Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi ili niweze kuchangia kwenye Kamati hizi mbili Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji pamoja na Kamati ya Ardhi na Maliasili.

Mheshimiwa Spika, niwapongeze sana Wenyeviti na Wajumbe wa Kamati zote mbili kwa kufanya kazi yao vizuri na hatimaye kutuletea taarifa hii hapa Bungeni. Pia niwapongeze sana Mawaziri wanaohusika na sekta hizi nne kwa sababu ya kazi wanazofanya tunaona kazi wanayofanya na kwenye maeneo yetu tunaziona.

Mheshimiwa Spika, nataka nizungumzie suala moja tu la ushirika hasa wa mazao. Ushirika ni kitu kizuri na umekuwa kitu kizuri toka wakati wa kupigania uhuru wa nchi yetu. Imekuwa kiunganishi cha watu wetu na hata kwenye nyakati za uhur, Mwalimu Nyerere pamoja na wenzake walitumia ushirika ili kuweza kuwaunganisha Watanzania na hatimaye kudai haki yetu ya uhuru.

Mheshimiwa Spika, pia ushirika umekuwa kitu kizuri kwa sababu umeliletea Taifa hili sifa nyingi sana. Wakati wa miaka ya 1968 Ushirika ulionekana ndiyo chanzo kikubwa na kizuri kwa mapato yanayotokana na mazao. Katika Afrika sisi Tanzania tulikuwa wa kwanza na wakati huo kwa dunia nzima, kwa mambo ya Ushirika sisi tulikuwa namba tatu, baada ya Israel na Denmark. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hii ni kuonesha tu kwamba ushirika ni jambo zuri na jambo tunaloendelea nalo mpaka leo. Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa sababu amelishupalia jambo hili na miaka miwili iliyopita ushirika umefufuka kwenye maeneo yetu. Hata hivyo, nataka niseme mambo machache ambayo ni kikwazo katika kuendelea kukua kwa ushirika.

Mheshimiwa Spika, la kwanza ni uongozi katika ushirika huu. Suala hili la uongozi ni katika ngazi zote za ushirika kuanzia kile Chama cha Msingi kwenda kwenye Wilaya na Mkoa, kuna matatizo ya kiuongozi sana. Hii ni kwa sababu viongozi waliopatikana kwenye ushirika huu ni wale viongozi tuliowarithi kutoka kwenye ushirika ule ambao ulikuwa umeharibika. Wengi wao tumewachukua na kuwaleta kwenye ushirika mpya ambao tumeuanzisha kwa mujibu wa Sheria ya Ushirika ya mwaka 2013. Sasa hawa watu walioko kwenye ushirika sasa hivi walikuwa na matarajio yao kinyume kabisa na matarajio ya ushirika unavyopaswa kuwa. Kwa hiyo, hawa ndio wamekuwa tatizo kubwa kwa sababu wanachojali ni maslahi yao binafsi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa naomba sana, hebu Serikali ijaribu kuangalia muundo wa kiungozi wa ushirika wetu kuanzia ngazi ya chini mpaka mkoa. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji) SPIKA: Ahsante sana Mheshimia Mashimba Ndaki, umeeleweka. (Makofi)

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)