Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi jioni hii kuwa mchangiaji wa kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwweza siku hii ya leo kuwa na afya njema na kupata muda wa kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Makamu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa. Kwanza naunga mkono maoni ya Kamati na nimpongeze Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati hii kwa uwasilishaji wake mzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuchangia, pia nianze na pongezi. Nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayofanya lakini pia kuzilea ofisi hizi mbili za TAMISEMI na Utumishi na Utawala bora. Wizara hizi mbili kuwa chini ya Mhehsimiwa Rais kuna mafanikio makubwa, pia wateule wake, Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI na Waziri wa Utumishi, kazi wanazofanya kwa kweli wanamuwakilisha vizuri sana Mheshimiwa Rais. Pia Manaibu Waziri wa Wizara zote mbili wanafanya kazi nzuri za kusaidia kwenye Wizara hizi, vilevile Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu, niwapongeze sana kwa kazi nzuri wanayofanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi hizo pia kuna mambo ambayo sisi kama Kamati tulikuwa tumeridhika na Wizara zote mbili kwa wao kukubali maoni ya Kamati. Asilimia kubwa ya mafanikio haya yametokana na maoni ya Kamati yetu. Tuwapongeze Wizara chini ya Mawaziri hawa kukubali ushauri wa Kamati, kwa kweli niwapongeze sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine, nichukue nafasi ya pekee kumpongeza Mheshimiwa Waziri Jafo; hivi karibuni tu, siku mbili zilizopita TAMISEMI walikuwa na kongamano au taarifa ya utekelezaji wa miradi ambayo Serikai ilitoa fedha na miradi hiyo imefanikiwa kwa asilimia 88 mpaka hivi sasa. Kwa hiyo ni imani yangu kwamba ifikapo Juni, kwa fedha hizi zitakazotengwa na zile zilizotengwa nina imani kubwa sana miradi yote itakuwa imekamilika, na sina shaka usimamizi ambao tunao kwenye Wizara hii mambo yote yatakwenda kama tulikusudia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nimpongeze Waziri wa Fedha na Wizara yake na Naibu wake kwa kupeleka fedha TAMISEMI kwa asilimia zaidi ya asilimia 75. Kwanini ninasema hivyo; ni kwamba miradi mingi ya afya imetekelezwa vizuri sana, yote hii ni kutokana na usimamizi mzuri pamoja na umakini katika makusanyo ya fedha ambayo yameweza kuweka rekodi ya pekee kwa maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka sasa tukizungumzia vifo vya mama na mtoto vimepungua kwa sababu zahanati na vituo vya afya vimesogea kartibu. Jana nilikuwa nasikia Mheshimiwa Kiula anasema kwake tayari wameshafanya oparetions za mama mjamzito na wakaokoa mtoto. Sasa kwa hilo nimeona nisisitize kwamba TAMISEMI sasa siyo TAMISEMI ile, TAMISEMI inapaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine nilitaka kusisitiza kwenye Kamati ni kwamba tuna mabasi ya mwendokasi, na kuna wakala ambaye anatarajia kupewa, au tender kutangazwa. Ningeshauri TAMISEMI wajitahidi kwanza Sheria iwepo kabla ya kuplewa mkataba, kwa sababu bila sheria tutarudi tena kusema mikataba mibovu na kadhalika. Kwa hiyo la kwanza niishauri TAMISEMI ihakikishe kwamba sheria inaletwa hapa na inapitishwa ili mambo yaweze kuwa mazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano sasahivi wanasema kwamba mabasi mengi yako pale, wakati wamvua wanapata shida. Hata hivyo, baada ya sisi kufuatilia kwa sababu tayari Kamati yetu ilitembelea kwenye maeneo; si kweli yale mabasi ni mabasi ambayo yalishaharibika. Hata hivyo Kamati yetu iliwashauri kwamba ni vizuri yakaondolewa kwenye eneo ili watu wasijue na wasielewe kwamba ni kila siku mabasi yanjaa maji; si kweli. Ni mabasi ambayo kweli wakati ule maji yalikuwa yanajaa, lakini sasahivi yaliyobaki ni yale ambayo huwezi kuyatengeneza na huwezi kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine, niende harakaharaka, ni suala zima la miundombinu. Kwakweli niipongeze sana TARURA inafanya kazi katika mazingira magumu kwa sababu haina fedha na haina tegemeo. Hizi Wizara mbili zote zina malalamiko Wizara ya Miundombinu wanasema kwamba fedha hiyo haiwatoshi na TARURA wanasema haiwatoshi. Mimi ningeshauri, hizi Wizara zingekaa pamoja, zikae pamoja zituletee nini kinachoweza kufanyika ili Sheria ya TANROADS ibadilishwe ya na TARURA waweze kupata fedha. Kama TARURA wangepata asilimia 40 kazi nzuri wangefanya kwa sababu tumetembelea miradi, wanajitahidi sana pamoja na kwamba hawana fedha. Tatizo kubwa ni kwamba kwa hali ya mvua ya sasahivi kuna matatizo makubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine, niende harakaharaka kwa sababu nina Wizara mbili; Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI tukuombe sana kwa bajeti hii; madeni ya Madiwani ambayo wanadaiwa hatutaki tena kwenye bajeti yetu tuje tukutane nayo. tunataka ikifika wakati wa bajeti ya mwaka huu madeni yote kama ulivyoagiza yale yamekwisha kwa sababu Madiwani wanafanya kazi ngumu, wanakopwa vikao hawalipwi na wana madeni. Kwa hiyo hili suala kwenye Kamati hatutaki tena lirudiwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini si hilo tu, niombe pia kuhusu Shirika la Kariakoo Sheria ile imepitwa na wakati, ni ya tangu mwaka 1974. Wakati ule kulikuwa na watu wachache, sasa Kariakoo si ile ya mwaka 74 iletwe Sheria ifanyiwe marekebisho, lakini kwa upande wa TASAF mpaka hivi leo karibuni walengwa kwa asilimia 30 hawajapatiwa fedha. Sasa, kwa kuwa tunaingia wkenye awamu nyingine ni vizuri asilimia 30 ikamilishwe ili walengwa wote waweze kupata haki yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine, niende harakaharaka, ni kuhusu suala la MKURABITA. Suala la MKURABITA ni tatizo kubwa tumetembelea kwenye Ofisi zao, lakini kwa bahati mbaya hati mpaka leo hazijachukuliwa. Niwaombe Waheshimiwa Wabunge hawa Wabunge wawahamasishe wananchi ambao hati zao ziko kwenye Ofisi wakachukue ili wajue maana ya kwenda kukopea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ningeomba kwa ridhaa yako kwamba wakala wa mafunzo kwa njia ya mtandao TAGLA, lengo la TAGLA kuanzishwa ni kuwawezesha watumishi wa Serikali au watumishi wa umma kwenda kujifunza na hatimaye kutumia mfumo huu wa mtandao ambao sasahivi upo. Kwa hiyo nimwombe Waziri mwenye dhamana ya utumishi ahakikishe kwamba anatoa waraka kwenye halmashauri kuhakikisha watumishi wanapata haki zao na wanakwenda kujifunza haya mafunzo ili kutumia posi vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naunga mkono.(Makofi)