Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nianze kwa kuwapongeza Wenyeviti wakamati zote mbili kwa mawasilisho mazuri ambayo wameyaleta leo hii. Nitachangia Kamati zote mbili kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza, ni suala hili la makampuni ya simu. Makampuni ya simu yamekuwa yakiwaibia Watanzania kwa kiasi kikubwa sana, leo ukiamua kuweka bando lako kwa mfano kwenye simu kwa mfano TIGO, au AIRTEL au VODA ukajiunga bando la wiki moja baada ya dakika tano au 10 au 20 wakati mwingine unatumiwa meseji kwamba bando lako limekwisha, huu ni wizi mkubwa sana ambao unafanywa na makampuni ya simu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Serikali kwamba ihakikishe ya kwamba makampuni ya simu yanafuatiliwa kwa karibu sana kwa sababu yamekuwa yanatuibia Watanzania, yameachwa hovyo wafanye wanavyotaka. Ukiwauliza wanakwamba vigezo na masharti kuzingatiwa hali ya kuwa bando lako haujatumia hata siku tatu bando la wiki linaisha ndani ya masaa 24, wanakwambia ujiunge tena, wizi huu unafanywa na makamouni ya simu. Serikali kama haipo vile Tanzania tunaomba sana kwa sababu Watanzania wengi ni maskini sana, Watanzania anavyochukua Sh.500 yake akaamua kujiunga bando atumie siku halafu anatumia dakika mbili tatu anaambiwa bando lako limeisha, hakuna ufuatiliaji wowote unaofanyika na Serikali. Tunaomba Serikali ihakikishe kwamba inafanya ufuatiliaji wa karibu. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. JACQULINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimpe taarifa mchangiaji anayechangia sasa kwamba ni kweli kabisa anavyosema kwamba haya mashirika ya mawasiliano yamekuwa ni tatizo kubwa kosa mfano shirika la mawasiliano la VODACOM. Mimi nataka nitoe ushuhuda ni jana tu usiku nimenunua kifurushi nikapiga simu nilipopiga simu nikaambiwa kwamba namba unayopiga kwa sasa haipatikani…

MWENYEKITI: Taarifa gani unataka kumpa?

MHE. JACQULINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikazima hiyo simu nikalala asubuhi nachukua simu yangu…

MWENYEKITI: Mheshimiwa…

MHE. JACQULINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naongezea nafafanua

MWENYEKITI: Hapana naomba ukae chini. Mheshimiwa usijibu endelea kuchangia.

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na nakubaliana kabisa na mawazo ya Mheshimiwa Ngonyani kwamba ni kweli kabisa napokea taarifa yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mashirika haya kama ikiwezekana sisi kama Wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi ni lazima tuweke utaratibu ikiwezekana kwa sababu kwa kuwa wizi ni dhambi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wizi haufai na ni kosa la jinai, ikiwezekana tuyachukulie hatua mashirika haya Waheshimiwa Wabunge ikiwezekana tuende mahakamani kuyashtaki mashirika haya ya simu kwa kuwaibia Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu nyingine ni suala la barabara. Sasa hivi Tanzania kwa kiasi kikubwa miundombinu inajengwa barabara nyingi zinajengwa lakini tatizo la barabara hizi zinazojengwa zinachukua muda mrefu sana kumalizika. Sasa tatizo ni nini tunaomba Serikali itueleze kwa nini barabara nyingi ambazo ni muhimu zimeanzishwa kujengwa Tanzania, lakini barabara ambayo inapaswa ikamilike kwa mwaka mmoja au kwa miezi sita au miaka miwili inachukua miaka minne mpaka miaka mitano barabara hazikamiliki. Kwa hiyo, niiombe Serikali kwamba fedha ambazo zinakusanywa kwa ajili ya barabara zipelekwe kwa wakati kwa wale wakandarasi ambao wamepewa kujenga hizi barabara ili barabara ziweze kukamilika kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano barabara ya Uchumi kule Kusini ambayo inaanzia Mtwara Mijini inafika Tandahimba, Newala mpaka Masasi muda wake umemalizika sasa hivi ni zaidi ya miaka miwili ile barabara haiajakamilika. Ukiwauliza hawa wakandarasi wanasema fedha wanachelewa kupelekewa, waki- raise kitu kinachoitwa certificate wakipeleka Wizarani kwa wahusika, wanachelewa kupata fedha zao ili waweze kuendelea na ule ujenzi. Tunaomba sana barabara hizi kwa sababu Serikali imeamua kujenga barabara, zikamilike kwa wakati, wakandarasi, wazabuni wapewe fedha zao kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilizungumza hapa ndani ya Bunge hili kwamba kuna barabara muhimu sana ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambazo Serikali ni lazima izijenge barabara hizi zikiwemo barabara zile za mipakani. Leo hii mpaka wa Kusini kuna barabara ya Ulinzi ambayo inazunguka Mkoa mzima wa Mtwara inafika Mkoa wa Lindi mpaka Mkoa wa Ruvuma, barabara ambayo ilitumika wakati ule wa kulinda wale ambao walikuwa ni wavamizi wanaotoka Msumbiji, wale Makaburu leo hii ile barabara imesahaulika sana. Tumekuwa tunazungumza ndani ya Bunge hili kwamba barabara za ulinzi ni barabara muhimu sana kwa ulinzi wa Taifa letu hili. Barabara inayotoka Mtwara kuelekea Mikoa hii ya Kusini yote hii inayozunguka Mto Ruvuma, tunataka Serikali kwa kuwa imehaidi ndani ya Bunge hili kwa muda mrefu kwamba itakuja kujenga barabara hii, tunaomba itekelezwe hii ahadi, barabara ile ijengwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara pia ambayo inatoka Dar es Salaam kuelekea Mikoa ya Kusini ni barabara ambayo miaka ya karibuni iliweza kujengwa na Serikali lakini barabara ambayo kutokana na maroli yanayosafirisha cement kutoka Kiwanda cha Dangote kuja Dar es Salaam kwenye soko kuu ile barabara inaharibika sana na inachukua muda mrefu sana kurekebishwa. Barabara ya Kibiti – Lindi, ni barabara ambayo Serikali inarekebisha lakini kwa utaratibu sana, maeneo mengi imebomoka. Tunachoitaka Serikali tuliwahi kuzungumza hapa hivi sasa Serikali imejikita kujenga meli kule kwenye Maziwa Makuu kupitia ile Taasisi za Serikali Marine Service, tunaomba Serikali itanue wigo itengeneze meli ziweze kutumika kwenye bahari ya Hindi kwa ajili ya kusafirishia mizigo ya cement kutoka Mtwara kuelekea Dar es Salaam na kwingineko duniani. Tunavyoendelea kutumia barabara moja barabara ya Kibiti - Lindi barabara inaharibika sana na Serikali inatumia fedha nyingi sana kurekebisha na kuweka viraka viraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu Mwenyezi Mungu ametubariki Tanzania tuna Bahari ya Hindi na bahari yenyewe ina kina kirefu kuanzia pale Bandari ya Mtwara, Serikali neno Marine maana yake ni bahari lakini leo hii imejikita kujenga meli katika Maziwa Makuu kana kwamba sisi hatuna bahari hapa Tanzania. Kwa hiyo niiombe Serikali kwamba iweke mpango wa makusudi kabisa wa kununua meli mbalimbali ambazo zitasafirisha mizigo ya cement na mizigo mingine kutoka Ukanda ule wa Kusini kuja Dar es Salaam na kuelekea duniani mpaka huko Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hili Bandari ya Mtwara imekuwa inarekebishwa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)