Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuchangia hutoba hizi za Kamati mbili. Awali ya yote kama Mjumbe wa Kamati ya Miundombinu nataka nichukue nafasi hii kumpongeza Mwenyekiti wetu wa Kamati kwa kuiongoza vyema Kamati ya Miundombinu Kamati ambayo inaongoza kwa upana kwa maana ya sekta nyingi tunazozisimamia, lakini kwa usimamizi wake mahili ndiyo tumeweza kufanikiwa kuleta haya mafanikio ambayo tunayaona leo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais ambaye anaposema kwamba anataka kuelekea kwenye nchi ya viwanda ni kwamba alijua jambo kubwa sana ambalo anatakiwa kulifanya ni kuuwisha miundombinu na ndiyo maana amewekeza sana kwenye upande wa miundombinu hakuna mtu ambaye hajui ni kwa namna gani nchi yetu sasa hivi kwa upande wa miundombinu hasa ya barabara, viwanja vya ndege, bandari zote hizi zimeenda kufanyiwa kazi na kazi yakiufanisi kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukizungumzia hata huko ziwa Victoria ziko meli mpya zimejengwa na zile za zamani zimekarabatiwa. Lakini hii yote ni katika kuimarisha miundombinu, kuimarisha miundombinu huko ambako kutaelekea kuimarisha uchumi wa Taifa letu. Juhudi hizi kubwa ambazo zinafanya na Mheshimiwa Rais na wananchi wote tunamuunga mkono zipo kasoro mbalimbali ambazo tunakiwa tuzichangie na tuziseme ili Serikali nao waweze kuchukue hili waweze kulifanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, liko suala limezungumzwa na Mheshimiwa Mtaturu suala la TPA, kwa kweli Mheshimiwa Rais amewekeza sana TPA, ameingiza fedha nyingi sana TPA kwa maana ya kuwataka kuimarisha bandari zetu ili hatimaye tuweze kuinua uchumi wetu. Vilevile alienda mbali sana akaonda ukaletwa Muswada, Serikalini tukaletwa Muswada tukaunda hii Taasisi ya TASAC kwa nia hiyo hiyo ya kuimarisha au kuondoa sintofahamu iliyokuwa inapatika kule bandarini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, chombo hiki TASAC tumekiunda kazi zinazofanywa na TASAC sasahivi ni kazi ambazo zilikuwa zinafanywa na watu zaidi ya 2000 huko nyuma, wdau mbalimbali wa sehemu ya bandari. Jambo hili limeipa ugumu sana TASAC kiasi kwamba sasahivi tumezua tatizo jingine kubwa zaidi kwenye sekta ya bandari; tatizo la ucheleweshaji wa mizigo bandarini kama ambavyo aliyetangulia kusema ameshalisema kwamba tayari tumeanza kupoteza wateja wadau mbalimbali wameaza kuamisha mizigo yao kutoka kwenye bandari yetu lakini kikubwa zaidi siyo utendaji mbaya wala uwe sifa ya zaidi ulikuwepo wizi na vitu vingine vya ulaghai wizi mdogo mdogo. Sasa hivi wizi kule hamna wafanyakazi wa bandari, lakini tatizo kubwa linakuwa manpower ya TASAC haiwezi kumudu mzigo uliko pale bandarini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, na naishauri Serikali ukisikia watu wanasema sana ujue kuna jambo hata kwenye hali ya kawaida hapa ukienda barabara ukikuta watoto wanacheza kwenye jalala hebu chukua muda kaa uwasikilize, wasome utajifunza tu. Sasa hizi kilele zinazopigwa hizi pamoja na kwamba wale wanaopiga kelele huko nyuma walishachafuka wanamajina mbalimbali, lakini hebu tuwaangalie hebu twende ndani tuangalie kuna nini kabla hatujaingia kwenye tope zaidi, niliona niliongele hili ili serikali nao mlichukue kwenye Kamati tumelijadili sana, lakini naomba kwa usisitizotu naomba TASAC bandari tuangalie utendaji wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ushauri wangu mwingine kwa upande wa Serikali suala la upembuzi yakinifu wa miundombinu mbalimbalui. Ushauri wangu suala la upembuzi yanikifu uendane na uhalisia, tunayo mikiradi mingi ya muda mrefu imeshafanyiwa upembuzi yakinifu lakini kuna miradi mengine leo inafanyiwa upembuzi yakinifu kabla ile miradi ambayo tumefanya umbembuzi yakinifu mwanzo bado haijakamilika. Kwa mfano barabara ya Nachingwea kwenda Masasi kilometa 45 imefanyiwa upembuzi yakinifu mwaka 2014, lakini barabara ile mpaka leo haijapatiwa fedha za kujenga, tangu 2014 mpaka leo 2020 tumeshafanya upembuzi yakinifu barabara ngapi kabla ya ile; mtaona kwamba bado tulikuwa tunaendelea kufanya umbembuzi yakinifu wakati barabara ambazo tayari tulishazifanyia upembezi yakinifu bado hatujazipatia fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ushauri wangu kabla hatujaanzisha miradi mingine hebu tuangalie ile miradi ambayo tayari tumeshafanyiwa upembuzi yakinifu inapatiwa fedha na hatimaye kujengwa kiwango cha lami. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye bajeti iliyopita mfano mwingine kwenye bajeti iliyopita kwenye Jimbo langu la Liwale pale kuna barabara yetu ile Nangurukuru Liwale imeshatolewa fedha za umbembuzi yakinifu, lakini matarajio wananchi wetu tukiwaambia kwamba barabara yetu tayari imeshafanyiwa upembuzi yakinifu ni mategemeo yao kwamba baada ya mwaka mmoja mwaka wa pili, barabara hiyo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tunapowaridhisha wananchi kwamba barabara hii tumeshafanyia upembuzi yakinifu halafu tukachukua miaka 10 bado haijajengwa tunaleta sintofahamu nyingine kwa hawa wananchi ambao tunakwenda kuwasimamia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine naomba niliongelee kuhusu TAZARA, Sheria ya uundwaji wa TAZARA wakati ule TAZARA inaundwa wa Zambia walikuwa wanaihitaji sana, ukiangalia hali ya jiografia kule Msumbiji na Malawi ilikuwa hakuko shwari. Kwa hiyo, TAZARA walikuwa wanahitaji sana hii reli ya TAZARA, lakini miaka hii ya karibuni naomba niiambie Serikali…

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Zuberi

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwani dakika ngapi?

MWENYEKITI: Muda wetu ndiyo huo.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono mia kwa mia. (Makofi)