Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nashukuru kwa fursa ili niweze kuchangia machache. Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia uzima na afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kipekee nipongeze taarifa za kamati zote tatu. Kamati zimesheheni weledi wa kutosha na ushauri ambao sisi tumeupokea kama Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitachangia katika taarifa za kamati mbili. Naomba nianze na Kamati ya Sheria Ndogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Serikali kipindi hiki tumefaidika sana na ushauri ambao umekuwa ukitolewa na kamati hii, maana kuna maelekezo, na sisi kama Serikali tumefanyia kazi ndio maana zile sheria zote ndogo ambazo zilikuwa zikilalamikiwa hapa zamani sasahivi imebaki ni historia. Naomba niipongeze sana kamati ukianzia na Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe wote kwa ujumla wamekuwa na msaada mkubwa sana kwa Wizara yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende kwenye Kamati ya Utawala na TAMISEMI. Kamati hii imekuwa ya msaada mkuba sana. Hata hivyo naomba nijikite katika suala zima ambalo sisi Waheshimiwa Wabunge kwa ujumla wetu; mwanzo lilivyoanza lilikuwa kama lina ukakasi. Ni suala zima la vitambulisho kwa wajasiriamali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kuna ubunifu ambao Mheshimiwa Rais amefanya ni suala zima la kuwatambua wajasiriamali wadogo na kwamba, kupitia wajasiriamali wadogo tutaweza kuwapata mamilionea wengi wa kitanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepata fursa nikimuwakilisha Mheshimiwa Waziri nikaenda Halmashauri ya Kigamboni, kuna wajasiriamali wadogo ambao wamepewa vitambulisho na CRDB kwa kuwatambua imeanza kuwakopesha pasi na riba; hakika pongezi kwa Mheshimiwa Rais ni ubunifu wa hali ya juu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ninaomba nichukue fursa hii kwa Waheshimiwa Wabunge, kama ambavyo tumekuwa tukishauri mambo mazuri basi nitumie fursa hii huko kwetu kwenye majimbo na sisi tuhimize wajasiriamali wadogo waweze kutambuliwa. Na katika fedha ambazo zinapatikana katika hii asilimia 10 ambayo tumekubaliana naomba nipongeze kamati zote ni jitihada za kamati ndio zimesababisha asilimia 10 ikatengwa ambayo inakopeshwa bila riba. Sasa ni vizuri tukaanza kuwatambua wajasiariamali hawa wenye vitambulisho ndio wakawa kipaumbele katika kupatiwa mikopo ambayo haina riba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zimetolewa hoja nyingi, katika hoja moja ni pamoja na suala zima la TARURA; tunashukuru kwa pongezi ambazo zimetolewa, lakini imesemwa hoja kwamba, kiasi cha fedha kwa maana ya asilimia 30 haitoshi. Ni kweli inawezekana ikaonekana haitoshi lakini ni vizuri tukakumbushana Waheshimiwa Wabunge. Mheshimiwa Waziri alivyokuja alitoa ufafanuzi kwamba, kuna mapitio ya formular ya namna ya ugawanyaji wa hiyo asilimia 30 kwa 70. Ninaomba niwaondoe wasiwasi Waheshimiwa pale ambapo utafiti utakuwa umekamilika formular ikaja hakika tunajua kabisa uko uhitaji mkubwa wa kujenga barabara hasa ambazo ziko vijijini. Vilevile lakini tusije tukasahau pale ambapo TANROADS wanajenga ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami pia ni wa gharama kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi ni kwamba, mapendekezo ya Waheshimiwa Wabunge tunayazingatia na Serikali itafanyia kazi ili tuje na formular ambayo itakuwa inazingatia uhalisia na pesa ziweze kwenda kwa mgawanyo uliosahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa ongezi ambazo zimetolewa kuhusiana na suala zima la afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala zima la Afya Waheshimiwa Wabunge wameongelea kuhusiana na Watumishi ambao wanatakiwa waende kwenye Vituo vya Afya na Hospitali zetu ambazo zimejengwa. Naomba tuendelee kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge, Serikali hii ya CCM ambayo sikio lake linasikia kila sauti ambayo inatoka na hivi karibuni ninyi nyote ni mashuhuda kwamba kuna nafasi ambazo zimetangazwa kwa ajili ya ajira ambazo deadline ni tarehe 7 mwezi huu hii yote ni katika kuhakikisha wanaajiriwa Watumishi wa kutosha ili haya majengo ambayo yanajengwa isije ikageuka kuwa white elephant.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala zima la Shirika la Soko Kariakoo kuna michango ambayo imetoka naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge na sisi Serikali tumeliona lakini pia kuna maboresho makubwa sana utendaji wa masoko Kariakoo umebadilika na hivi kwa mara ya kwanza wametoa gawio kwa Serikali jumla ya shilingi milioni kumi ni mwanzo mzuri nakushukuru kwa fursa. (Makofi)