Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

Hon. Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninamshukuru pia Mwenyezi Mungu kwa kusimama hapa mwaka huu wa 2020. Ninapongeza na kuunga mkono kamati zote tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mengi yamezungumzwa na Waheshimiwa Wabunge wenzangu. Jambo kubwa ambalo nawapongeza sana kwa jinsi ambavyo wameweza kuizungumzia asilimia mbili kwa watu wenye ulemavu ambayo ni kazi kubwa pia inafanywa na Serikali yetu. Kipekee kabisa kwa kweli nimpongeze Mheshimiwa Rais wetu pamoja na Serikali yake kwa jinsi ambavyo leo hii miaka minne tunasimama tukizungumza huku tukijidai kwa yale mambo mazuri aliyofanya katika nchi hii kwa kipindi kifupi, haijawahi kutokea na hii ni historia imeandikwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona matunda mazuri, tumeona ni kwa jinsi gani ambavyo Rais huyu amejitoa kwa Watanzania. Pamoja na lawama zote lakini hata siku moja hajawahi kurudi nyuma amesimama katika kile anachokiamini. Kutokana na mazuri anayoyafanya Mheshimiwa Rais ndio maana hata kelele zinakuwepo nyingi na ukiona kwamba unaporusha jiwe ukasikia kuna kelele ujue kwamba, tayari kuna mtu limempata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii Rais wetu tunaona kwamba ni kwa jinsi gani hata hiyo demokrasia ambayo wenzetu wamekuwa wakiizungumzia, na kwa miaka zaidi ya miango sasa miwili sijawahi kuona hiyo demkorasia ambayo wao wanaizungumzia kwa upande wa pili, lakini kwao wenyewe utekelezaji umekuwa ni ngumu. Unapozungumzia jambo wanasema kwanza kabla hujanyoosha kidole kwa mwenzako angalia hivyo vidole vingine inarudi wapi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii tunasimama hapa tangu miaka hiyo na leo hii tuko katika Bunge, tangu tumeanza kumsikia Mheshimiwa Mbowe ni Mwenyekiti na mpaka sasahivi ni Mwenyekiti. Je, hii ni demokrasia gani? Kama si kwamba, ni kuisema upande wa pili wa Chama Cha Mapinduzi ambao ndio wana Serikali? Serikali ambayo inafanya mambo makubwa katika kuwatetea wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wamekuwa wakipinga ndege, lakini leo hii wao ndio wa kwanza kupanda hizo ndege, pamoja na kwamba, wanazipinga hizo ndege na wamekuwa wakizikimbia kamera zisiwarekodi kwa ajili ya hizo ndege. Sisi kama Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi tuna kila sababu ya kujivunia kazi nzuri inayofanywa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Joseph Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa moyo wa dhati ninaomba nimpongeze Waziri wa Mambo ya Nje kwa kazi nzuri aliyoifanya, pamoja na lawama nyingi, lakini umeonesha kwamba, wewe ni mwamba usiotetereka. Sisi kama Wabunge tuna kila sababu ya kumpongeza na leo hii tunajivunia yale ambayo yalikuwa yanapingwa, leo hii tunayo Twiga ambapo Barrick wamebwaga manyanga na hatimaye kuona ni kwa namna gani washirikiane na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi ili Watanzania waweze kufaidika na asilimia 16. Yote hii ni kwa sababu ya Dkt. John Joseph Pombe Magufuli ambaye hababaishwi na hajawahi kuyumba hata siku moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli tuna kila sababu ya kujivunia. Walisema kwamba, hapa sisi tungeweza kuwekewa vikwazo kwa kuvunja mikataba, hakuna mikataba iliyovunjwa, sheria zimeletwa hapa na tumezipitia. Mwaka wa nne leo tuna kila sababu huu mwaka wa tano kujivunia yote yaliyofanywa na Serikali ambayo inaongozwa na Dkt. John Joseph Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanapiga kelele sana, lakini ukweli ni kwamba baadhi yao wamekimbia hata majimbo yao. Sasa unategema nini? Siku zote utavuna ulichopanda, mwaka 2020 tunakwenda kuonesha kwamba Watanzania wanaelewa sasa pumba ni zipi na mchele ni upi. Kwaajili ya kazi nzuri iliyofanywa na Dkt. John Joseph Pombe Magufuli, Wabunge wa CCM wana asilimia kubwa ya kurudi katika Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati mwingine unajiuliza hivi mtu mzima inakuwaje leo anazungumza anasema tutashiriki kikamilifu kwenye huu uchaguzi, lakini dakika za misho maji ya shingo anasema hatushiriki kwenye uchaguzi? Hebu tunaomba safari hii kama kweli ninyi ni wanasiasa mahiri msuse uchaguzi wa 2020.

Mheshimiwa MwenyekitiKazi kubwa itafanywa na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi na wengi wanakwenda kufa kifo cha taratibu. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo ninakushukuru sana. Ninawapongeza sana Mawaziri kwa kazi nzuri wanayoifanya na wao ndio wanaotufanya tutembee vifua mbele. Vituo vingi vimejengwa, barabara tunaona zimetengenezwa; waulize upande wa pili, hawajui hata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nimalizie kwa kusema kwamba, Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi kwa kazi kubwa wanayoifanya, iwe wa Viti Maalum, wa Majimbo, tumeshuhudia ni kwa jinsi gani wanajituma. Ahsante sana.