Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. LUCY S. MAGERELI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Naomba nianze mchango wangu kwa kuipongeza Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji, lakini sana sana Mwenyekiti wetu kwa uwasilishaji alioufanya leo ambapo ameleta kitu cha pekee kabisa, ameeleza na mafanikio na shughuli zilizofanywa na Kamati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nisaidie kushangaa na katika kushangaa kwangu mnisaidie na ninyi kushangaa; na tukishashangaa, Maazimio ya Kamati yetu yaweze kuchukuliwa na kufanyiwa kazi.

Mheshimiwa Spika, nina swali la kuuliza, hivi ni kwa nini kilimo au Wizara ya Kilimo isiwe Wizara kipaumbele? Ni kwa nini bajeti ya Wizara ya Kilimo inatolewa kwa shida sana? Kwa nini mpaka leo pembejeo ni shida sana? Kwa nini mpaka leo hatuwezi hata kujitosheleza kwa mbegu tu kwa ajili ya uzalishaji wa kilimo? Kila siku tunazungumza tunasema, kilimo ndiyo uti wa mgongo wa Taifa, kilimo kinaajiri Watanzani wengi, lakini tunayoyafanya kwenye kilimo haya- reflect huo ukweli tunaoujadili kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna mambo ambayo inabidi tu tufike mahali tuyachukulie very serious. Bajeti ya kilimo mpaka leo, kuanzia baada ya yale niliyowaambia mnisaidie kushangaa halafu tuchukue hatua pamoja; Bajeti ya kilimo sasa itengwe ya kutosha halafu wapewe fedha yote kama ilivyoidhinishwa na Bunge. Tuepushe mambo ya mazao yetu kuozea shambani, tuepushe maziwa ya akina mama kuozea huko mashambani wanakoyakamua, twende na mkakati madhubuti wa kuandaa utaratibu ambao mazao ya kilimo yatakuwa processed, moja kwa ajili ya soko la ndani lakini ikiwezekana iwe na kwa ajili ya soko la nje.

Mheshimiwa Spika, kinachoendelea Wizarani, kwa sasa kuna mapitio ya Sera ya Kilimo. Naomba nilete mapendekezo yangu. Kuna suala la kilimo hai, kilimo mseto na kilimo hifadhi. Hili Mheshimiwa Mama Ishengoma amelizungumzia vizuri kwa upana, dakika zangu ni tano tu. Naomba lipokelewe, liingizwe katika sera na litajwe kwenye Sera ya Kilimo kwa kuwa asilimia 96 ya wakulima wa nchi hii ni wakulima wadogo. Kilimo hai, mseto na hifadhi ni kilimo ambacho tukiki-adopt kwa hao wakulima wadogo (peasants) tutamudu kuzalisha zaidi, kutunza ardhi yetu, kuhifadhi rutuba na kulinda mazingira.

Mheshimiwa Spika, niende kwenye suala la mazao ya kilimo na mboga mboga. Unaweza kuona mwenyewe; sasa hivi mazao yetu ya biashara, korosho, kahawa, chai, pamba, yote tunazidi kuserereka kuelekea negative. Basi wakati tukiangalia nini kimetukuta huko, naomba tuhamie kwenye suala la kilimo cha matunda, mboga mboga na maua. Bahati nzuri hiki ni kati ya kilimo ambacho kinaweza kulimwa pia katika ule mfumo wa kilimo hai, hifadhi na mseto, kwa sababu mazao organic yanayozalishwa katika mfumo huo yanapata soko zuri sana kwa nchi za Ulaya kwa maana yanapokuwa exported.

Mheshimiwa Spika, sasa wakati tunajadili kwa nini korosho inatusumbua, kwa nini pamba imeshindwa kununuliwa msimu huu; na bahati nzuri kilimo cha matunda na mboga mboga ni watu private wanafanya; Serikali haijawekeza huko wala hakuna ambacho kimeshafanyika kwa niaba ya Serikai kuwekeza.

Mheshimiwa Spika, sasa kati ya mambo ambayo ni kikwazo kikubwa sana kwenye suala la kilimo cha matunda na mboga mboga ni hizi kodi na tozo. Nina orodha ukurasa wa 11 wa Ripoti ya Kamati mnaweza kuona. Pana tozo na kodi zaidi ya 45. Nilitamani niwasomee, lakini dakika zangu ni tano. Kwakweli katika mazingira haya, maana yake tunawavunja moyo na tuna-discourage aina hii ya kilimo ambacho ni muhimu sana kwa ajili ya maisha yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niende kwenye suala la mifugo, kwa maana ya Wizara ya Mifugo. Tulipata bahati kama Kamatiā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Dakika tano zimekwishapita. Ahsante sana kwa mchango wako Mheshimiwa Lucy.