Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kwanza niipongeze Serikali kwa kazi ambayo inaendelea kufanya hususan kwenye mambo ya masuala ya miundombinu, lakini nataka nichangie kwenye Sekta ya Miundombinu. Katika Jimbo la Segerea kuna wananchi ambao wanadai fidia tangu mwaka 1997, wananchi ambao walipisha Airport Terminal Three, hao wananchi mpaka sasa hivi hawajalipwa, kwa hiyo naiomba Serikali kwa sababu tuko sasa kwenye Bunge la mwisho ili iweze kuangalia ni jinsi gani inaweza ikatoa tamko au ikawalipa hawa wananchi kwa sababu imekuwa ni muda mrefu sana na kila siku tukisimama hapa tunaongelea kuhusu hao wananchi. Pia nimekuwa nikifuatilia bajeti zinavyotoka nione hata kama kuna bajeti wamepangiwa kwa ajili ya malipo yao sijawahi kuona bajeti yoyote katika hii miaka miwili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka niiulize Serikali, je, ni lini sasa itawalipa hawa wananchi kwa sababu nimekuwa hapa huu unaenda mwaka wa tano lakini nimekuwa nikichangia kila mwaka kuhusiana na hawa wananchi, lakini hawajaweza kulipwa. Naomba sana Kamati ya Miundombinu pamoja na Mawaziri wote ambao mmoja mmoja wameshawahi kufika kwenye Jimbo langu na wakafanya mikutano na wakawaahidi hawa wananchi kwamba watarudi kwa ajili ya malipo yao. Sasa umefika wakati wa kuwalipa hawa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ambacho nataka kuchangia ni kuhusiana na miundombinu ya barabara. Tunajua watu woe kwamba Mkoa wa Dar es Salaam kwa sasa kutokana na mvua ambayo inaendelea miundombinu ya barabara imeharibika sana na Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na kwamba sio Makao Makuu ya Nchi lakini pia ni mji maarufu na ndio mji ambao unaingiza kipato kikubwa katika Nchi ya Tanzania. Sasa hivi kwa Mkoa wa Dar es Salaam miundombinu yake ni mibovu sana. Nataka niishauri Serikali tukisema tu kwamba tuangalie bajeti ambayo tuliipitisha 2019/2020 ambayo ndio ikatengeneze ile miundombinu, bajeti haitoshi kwa sababu tumeshaongea sana na watu wa TARURA wanataka kufanya kazi lakini hawana bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nina ushauri kwa Serikali, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri wa Fedha jana alituambia kwamba, wanapanga asilimia moja ya bajeti kwa ajili ya majanga na kwa tafsiri yangu kwamba majanga sio tu lazima watu wafe, majanga ni kama haya yaliyotokea sasa hivi miundombinu ya barabara mibovu lakini pamoja na watu wamepata maafa mengi sana kuhusiana na mvua. Sasa asilimia moja ukisema nusu ya hiyo asilimia moja ni bilioni 30. Sasa kama tukipewa bilioni 15 sisemei kwa Jimbo la Segerea peke yake, lakini nasemea kwa Mkoa wa Dar es Salaam ili waweze kurekebisha hiyo miundombinu ambayo imeharibika, kwa sababu kwa kawaida, kama nilivyosema tukisema bajeti ambayo iliyopangwa 2019/2020 TARURA hawana pesa hizo. Sisi kama Wabunge au mimi kama Mbunge nimekuwa niliongea sana na watu wa TARURA kuhusiana na miundombinu ambayo imeharibika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano kwenye Jimbo langu kuna barabara kama sita hivi hazipitiki kabisa ukianza na ile barabara ya Vingunguti ambayo inatokea Vingunguti Mataa mpaka Barakuda, hiyo barabara haipitiki kabisa na watu hawataki kupitisha magari yao kwa sababu ina mashimo makubwa na watu wanaenda kujaa kwenye hii barabara ya Tabata. Sasa barabara hii ya Tabata utakuta foleni kuanzia saa moja mpaka saa nne na ndio maana inasababisha hata uchumi kushuka kwa sababu watu wanakaa muda mrefu barabarani badala ya kuwa makazini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama Serikali itawaaachia tu TARURA kwamba ndio wenyewe wawe waendelee na hii kwa ajili ya kurekebisha hizi barabara naomba sana Serikali iwaongezee TARURA pesa na kila siku nimekuwa nikisimama hapa naomba TARURA waongeze bajeti kwa sababu hali ya mijini kutokana na miundombinu na barabara zetu ni chakavu na hazijafanyiwa matengenezo kwa muda mrefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha kutokana na hiyo bajeti hiyo aliyosema kwamba kuna asilimia moja ambayo anaiweka, aweze kuwapa watu wa TARURA ili waweze kufanya marekebisho yaliyotokea Dar es Salaam nzima au Tanzania kote mvua inakonyesha. Kwa hiyo, naomba sana kwenye masuala ya miundombinu kwa sababu mjini sasa hivi pamekuwa hapafanyiki kitu chochote sababu ya foleni. Kwa hiyo nimwombe sana Mheshimiwa Mwenyekiti…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. (Makofi)