Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipatia fursa ya kuchangia taarifa za Kamati hizi mbili zilizopo mbele yetu, lakini kwa sababu sijavaa vazi la kidiplomasia nitachangia sekta ndogo ya nishati upande wa mafuta na gesi nikikumbuka nguo nilizokuwa navaa miaka 36 iliyopita wakati nafungua valve.

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Mheshimiwa Waziri. Nilieleze Bunge lako Tukufu kwamba unaweza kuwa na kitu na usijue thamani yake. Kwa watu wanaojua historia ya mafuta nchini wakati watu wanapata mafuta kwa mgao ndiyo utaweza kujua kwamba Wizara ya Nishati leo inafanya kazi iliyotukuka. Nimeisoma vizuri taarifa ya Kamati, inavutia. Tunayo hifadhi ya mafuta ya kutosha miezi mitatu, lakini kipekee hifadhi hiyo imenunuliwa na Private Sector. Ina maana mfumo wa Bulk Procurement unaodhibitiwa na Serikali unaifanya sekta binafsi kuleta mafuta kuwa hapa bila fedha ya Serikali na watu hawawezi kugundua kwamba nchi ina upungufu wa mafuta.

Mheshimiwa Spika, nipongeze suala lingine la bulk procurement ambapo kwa historia, najua hili unalifahamu vizuri; wakati meli zinakuja Dar es Salaam tulikuwa tunaweza kukalisha meli nje tukaingia gharama (demurrage) ya dola 20 mpaka 40. Taarifa ya Kamati inafurahisha, kwamba demurrage charges sasa ni chini ya dola mbili (dola 1.6). Ni jambo zuri sana niwafurahishe wanakamati kwamba muendee hivyo tuweze kwenda kwenye mambo mengine yanayofurahisha.

Mheshimiwa Spika, nitofautiane kidogo na Kamati; kwamba tathmini yao haijatupeleka kwenye malengo ya kuanzisha bulk procurement, pamoja na haya availability of product, affordability na quality ambayo kweli quality tumeiweza hatujaweza kujibu au taarifa yenu haikutueleza. Je, haya mafuta margin yake ni kiasi gani? Mwenyekiti wa Kamati anaelewa kwa sababu mimi ndiyo nilimpokea kazini nikamuonesha dawati na kumfundisha kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Kitandula ni kijana wangu nilimpoke kazini mika hiyo kwa hiyo hii success ugomvi wa kuagiza mafuta uko kwenye ile margin. Je, unapokuwa umenunua margin iko kiasi gani, lakini Mwenyekiti wa Kamati nikueleze haujatueleza mafuta yanayopotea. Ugomvi mkubwa wa Wizara ya Fedha ni mafuta yanayopotea kutoka kwenye meli kuingia kwenye matenki, hili suala kamati yenu haijalijibu.

Mheshimiwa Spika, nimweleze Mwenyekiti wa Kamati kwamba kuna suala tata la floor meter, floor meter inayopigiwa kilele ambayo kimsingi mimi mwenyewe kama mtalaam wa shughuli siiungi mkono, lakini solution ya upoteaji wa mafuta ni kuwa na single receiving tanks. Hili suala tata la single receiving tanks Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati haujalijibu, umekuwa wimbo wimbo wimbo wa kila siku.

Mheshimiwa Spika, jambo moja la kufurahisha niwapongeze Mheshimiwa Waziri kwa kuongeza storage capacity, kwamba leo nchi ina uwezo wa kutunza mafuta lita bilioni 1.3 ambayo matumizi ya nchi inakwenda kwenye lita karibu 3.8 bilioni. Jambo la kufurahisha ni kwamba mafuta ya jirani yetu yanayopita Tanzania ni takriban kiasi hicho cha 1.9 billion litters kwa miezi sita. Maana yake ni nini, wakati una mafuta ya kutumia nchini kwa miezi mitatu una mafuta mengine ya jirani yako yanayopita; ina maana hatuwezi kulala njaa wakati mafuta ya jirani yapo. Kwa lugha ya kawaida huwezi kuwa umemuwekea mwenzako mihogo halafu baba hajatoka kuhemea watoto wakalala njaa, hapana utakula mihogo hiyo halafu kesho yake utakuja urudishie. Kwa hiyo niwapongeze Wizara ya Nishati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini wakati nawapongeza tumeshindwa kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi inayotuelekeza kwamba Dar es Salaam inapaswa iwe trading hub ya mafuta kwa nchi zilizotuzunguka. Kwa masikitiko watu wa Kenya wanatumia bounded warehouse, watu wa Uganda wanatumia bounded warehouse, Rwanda wanatumia bounded warehouse. Maana yake ni nini, kama mafuta yangeletwa yakazuiliwa Dar es Salaam tungefanya re-export. Ina maana kwenye lita zinazopita hapa 1.9 billion kwa miezi sita tungeongeza cha juu tukaweza kuuza nje. Kwa hiyo tunapoteza fursa ambayo ingetuongezea kodi nyingine Mheshimiwa Waziri wa Fedha. Yaani unaongeza make up inaitwa cha juu unaweza kuuza. Niwaeleze, watu kutoka nchi zilizotuzunguka hawapendi kununua kutoka nje. Ndicho kitu nilichokifanya kwenye sekta ya saruji; watu wa Rwanda na Burundi walikuwa wananunua saruji Pakstan lakini viwanda vya saruji vilipochangamka wakaja na malori wakanunua saruji kwetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nahimiza kwamba tutekeleze Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa kujenga storage tanks zile za Tanga, tengeneza bounded warehouse tusimamie ile damping na whatever tuweze kuongeza kile cha juu 1.9 billion litters ukiweka dola moja moja mambo ya kujenga madarasa tunaweza kufanikisha kwa haraka.

Mheshimiwa Spika, nipongeze wizara na TPDC; katika taarifa yenu mliwahi kuzungumza, mlirashiarashia kidogo. Zipo jitihada za TPDC kuanza kutafuta na kuchimba gesi. Si jambo jipya, mmerudi kule tulikoanzia, TPDC katika historia ya kutafuta mafuta imewahi kuchimba visima, Munazi Bay, Songosongo, akina Mzee Kaaya, akina Mzee Barongo walichimba visima na wakakuta gesi. Kwa hiyo jitihada za sasa ni lazima tuziendeleze. Msiwe na wasiwasi, kazi hii ina gharama kubwa. Kupata mafuta, kuchimba mafuta kwa gharama yako ni kubwa lakini failure ni kubwa. Mtachimba visima kwa gharama kubwa na unaweza kuchimba visima hata kumi usipate lakini ukipata ulichokipata ni cha kwako. Kwa hiyo hapo wanaofanya maamuzi lazima mkae chini mtulie. Libya kuja kupata kisima cha mafuta ya kutosha (economic quantity) walichimba visima zaidi ya 50. Kwa hiyo na sisi tunaweza kuchimba visima vingi lakini tukipata tumepata tunaondoa yale mashaka ya kwamba tunaliwa.

Mheshimiwa Spika, Kuhusu Suala la Utafutaji. Suala la utafutaji lina faida nyingi, utafutaji wa mafuta ni shule. Wako vijana wengi wanafanya suala la geology, petroleum chemicals na whatever, hawa vijana tunawapatia nafasi ya kuweza kujifunza hii sekta. Kitu kimoja kilichodokezwa na Kamati ambacho nawaunga mkono, naiomba Serikali yangu ya Chama Cha Mapinduzi muharakishe kufanya maamuzi na kuzipitia PSA ambayo nina hakika Kamati yetu iliwahi kupitia, kuna Kamati ya Gesi iliwahi kupitia; lakini ukisoma mtu yeyote kuna makandokando ambayo kwa sababu ya kupitwa na muda tunaweza kufanya maboresho. Tufanye maamuzi kusudi watafutaji na wachimbaji waanze kuchimba kwa sababu hizi rasilimali haziko Tanzania peke yake, lakini hizi rasilimali zina rasilimali mbadala kwingine.

Mheshimiwa Spika, sehemu nyingine sasa hizi liquefied natural gas si biashara tena, lakini anayekuwahi sokoni anakwenda kukamata mteja, mteja atakayechukuliwa na Mozambique wewe kuja kumtoa Mozambique uuze gesi yako itakuwa ni tatizo. Kwa hiyo naomba Serikali yetu fanya michakato usiku na mchana, pitia hizo PSA, pitia hizo leseni, waite hao watafutaji na wachimbaji watafute. Mimi nina uhakika Mwenyezi Mungu na sisi ametuwekea mafuta sehemu, ametuwekea gesi mahali, ningependa na sisi tuweze kuyafaidi haya mafuta si kwamba wajukuu wetu waje waseme babu zetu walikuwa wazuri, waliishi na mafuta wakayaacha ngoja sisi tuweze kufanya nini, tuweze kuyatumia. Tukiweza kupata mafuta yakaweza kuchochea zile sekta za kilimo na mifugo zikaziunga mkono tutaweza kwenda kwenye uchumi mkubwa haraka sana kuliko tunavyotegemea.

Mheshimiwa Spika, nilizungumze hili wakati nataka kumalizia. Safari yetu ni ya kwenda kwenye uchumi mkubwa, si uchumi wa kati, uchumi wa kati ni kituo. Kwa hiyo ili uende kwenye uchumi mkubwa unahitaji nguvu nyingi, moja wapo ya nguvu ni nishati na nishati yenyewe ni mafuta na gesi ambayo Mwenyezi Mungu alitujalia. Kwa hayo machache naomba niunge mkono hoja, ahsanteni Mheshimiwa Kitandula kwa repoti nzuri.