Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

Hon. Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia taarifa za Kamati zilizopo mbele yetu. Kwa dakika tano ulizonipatia nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa namna anavyotekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Pwani ndiyo mfano mzuri sana kwa namna gani Mheshimiwa Rais ameweza kutekeleza Ilani. Nasema hivyo nikiainisha miradi mitano ya kimkakati ama miradi mitano ya Kitaifa yote inaonekana ama inapatikana ndani ya Mkoa wa Pwani. Tuna mradi wa kufua umeme Bwawa la Mwalimu Nyerere, unapatikana Rufiji Mkoa wa Pwani, tunao mradi wa njia nane ambao unapatikana Kibaha Mkoa wa Pwani, tunao mradi wa ujenzi wa bandari kavu inapatikana Kibaha Mkoa wa Pwani, tuna mradi wa reli iendayo kwa haraka standard gauge ambayo kimsingi pia inapita Mkoa wa Pwani na pia tunao ujenzi wa viwanda unaoendelea takribani kwenye mikoa yote ya Pwani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sina budi kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa hili kubwa analolifanya. Sambamba na hilo, napenda sana kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa ununuzi wa ndege. Napenda tu kusema kwamba muda siyo mrefu, ndani ya mwaka huu tunatarajia kwenye kupokea ndege nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri hapa watu wanashindwa kufungamanisha maisha ya watu pamoja na aspects za uchumi. Wanaposema wananchi hawataki ndege ni kwamba wanashindwa kuainisha ni kwa namna gani ndege zinaweza kuingizia nchi yetu mapato ambayo kimsingi mapato yale yakikusanywa yakiingia kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina, ndiyo yanaenda kulipa Elimu Bila Malipo, ndiyo yanaenda kwenye miradi ya maji na elimu ya juu. Kwa hiyo, sijajua wenzetu wanafeli wapi? Ila nafikiri wanashindwa kuoainisha hivi vitu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ninalopenda kusema, kazi kubwa ambayo Mheshimiwa Rais anafanya na hatuna budi kumpongeza na bado nikuchukulia mfano wa Mkoa huo wa Pwani, ametupatia miradi mbalimbali kwenye Wilaya mbalimbali za Mkoa wetu wa Pwani ya ujenzi za Ofisi za Halmashauri. Tuna ujenzi wa Ofisi ya Halmashauri Kibiti, ujenzi wa Ofisi ya Halmashauri Kibaha, ujenzi wa Ofisi ya Halmashauri Mafia na ujenzi wa Ofisi za Halmashauri Kibaha Vijijini. Kwa sababu hiyo, Mheshimiwa Rais anafanya mambo makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile ujenzi wa Hospitali za Wilaya, Mheshimiwa Rais ametoa shilingi 1,500,000,000/= kwa ujenzi wa Hospitali za Wilaya karibia kwenye Wilaya nne za Mkoa wa Pwani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hayo yote na mengine mengi yanayofanywa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli hatuna sababu ya kushindwa ifikapo Oktoba, 2020. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yamekuwepo hapa malalamiko juu ya uhamasishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, kwamba inasemekana daftari limekuja mwishoni. Daftari hili lilianza nyuma kidogo, liko linaendelea kutoka Mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine. Mkoani kwetu linatarajia kuingia muda siyo mrefu mnamo tarehe 14 mpaka tarehe 20. Serikali imefanya kazi kubwa ya uhamasishaji, lakini suala la uhamsishaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura lina mahusiano ya karibu na ushikaji wa dola. Kwa maana hiyo, kama unataka Serikali ndiyo ikuhamasishie, hakika itakapifika hapo kesho kutwa tutakapoenda kupata ushindi wa kishindo, bado mtabaki kulalamika na Wakurugenzi, bado mtabaki kulalamika na kuibiwa kura, lakini dola inatafutwa, dola inaandaliwa, dola inachakarikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mziki wa Mheshimiwa Magufuli sioni wa kumuingia mpaka sasa. Kuna mambo makubwa ambayo yamefanywa na Mheshimiwa Rais na pengine wenzetu walikuwa wanadhani pengine Mheshimiwa Rais ana-bip, lakini kwa matokeo ya Serikali za Vijiji na Vitongoji, walipoona mziki umekaa vibaya, ndipo walipoona ngoma ngumu na kuomba maridhiano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Naunga mkono taarifa zote tatu. (Makofi)