwamba wanatoa fursa ya kuolewa kwa wingi Tanzania ili kuweza kupata uraia wa Tanzania na hivyo kutumia fursa hiyo ya ile mipaka kuweza kujipenyeza na kuishi huku isivyohalali lakini baadaye wanakuwa halali kwasababu wengi wao wanaomba kuwa raia wa nchi hii.

Mheshimiwa Spika, suala la Magereza tumelichukua.

Mheshimiwa Spika, lingine lililozungumzwa hapa ni suala la Diplomasia. Mimi niseme wazi kwamba tunakwenda vizuri kwasbabu Waziri wa Mambo ya Nje ya Nchi, Mheshimiwa Profesa Palamagamba Kabudi kwa kweli tuseme wazi kwamba tumepata hazina nzuri, ni nguzo ya Nchi yetu, ana uwezo mzuri wa kuisemea Tanzania ndani na nje ya nchi. Katika eneo hili haogopi kitu na amekuwa akisimama kizalendo kuhakikisha kwamba thmanai na hadhi ya Tanzania inaweza kutambulika na kuweza kupewa hadhi inayostahili ndani ya sura ya Dunia. Nimpongeze sana na nishukuru kwa uzalendo na nguvu ambayo anaitumia kuhakikisha kwamba nchi hii haiweze kuonewa wala haiweze kudhulumiwa kwa njia nyingine yoyote ile. Sisi kama Kamati tuseme wazi kwamba tutashirikiana naye kwa karibu zaidi kuona kwamba tunaweza kufanikiwa kwa kila ambalo tumekuwa tukilipanga.

Mheshimiwa Spika, lakini hata lile ambalo tunasema kwamba halikuguswa, la maradhi ya Corona kule China tuseme wazi kwamba sisi kupitia Wizara hii tumezungumza kwenye Kamati na Mabalozi wetu wanafnya uratibu wa watu wetu ambao wako katika nchi mbalimbali duniani kuhakikisha wkamba Watanzania hawawezi kuathirika. Lolote litakalotokea nchi yetu itatoa taarifa kupitia viongozi hawa wa Mabalozi pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje kuijulisha hali ilivyo kwa maradhi haya lakini na maradhi mengine.

Mheshimiwa Spika, lakini vilevile nimdokeze Dada yangu Salome, kwamba nchi haijajitoa kwenye suala zima la ICC, bado maelezo yaliyokuwepo ya kwamba nchi imejotoa si kweli na tunajua msimamo wa Tanzania ulivyo katika eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo tumeweza kulishughulikia kama Kamati ni suala zima la kuhskikisha kwamba diplomasia ya uchumi kwa Mabalozi wetu inafanyakazi; na ndiyo maana kipindi hiki cha karibuni wameletwa Mabalozi hapa nchini kuja kuona vivutio na fursa zilizopo ndani ya nchi na kujua kwamba wakienda kule wanakokwenda waweze kuitangaza Tanzania kwenye diplomasia ya uchumi. Wameona miradi mikubwa ya umeme, reli ya mwendokasi, Bandari pampja na utayari wa Watanzania tulivyoweza kujipanga kwenye suala zima la utalii. Moja ya task ambayo wamepewa ni kuhakikisha kila Balozi analeta watalii ndani ya nchi hii na kuongeza Pato la Taifa lakini kuongeza watalii ambao wanaitembelea nchi yetu hii ya Tanzania.

Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache ambayo tumeweza kuyaangalia na kuyatolea ufafanuzi niseme wazi kwamba yale ambayo yaliyokuwa hayakuguswa au wale Wabunge ambao hawakuguswa mawazo yao yote tumeyachukua sisi kama Kamati tutayafanyia kazi na tutayaleta majibu yake kwa maandishi kwa wahusika ambao wanayahitaji hayo majibu.

Mheshimiwa Spika, zaidi ya hapo mimi nikushukuru na niombe tena kutoa hoja ili niweze kukamilisha hoja yangu hii ya report hii ya nusu Mwaka 2019/2020 kwa awamu hii ya pili.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Spika, naafiki.