Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii, kwanza kabisa niwapongeze Kamati zote mbili Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na Kamati ya Nishati na Madini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nishauri tu kwamba nimesikiliza mijadala tangu asubuhi ili mijadala yetu iweze ikawa na afya tuzingatie misingi ya utu wakati tunajadili, misingi ya kuwa na utulivu wa fikra, msingi wa rasilimali muda baadaye rasilimali fedha kwa muda utakaotumia katika mijadala yetu. Na wazo zuri ni wazi zuri usiangalie limetoka upande upi. Tujadili pamoja, tufakari pamoja na hatimaye tushauri pamoja. Hii italeta tija na itatusaidia sana kama Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nasema hivi kwa sababu tukigawanyika na yote mazuri ambayo tunayazungumza ambayo nimeyasikia hapa na mengine yanaonekana basi kauli zetu kwa sababu sayansi nilishawahi kusema tena narudia sayansi ambayo imekuwa duniani kwa miaka
300 hivi inaonesha hisia kunuia na kutenda kwa mwanadamu hasa zile nguvu zinazotoka kwenye moyo wake zinaitwa magnetic force hasa spoken words maneno yanayotumika neno likishatoka limetoka na kipaji chetu cha kusikiliza.

Mheshimiwa Spika, nimeanza na hilo kwa sababu dunia ya leo tunaenda kwenye artificial intelligence. Kwenye diplomasia ya kiuchumi kwenye artificial intelligence yaani mashine zimeanza kufikiri kama binadamu, mashine zimeanza kutoa majawabu kama binadamu na kwenye logic naaanza kufikiria na kwenye logic unaenda kwenye tautology, wale waliosoma hesabu, if and only if na kwenye tautology unaongea nini na nani mahali gani wakati gani halafu hii halafu inaenda kwa kasi kubwa sana. Unaongea nini narudia unaongea nini na nani, mahali gani, wakati gani, halafu hii halafu ndio iliyo nzito zaidi kuliko yote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na kwenye artificial intelligence tunaangalia dunia na Mheshimiwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje yupo hapa. Kwenye diplomasia ya kiuchumi wakati Taifa hili linaasisiwa Mwalimu Nyerere alianza na kanuni ya utu, binadamu wote ni ndugu zangu, hakusema Afrika wote ni ndugu zangu, alisema binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja.

Sasa tukishasema binadamu wote ni ndugu zangu tuchunge sana ndimi zetu hasa kutoa lugha ambazo zinaudhi wengine, tunatoa lugha ambazo zinadhalilisha wengine na hili ni kwetu sote tu. Kwa mfano tukitoa lugha za kukebehi na kujadili mataifa mengine tuangalie lengo la kumi na saba la malengo endelevu ya dunia linazungumzia global partnership, linazungumzia ushirika wa kidunia halizungumzii ushindani wa kidunia. Leo hii tuko humu ndani tunazungumza ushindani wa kivyama badala ya kuzungumza ushindani wa Taifa katika ushirika wa dunia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wakati wa mijadala kama hii na sisi tunaisimamia na kuishauri Serikali. Niishauri tu Wizara ya hasa Mambo ya Nje kwenye suala la global partnership ili yale malengo kumi na sita na lile la kumi na saba la global partnership badala ya kusema mimi unasema sisi, badala ya kusema yangu unasema yetu. (Makofi)

Sasa katika misingi hiyo umimi huu au ubabe huu hautatusaidia sana, lugha ni lugha tu nafasi yetu Tanzania katika mahusiano ya kimataifa, diplomasia yetu ya kiuchumi katika mataifa mengine, tunashauriana namna gani, tunasikilizana namna gani, kwa sababu mataifa yetu ni mataifa huru (a sovereign state). Unakaaje na wenzako kama wametoa kauli mnazungumza kwa lugha ya staha badala ya kutoa lugha tu, labda wakoloni hawa, mabeberu hawa, wamefanya hivi hata tukipiga kelele sana wao wanajibu kwa vitendo na tukiri kwenye artificial intelligence leo hii wenzetu wanaenda kwenye mashine za namna hiyo wakati sisi bado tuna upungufu hata kwenye shule zetu za miundombinu ya vyoo kwa takribani asilimia 60.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo we must think big and we must think globally while we want to have a local solution. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye diplomasia ya kiuchumi kwa mfano nilibahatika mwaka juzi kwenda Israel, tulialikwa na Chuo cha True Man Institute kwenye masuala ya ushirikiano kati ya Afrika na Israel. Waisraeli leo hii wanavuna maji yaliyo safi na salama kwa kutumia hewa angani, lakini dunia ya leo zaidi ya watu bilioni moja hawana maji safi na salama. Sasa ni namna gani mahusianao yetu kwenye hii free market ya dunia ya leo mahusiano yetu ya kuweza kuvuna rasilimali hii knowledge hii katika kuisaidia taifa letu la Tanzania tukiwa wamoja.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano wakati wa Mwalimu mahusiano kati ya Wapalestina na Waisraeli mwaka juzi tulipokuwa kwenye hicho chuo cha True Man Institute tulikuwa na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje ya Marekani akina Poel, wakina Mheshimiwa Raila Odinga, Balozi mmoja wa Israel aliwahi kuwa Kenya akiwa anashughulikia Afrika Masharikia akasema uso mzuri hauitaji urembo. Nanukuu maneno yake; “uso mzuri hauitaji urembo.” Maana yake nini kwamba chema chajiuza, kibaya chajitembeza. (Makofi)

Sasa tukifikiri tukiwa na utulivu mzuri tu, tukaangalia sisi sasa tunatumia namna gani nafasi hii kuvuna teknolojia hii, kuweza kuona namna gani inatusadia katika maji, basi Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje inashirikiana na zile Wizara nyingine zinazohusika tunasimama wote kwa pamoja kama Taifa kwa sababu hili lina maslahi kwa wote kama ni maji ni yetu sote katika majimbo yetu, kama ni suala la umeme ni letu sote katika majimbo yetu, kama ni suala lolote lile sote tunasimama kama Taifa na vita hivi vya kiuchumi tutavishinda tukiwa wamoja kama Taifa la Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nasema hivyo tunakumbuka Zimbabwe ilivyokuwa kwenye hali n zuri tu mwaka 2002 nikiri nilienda Zimbabwe tulitumwa na Rais Mkapa kuangalia uchaguzi wa Zimbabwe, lakini walikuwa wamegawanyika. Tulienda Bulawayo tukaenda Tumbuiza, tukaenda Harare mpaka Victoria Falls sasa wanatumia nafasi ya mgawanyiko ndani ya Taifa ili kutugawa. Sasa tusijaribu kuona kwamba tunafanya tu upande mmoja tufikiri kwa pamoja, tuwe na utulivu kwa pamoja, tuone ni namna gani ya kuweza kuvuka katika hali ya namna hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niishauri Kamati na niiombe Kamati na hasa ya Mambo ya Nje ukiangalia Taifa la India leo hii na teknolijia yao ya afya na vijana wao wanavyojitahidi kwenye afya namna gani mgogoro ulioko kati ya India na Pakistan hasa mambo ya Jammu na Kashmir. Kwa sababu kila mara India wanauliza wao wanataka wafanye mazungumzo yao, sasa Tanzania sisi tunasimamia wapi kwenye mahusiano yetu kati ya Pakistan na India hasa masuala ya Kashmir, halafu tunakuwa na msimamo gani ili sisi wote tunaweza tukafaidi yale mengine ambayo ni makubwa badala ya kutoa lugha tu ambazo sio nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya muda nizungumzie kidogo masuala ya usalama katika Taifa letu. Yako haya mambo yanayoendelea kwenye Taifa letu hata juzi yalitokea mauaji huko Kilimanjaro ambayo lazima tujiulize sote na tutafakari kwa sote kwa pamoja. Nimejaribu kujiuliza maswali yafuatayo kwenye suala la ulinzi na usalama wa taifa letu. Kwanza nitoe tena pole kwa vifo vilivyotoke kule, lakini kwenye masuala ya hivi vikundi mbalimbali tujiulize je, kuna matatizo au vikwazo au changamoto gani katika jamii yetu labda ya kikatiba, kisheria husika na kanuni zake, jamii kujitambua, mifumo yetu ya kitaasisi hasa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama mfano public order (usalama wa raia), public health (masuala ya afya), peace (suala la amani ya Taifa), crowd management na disaster preparedness endapo jambo lolote lile linatokea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na tujiulize kama taifa na hasa Wizara ya Mambo ya Ndani kwa nini haya yote na matakwa yake ya kisheria yanatokea mambo ya namna hii, je, ni maadili yetu ya kitaifa yamemomonyoka, je, elimu ya kimungu ndani ya madhehebu yetu yenyewe yako katika misingi ya namna gani.

Mheshimiwa Spika, tukiwa na tafakuri ya kina sote kwa pamoja tunaamini kwamba tutabaki kuwa pamoja na wakati wa mijadala hasa wakati huu tunashauri Serikali, tunashauriana Wabunge na hasa Kamati tuhakikishe kwamba kipindi cha mwaka kama hiki sisi kama Wabunge yale majukumu makuu manne ya Mbunge tunasimamia kwanza jukumu la kwanza ambalo ni kwa Taifa lako, la pili kwa jimbo lako la uchaguzi yale ya vyama na mengine unaweka pembeni Taifa linakuwa pamoja tunashiriki pamoja, tunajadiliana pamoja, taifa letu litasonga mbele na tumpe upendo mama Tanzania kwa maslahi ya wote.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi uliyonipa. (Makofi)