Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu, leo nami nasherekea kumbukumbu ya siku yangu ya kuzaliwa, natimiza umri wa miaka kadhaa. Kwa hiyo nakushukuru kupata fursa hii, lakini pia namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa umri alionijalia.

Mheshimiwa Spika, nianze suala la Uhamiaji hususan kwa Mikoa ya Lindi na Mtwara. Mpaka kati ya Msumbiji na Tanzania sielewe kuna tatizo gani? Kuna ndugu zetu; ukienda Mtwara kuna watu wanahitwa Wamakonde. Hawa Wamakonde wapo kwenye nchi mbili; wanaotoka Msumbiji na wengine waliopo huku ng‟ambo, Tanzania.

Mheshimiwa Spika, unakuta unapofika wakati wa uchaguzi wa Msumbiji hawa watu wanaletewa masanduku na wanapiga kura kuchagua Rais wa Msumbiji, halikadhalika watu hawa hawa ukienda unakuta wamejiandikisha kupiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, sasa jambo hili ni hatari sana. Namshukuru Afisa Uhamiaji wakati ule wa mchakato wa Serikali za Mitaa, Afisa Uhamiaji wa Mkoa wa Lindi tulishirikiana naye vizuri sana na kuna baadhi walikwenda wakawaondoa kwenye list ya watu waliojiandikisha kwa ajili ya kupiga kura kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kujua kwamba walishiriki kwenye uchaguzi wa Msumbiji. Kwa bahati mbaya, watu wale waliondolewa kwenye daftari la kupiga kura za Serikali za Mitaa lakini wapo wengine kwenye daftari la kudumu la wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba jambo hili lifuatiliwe, hususan Waziri wa Mambo ya Ndani, namheshimu sana kaka yangu Komredi Simbachawene, hayupo lakini jambo hili ni muhimu sana kuhusu suala la uhamiaji. Unajuwa sasa hivi pale mpakani kati ya Mtwara na Msumbiji hali siyo nzuri sana, kumetokea mauaji hivi karibuni, lakini nafikiri kama kuna uholelaholela wa namna ya watu kupita pale, mwingiliano umekuwa wa kawaida sana, yaani huwezi kujuwa kama mtu anavuka anaenda upande wa pili; anaenda Msumbiji au anaingia Tanzania.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na uholela mkubwa sana, inafikia hatua tuliona wakati fulani hapa mwaka uliopita 2019, kuna ndugu zetu kule Tandahimba walipoteza maisha na sijajuwa kama wale watu walishakamatwa au namna gani, lakini ni kwa sababu ya ule mwingiliano. Waziri wa Ulinzi, yupo anafahamu kwamba kuna watu wa Tanzania wanalima Msumbiji na kuna watu wa Msumbiji wanalima Tanzania.

Mheshimiwa Spika, sasa lile suala la mpaka pale, namwomba Mheshimiwa Waziri alichukulie kwa umakini na kwa uzito mkubwa sana. Kumekuwa na uholela sana katika mpaka kati ya Tanzania na Msumbiji kwenye kile kipande cha kule Mkoani Mtwara.

Mheshimiwa Spika, Jambo lingine, pale Jimbo la Mchinga kuna Gereza moja linaitwa Kingurugundwa. Ni Gereza maarufu sana, wale wafungwa watukutu ndio wanapelekwa pale. Kwenye kadhia hii ya mafuriko yaliyotokea Mkoa wa Lindi, hili Gereza sasa hivi kama liko kisiwani vile; na wako mahabusu pale wanatakiwa wapelekwe Mahakamani, lakni takribani sasa karibu wiki ya pili inashindikana.

Mheshimiwa Spika, hata yale maji yakiondoka, barabara ya kutoka pale barabara kubwa kwenye eneo la Mkwajuni kwenda pale Kingulugundwa almost too kilometers, ni ngumu kulifikia. Kwa hiyo, naomba hili Gereza kwa sababu la umuhimu wake huo na haliko mbali kutoka barabara kuu, lakini wamekuwa wakipata shida sana ya usafiri, namna ya kusafirisha watuhumiwa au mahabusu kuwapeleka Mahakamani na hata wale Askari wenyewe, huduma zile za kiusafiri zimekuwa ngumu sana.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine, kumekuwa na malalamiko mengi kwa wananchi ukisikiliza juu ya traffic kubambikia kesi madereva. Jambo hili nalo ni kero kwenye jamii. Tunajadili suala la mambo ya ndani ya nchi, tunaangalia viashiria ambavyo vinaweza vikaleta shida kwenye nchi; suala la ma-traffic kubambikia kesi madereva limekuwa kubwa na wakati wengine hata sisi wengine linatukuta.

Mheshimiwa Spika, unamkuta traffic anakwambia ume-over speed, ukimwambia nionyeshe gari, wengine hawataki na akikuonyesha unakuta siyo gari yako kabisa. Kwa hiyo, hili limekuwa ni tatizo na wamekuwa watu wakibambikiwa na madereva wanalalamika sana kwamba kwa nini tunabambikiwa kesi namna hii? Inaonekana kama ni kitega uchumi cha kukusanya fedha, jambo ambalo kwa kweli siyo nzuri sana. Naelezwa hapa, wakati wengine wanakaa porini wanajificha kwa ajili ya kuchukuwa hizo picha.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo nataka nizungumzie ni kuhusu suala la matamko yanayotolewa na baadhi ya viongovi wa Vyama vya Siasa. Taifa hili letu wote na tunapenda tuendelee na amani hii iliyokuwepo, lakini panapotokea viongozi wanatoa matamko ya kuashiria kama ni uchochezi, wakitoa upande fulani hawashughulikiwi, huoni hata wameitwa Polisi, wakitoa upande mwingine wanaitwa. Jambo hili kwa ustawi wa Taifa letu siyo jema sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimeona juzi huko Arusha Mwenyekiti wa UVCCM ametoa tamko baya sana. Nilifikiri angalau angewahi kuitwa akahojiwa.

SPIKA: Mheshimiwa Bobali, unajua watu wengine wala huna haja ya kupoteza muda. Niko na wewe, sikupingi, yaani wako watu, wewe hebu endelea na mengine tu.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Spika, ahsante, nashukuru Mheshimiwa Spika.

SPIKA: Kwa sababu ni matamko ambayo hakuna anayekubaliana nayo hata robo. Hakuna! Kwa hiyo, tutakuwa kama tunakuza kitu ambacho… mmh!

Nafikiri sisi kama Wabunge, tuko above that.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Okay.

SPIKA: Huo ndiyo ulikuwa ushauri wangu, ahsante.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Spika, nashukuru.

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho nilitaka niongelee dogo tu. Kwa kuwa tunazungumza Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi na furaha kwenye nchi; kuna jambo ambalo linaendelea sasa hivi hasa kwenye mitandao ya kijamii, watu wanalalamika sana juu ya upendeleo wanaopewa timu ya samba. (Kicheko/Makofi)

Eeeh, ndiyo! Marefaree, nilikuwa naomba…

SPIKA: Mheshimiwa Bobali ngoja nikae vizuri. Ngoja nikae sawa sawa, unaweza ukaendelea Mheeshimiwa Bobali. (Kicheko/Makofi)

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Spika, kumekuwa na tendency ya watu watu kulalamika. Mambo haya, wakati timu fulani inapendelewa kulikuwa na viti vilivunjwa pale na wengine walirusha viti pale Uwanja wa Taifa. Ni jambo baya sana. Sasa hili lazima likemewe na Waziri wa Mambo ya Ndani lazima ahakikishe kuna amani. Sisi wote tunapenda furaha.

Mheshimiwa Spika, jana nimelala sikufurahi kabisa kwa sababu siyo Yanga ilifungwa, sikufurahi kwa sababu Timu ya Polisi walichofanyiwa jana is not fair. Kwa hiyo, jambo hili sasa imeonekana kama tabia inataka kukua na wananchi tuna mambo mengi ya kufurahia. Wengine tunapenda mpira, kwa hiyo...

SPIKA: Kuna taarifa unapewa, sijui! (Kicheko)

MBUNGE FULANI: Aah, hapana Mheshimiwa Spika! (Kicheko)

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Spika, kuna taarifa bwana!

T A A R I F A

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wao walipokuwa wanachangia bila kibali, sisi tulikuwa hatusemi. sasa inawauma, wakae watulie tu, ubingwa ni wetu. (Kicheko)

SPIKA: Pokea hiyo taarifa Mheshimiwa Bobali.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Spika, nimeipokea, nakushukuru sana. Ahsante sana.