Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nianze kwanza kabisa kukushukuru kwa kusimamia vizuri mjadala huu na pia kwa shughuli zote ambazo unafanya kwa Bunge hili na kwa nchi hii tutakukumbuka sana na historia yako itabakia. Ni katika kipindi chako mambo makubwa na mengi yanafanyika katika nchi ambayo nchi hii inaweka msingi mzuri wa kwenda mbele zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili namshukuru sana Kamati ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama chini ya Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Salum Rehani, Mbunge wa Uzini kwa kazi kubwa na maoni mengi mazuri ambayo wameyatoa, nasi kama Serikali kusema kweli baadhi yake tunakubaliana nayo na tutayachukua.

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa waliochangia na kugusa Wizara ya Mambo ya Ndani sio wengi sana, lakini kwa hawa wachache wamezungumza mambo ambayo yanagusa maeneo makubwa na kwa sababu ya muda nitajaribu kuongea kwa kifupi sana.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba wakimbizi tulionao hapa nchini ni wengi, hadi jana walifikia kiasi cha tunawakimbizi hapa nchini 293,931. Katika idadi hii, wakimbizi wengi zaidi wanatoka Burundi ambao wako 217,501.

Mheshimiwa Spika, jitihada kubwa zinafanyika kuhakikisha kwamba wakimbizi hawa wanarudishwa makwao. Mwezi Novemba, 2019 mwaka jana yalifanyika makubaliano kati ya UNHCR, Serika ya Tanzania na Burundi juu ya utaratibu mpya. Kwa sababu pamoja na wale waliokubali wenyewe kwa hiari yao kurudi kwao, lakini logistic namna ya kuwarudisha nyumbani imekuwa kidogo zina mchakato mgumu. Kwa hiyo, tumekubaliana kuweka malengo kwamba kila wiki tutarudisha wakimbizi 2,000, ni imani yangu kwamba kama hili likitoka tukalisimamia, basi idadi kubwa ya wakimbizi watakuwa wameondoka nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia jambo la pili ambalo lilizungumzwa hapa ni juu ya vitambulisho vya Taifa jukumu ambalo linafanyika na NIDA. Kazi kubwa imefanyika sana tu, kwa sababu mchakato wa kutoa vitambulisho vyenyewe kuwakabidhi wananchi ni wa mwisho kabisa; lakini kuandaa mpaka kufikia kutoa vitambulisho, ndiyo kazi ngumu zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kazi hii imefanyika, lengo letu ilikuwa ni kutoa vitambulisho milioni 24,200,000. Katika usajili, tumesajili 20,131,014, alama za kibaolojia tumeweza kuchukua 18,157,624, lakini kuingiza kwenye mfumo, tumeingiza 16,240,341. Kwa hiyo, utakuta kwamba karibu tumefanya kwa haya yote yote kwa kiasi kikubwa vizuri, kasoro ile hatua ya mwisho. Kwa upande wa vijijini tumeweza kuhakiki wananchi 15,488,766, pia tumetoa namba za utambulisho 13,872,281, lakini vitambulisho tulivyovitoa ni vichache na sababu kubwa ni mtambo wa kuzalishia vitambulisho hivi.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa jitihada kubwa inafanywa kukamilisha mtambo ambao tayari umenunuliwa, una kasoro kidogo ambazo ni chache, unarekebishwa na tunaufunga pale Kibaha ili tuweze kutoa vitambulisho vingi; na uwezo wa mtambo huo ni kutoa vitambulisho 9,000 kwa siku moja. Kwa hiyo, ninaamini kwamba tutaweza kufikia malengo.

Mheshimiwa Spika, eneo la tatu, zimezunguziwa jitihada za kupunguza mahabusu. Jitihada kubwa zimefanyika lakini hata hivyo, pamoja na kufanyika jitihada hizo za kupanua Magereza hasa na kurekebisha miundombinu ya Magereza ni lazima pia jitihada nyingine hizi tuweze kuziendeleza. Tumeamua kuunda Kamati ya kusukuma kesi, pia DPP anazunguka katika Magereza na kuhoji mahabusu waliokaa muda mrefu ili kesi zao ziweze kusikilizwa kwa haraka. Kwa hiyo, jitihada zote zinaweza zikasaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la mwisho ni hili la uhuru wa kuamudu ambao upo kwa mujibu wa Katiba. Hoja iliyotolewa na Waheshimiwa Wabunge ni kwamba, pamoja na uhuru huu lakini lazima tuangalie namna ya kuudhibiti au kuuwekea utaratibu uhuru huu. Nakubaliana kabisa kwa asilimia 100 kwamba kanuni zetu hazioneshi namna nzuri zaidi ya kuweza kuweka mfumo mzuri wa udhibiti wa uhuru wa kuabudu. Serikali haiingilii kamwe na wala haitaingia kamwe uhuru wa kuabudu, lakini kuweka utaratibu unaohakikisha amani na usalama ya wanaoabudu ni jambo la msingi.

Mheshimiwa Spika, tumejaribu kujifunza kutoka kwenye nchi nyingine, wenzetu kwa mfano Nigeria wenyewe hawana masharti yoyote, lakini tunaona yanayotokea huko. Wenzetu wa Rwanda wameweka utaratibu na wameweka hata elimu ya mtu anayeweza kutoa au kuanzisha ministry au huduma ya namna hiyo, lazima awe na aina fulani ya elimu. Wenzetu Kenya walijaribu wakaenda nalo lakini hawakulimaliza na Uganda vilevile na wenyewe wanaendelea nalo.

Mheshimiwa Spika, nasi nadhani iko haja ya kuchukua maoni haya na kubadilisha hata kama siyo sheria, basi kanuni zilizopo kwa haraka ili tuweze kuwa na mfumo mzuri wa namna ya kuabudu. Sitaki niseme zaidi ya hapo kwa sababu, ni leo hii mchana nimekutana na wahusika wa dhehebu lile la Calvary Assemblies of God ambao Boniphace Mwamposa anafanya kazi katika lile dhehebu na kwamba ile huduma anayoitoa siyo huduma iliyosajiliwa nasi hatuna usajili wa huduma ile, lakini ile ni slogan tu; lakini yeye amesajiliwa na wenye lile dhehebu wamekuja wamekiri kwamba ni mtumishi wao, ni mfanyakazi wao, ni kiongozi ambaye anahudumu Dar es Salaam na Kilimanjaro na amekuwa akifanya hivyo mara zote.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunaendelea na hatua nyingine za jambo lile kama kioo na Mwalimu wa mengine yasitokee huko mbele ya safari.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, naunga mkono hoja ya Kamati. (Makofi)